BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
08 October 2012 | Mwananchi
SERIKALI imeipongeza Kampuni ya African Barrick Gold (ABG) kwa kuleta manufaa makubwa kwa taifa kutokana na uwekezaji unaoendelea kufanywa na migodi yake nchini katika nyanja mbalimbali ukiwamo uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii.
Kampuni ya ABG inamiliki migodi minne ya dhahabu nchini -- Bulyanhulu, North Mara, Buzwagi na Tulawaka -- na ndiyo kampuni kubwa kuliko zote kwenye sekta ya madini.
"Nimejifunza mambo mengi sana baada ya kutembelea mgodi wa North Mara," alisema Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele, baada ya kufanya ziara ya mgodi huo wa ABG ulioko Wilaya ya Tarime, mkoani wa Mara.
Katika ziara hiyo, Masele pamoja na Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Charles Kitwanga, walitembelea miradi mikubwa ya jamii ambayo inatekelezwa na mgodi huo kwenye sekta mbalimbali ikiwamo elimu, maji na afya.
Masele alisema kuwa mgodi wa North Mara kihistoria umekuwa na matatizo ya uhusiano na jamii inayoizunguka, lakini hatua kubwa zimepigwa sasa kuboresha uhusiano na vijiji vinavyozunguka mgodi huo.
"Mimi binafsi, bungeni nimesikia pale wabunge wa huku wakilalamika kwamba kuna shule za msingi ziko jirani sana na mgodi. Kazi za mgodi zinapoendelea, ile milipuko inakuwa ikiwaathiri wanafunzi," alisema.
"Lakini leo nimetembelea shule ambayo inatakiwa kujengwa ili kuhamisha ile ambayo inaathiriwa na shughuli za mgodi. Nimejionea kazi ambayo inaendelea pale. Wakandarasi wako saiti wanajenga hizo shule."
Masele alisema kuwa kipindi cha nyuma kulikuwa na tatizo la wanafunzi kukaa chini katika shule zilizopo katika maeneo hayo ya mgodi, lakini mgodi wa North Mara sasa unatekeleza mradi kabambe wa kuzipatia shule hizo madawati.
"Nimejionea kwamba mgodi umeweza kutekeleza ahadi ya kuweka madawati katika shule zote ambazo zinazunguka mgodi na wanafunzi wamekaa kwenye madawati," alisema.
Hivi karibuni, mgodi wa North Mara ulitoa msaada wa zaidi ya madawati 1,000 kwa Shule za Msingi za Wilaya ya Tarime ambazo zinazunguka mgodi huo.
SERIKALI imeipongeza Kampuni ya African Barrick Gold (ABG) kwa kuleta manufaa makubwa kwa taifa kutokana na uwekezaji unaoendelea kufanywa na migodi yake nchini katika nyanja mbalimbali ukiwamo uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii.
Kampuni ya ABG inamiliki migodi minne ya dhahabu nchini -- Bulyanhulu, North Mara, Buzwagi na Tulawaka -- na ndiyo kampuni kubwa kuliko zote kwenye sekta ya madini.
"Nimejifunza mambo mengi sana baada ya kutembelea mgodi wa North Mara," alisema Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele, baada ya kufanya ziara ya mgodi huo wa ABG ulioko Wilaya ya Tarime, mkoani wa Mara.
Katika ziara hiyo, Masele pamoja na Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Charles Kitwanga, walitembelea miradi mikubwa ya jamii ambayo inatekelezwa na mgodi huo kwenye sekta mbalimbali ikiwamo elimu, maji na afya.
Masele alisema kuwa mgodi wa North Mara kihistoria umekuwa na matatizo ya uhusiano na jamii inayoizunguka, lakini hatua kubwa zimepigwa sasa kuboresha uhusiano na vijiji vinavyozunguka mgodi huo.
"Mimi binafsi, bungeni nimesikia pale wabunge wa huku wakilalamika kwamba kuna shule za msingi ziko jirani sana na mgodi. Kazi za mgodi zinapoendelea, ile milipuko inakuwa ikiwaathiri wanafunzi," alisema.
"Lakini leo nimetembelea shule ambayo inatakiwa kujengwa ili kuhamisha ile ambayo inaathiriwa na shughuli za mgodi. Nimejionea kazi ambayo inaendelea pale. Wakandarasi wako saiti wanajenga hizo shule."
Masele alisema kuwa kipindi cha nyuma kulikuwa na tatizo la wanafunzi kukaa chini katika shule zilizopo katika maeneo hayo ya mgodi, lakini mgodi wa North Mara sasa unatekeleza mradi kabambe wa kuzipatia shule hizo madawati.
"Nimejionea kwamba mgodi umeweza kutekeleza ahadi ya kuweka madawati katika shule zote ambazo zinazunguka mgodi na wanafunzi wamekaa kwenye madawati," alisema.
Hivi karibuni, mgodi wa North Mara ulitoa msaada wa zaidi ya madawati 1,000 kwa Shule za Msingi za Wilaya ya Tarime ambazo zinazunguka mgodi huo.