chakii
JF-Expert Member
- Sep 15, 2013
- 19,666
- 22,674
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema sababu ya kutotangaza mwenendo wa ugonjwa wa Corona ni kutokana na maboresho yanayofanyika kwenye Maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii, ambapo kuna marekebisho yanafanyika na ndani ya siku chache marekebisho yatakamilika na watatoa taarifa
Waziri Ummy ameeleza hayo leo wakati akizindua mfumo wa mawasiliano wa huduma kwa wateja katika Wizara hiyo ambapo amesema itasaidia wananchi kupata taarifa sahihi kwa haraka zaidi.
Aidha Waziri Ummy amesisitiza kuwa vifo vinavyotokana na Corona vipo na kesi za maambukizi zipo, hivyo wananchi wanatakiwa waendelee kuchukua tahadhari ili kuepuka kuambukizwa huku akiwataka kufuata taarifa sahihi na kuacha kujawa na hofu.