Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,261
Dar es Salaam. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, Watoto na Walemavu, Ummy Mwalimu amesema kuwa amebaini katika Taasisi ya Mifupa (MOI) kuna upendeleo na hakuna utaratibu wa wazi katika kutoa huduma za matibabu.
Jana, Mwalimu alifanya ziara ya kushtukiza MOI na kuagiza kambi za upasuaji zilizokuwa zikifanyika mwishoni mwa wiki zirudi mara moja ili kupunguza idadi ya wagonjwa wanaosubiri upasuaji.
“Nimewaambia waweke wazi utaratibu wa upasuaji, kama siyo majina basi watumie hata namba ili mgonjwa ajue, lingine wanatakiwa kurudisha utaratibu wa kambi za upasuaji maana wodi zimejaa wagonjwa wanaosubiri huduma hiyo,” amesema Ummy.
Chanzo: Mwananchi