Chimo
JF-Expert Member
- Aug 31, 2008
- 714
- 360
Kwako dada yangu Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, haitoshi na haitatosha kukuelezea mabaya na maovu yanayotokea kwenye kituo cha afya Igoma, Mwanza.
Naweza kukesha na kuandika mabaya hayo siku mbili au tatu na nisimalize yote.
Kwa ufupi, bora kituo hicho kifungwe kinaitia aibu serikali na Wizara yako.
Kuanzia mlinzi wa getini mpaka wauguzi ni wanyanyasaji, watesaji na wauaji na hawapaswi kuendelea kuwepo uraiani, walitakiwa wawe Butimba gerezani.
Imagine mimi ni dereva nilikodishwa tu kupeleka mgonjwa kwa muda wa dakika 20 ila niliyoyaona nililia nikasamehe na nauli.
MUUGUZI MKUU WA WILAYA YA ILEMELA
MGANGA MKUU WA WILAYA YA ILEMELA
MGANGA MKUU WA MKOA WA MWANZA
Ni AIBU KABISA!
Mlinzi wa getini, mwanamke, anatukana wagonjwa anafukuza wajawazito vitandani anagoma kufungua getini, mgonjwa mahututi yupo kwenye bodaboda, ana amri zaidi ya mkuu wa kituo cha afya - Aibu! Aibu! Aibu!
Inasikitisha sana Waziri, hizo ni pesa zetu wananchi tunalipa kodi ya kila aina; serikali yako ituhudumie kwanini mnashindwa kuweka utaratibu mzuri kwa vituo vya umma ilihali tunalipia huduma hizo? Ya Igoma haya tofauti na Hospital ya Mkoa Sekou Toure.
Sent using Jamii Forums mobile app
Naweza kukesha na kuandika mabaya hayo siku mbili au tatu na nisimalize yote.
Kwa ufupi, bora kituo hicho kifungwe kinaitia aibu serikali na Wizara yako.
Kuanzia mlinzi wa getini mpaka wauguzi ni wanyanyasaji, watesaji na wauaji na hawapaswi kuendelea kuwepo uraiani, walitakiwa wawe Butimba gerezani.
Imagine mimi ni dereva nilikodishwa tu kupeleka mgonjwa kwa muda wa dakika 20 ila niliyoyaona nililia nikasamehe na nauli.
MUUGUZI MKUU WA WILAYA YA ILEMELA
MGANGA MKUU WA WILAYA YA ILEMELA
MGANGA MKUU WA MKOA WA MWANZA
Ni AIBU KABISA!
Mlinzi wa getini, mwanamke, anatukana wagonjwa anafukuza wajawazito vitandani anagoma kufungua getini, mgonjwa mahututi yupo kwenye bodaboda, ana amri zaidi ya mkuu wa kituo cha afya - Aibu! Aibu! Aibu!
Inasikitisha sana Waziri, hizo ni pesa zetu wananchi tunalipa kodi ya kila aina; serikali yako ituhudumie kwanini mnashindwa kuweka utaratibu mzuri kwa vituo vya umma ilihali tunalipia huduma hizo? Ya Igoma haya tofauti na Hospital ya Mkoa Sekou Toure.
Sent using Jamii Forums mobile app