Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Waziri wa afya Maendeleo ya Jamii jinsia wazee na watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu, ameiagiza timu ya uendeshaji wa huduma za afya ya mkoa wa Rukwa, kusimamia utendaji wa vituo vyote vya kutolea huduma ya afya ili kudhibiti takwimu zisizokuwa sahihi, ambazo zinasababisha bajeti ya dawa isiwe halisi na kuendelea kuwepo upungufu mkubwa wa dawa.
Waziri huyo Ummy Mwalimu akiongea kwenye kituo cha afya cha Matai wilayani Kalambo, ameshangazwa kuona menejimenti ya kituo hicho cha afya ambacho hivi sasa kinatumika kama hospitali ya wilaya hiyo, inakuwa haijui kwa uhalisi bajeti ya dawa, na huku wakiendelea kupata bajeti ya kiwango cha kata kwa idadi ya watu elfu tatu, wakati sasa matai ni makao makuu ya wilaya na idadi ya watu ni zaidi ya 10,000 jambo ambalo haliendani na upatikanaji wa dawa.
Nao baadhi ya viongozi wa wilaya hiyo akiwemo katibu tawala Bw. Frank Sichalwe, wamemueleza waziri huyo wa afya kuhusu utendaji wa bohari kuu ya dawa MSD kanda ya Mbeya, kuwa mara nyingi wamekuwa wakileta dawa nyingi ambazo tayari zinakaribia kuisha muda wa matumizi, na kwamba wilaya inakabiliwa na tatizo kubwa la kutokuwa na gari la wagonjwa kabisa.
Chanzo: ITV
Waziri huyo Ummy Mwalimu akiongea kwenye kituo cha afya cha Matai wilayani Kalambo, ameshangazwa kuona menejimenti ya kituo hicho cha afya ambacho hivi sasa kinatumika kama hospitali ya wilaya hiyo, inakuwa haijui kwa uhalisi bajeti ya dawa, na huku wakiendelea kupata bajeti ya kiwango cha kata kwa idadi ya watu elfu tatu, wakati sasa matai ni makao makuu ya wilaya na idadi ya watu ni zaidi ya 10,000 jambo ambalo haliendani na upatikanaji wa dawa.
Nao baadhi ya viongozi wa wilaya hiyo akiwemo katibu tawala Bw. Frank Sichalwe, wamemueleza waziri huyo wa afya kuhusu utendaji wa bohari kuu ya dawa MSD kanda ya Mbeya, kuwa mara nyingi wamekuwa wakileta dawa nyingi ambazo tayari zinakaribia kuisha muda wa matumizi, na kwamba wilaya inakabiliwa na tatizo kubwa la kutokuwa na gari la wagonjwa kabisa.
Chanzo: ITV