Waziri Ummy (TAMISEMI) ashtukia Halmashauri ya Hai kutumia visivyo pesa za Serikali

mirindimo

JF-Expert Member
Nov 2, 2009
821
1,337
FC8F05D8-44BC-4CF3-9029-566D4C5B6893.jpeg

7AF9C2FB-AB0C-46F0-A566-95F0B2D1E5C4.jpeg
O
Hai DC, tumeleta milioni 50 kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Chemka.Ujenzi umeanzishwa kwa nguvu za wananchi. Sijaridhika na matumizi ya fedha tulizoleta.

Wananchi wanasema jengo hili wameezeka kwa nguvu zao. Wataalam wameeleza wametumia pesa za Serikali! Nimemtaka DC kuchunguza.
 
Matokeo ya kuongoza kila kitu kutoka Dodoma. Hata mambo madogo kama ujenzi wa zahanati mpaka waziri afuatilie? Wakiambiwa inahitajika katiba mpya itakayowapa wananchi uwezo wa kijisimamia wenyewe kwenye maeneo yao wanauchonga mwingi. Bila kufumua system ya utawala na kusuka upya ni bure. Mnatwanga maji kwenye kinu.
 
Kama tuu ulikuwa hujui take it from me. Pesa iliyoingizwa kwenye mashule mbalimbali nchini bodi za shule na kamati za ujenzi zimeelekeza izo fedha kwenye maboma au miradi ilikuwa imekwama au ipo kwenye hatua za mwisho na ripoti wanaandika tumejenga kwa fedha za mhe RAIS ilinihali miradi iliyokuwepo ilifadhiliwa na nguvu za wanainchi au wahisani wengine. Hii inji imejaaa majanja majanja sana sio madiwani sio wabunge wala wakurugenzi mengi ni mapigaji tuu.
 
Vikauli kama hivi vya kumilikisha viongozi fedha na miradi kama vile ni ya kwao binafsi ndio huleta matatizo baadae. Mkianza' kusema fedha ya Ummy' tayari mnawajengea watu wa hali ya nchi mtazamo wa kuwa si fedha zao hivyo haziwahusu kupelekea kutokuhoji hata zikiliwa.
Sema fedha ya umma utaeleweka, Ummy ni kibaraka tu wa kuwakilisha fedha hizo.

Kurudi kwenye mada, fedha gani ya serikali ilishawahi tolewa na ikatumika kwa kusudio lake? Kuliwa kwa fedha hii ni muendelezo tu kutoka walioko juu mpaka chini.
 
Madarasa,zahanati na vingine vilishajengwa kwa nguvu za wananchi,hela zimemwagika,kwanini wasiziandikie uongouongo.Kwa mama ni kupiga tu.
 
Back
Top Bottom