Waziri Ummy: Deni kubwa la matibabu ya nje lililoibuliwa na CAG halihusu Serikali ya Magufuli tu,ni malimbikizo ya nyuma

Wazeee trilion ni pesa nyingi mazeee...
Huu upigaji ni hatari,anavotoka huyu mzee Tanzania itakuwa haina kitu.

Wabunge wamefungwa midomo,mawaziri vile vile.
 
Mbona umeshikia sana bango hili swala, hapa ndipo unapopatia ujira wako nini? Mbowe & Co. wanaiba Mabilioni wengine mmekalia kumpigia makofi, achaneni na Raisi na Serikali yetu, you can go hang!
Serikalini yenu na nani? Raisi wenu na nani? Kwani ikiingia awamu mpya kila kitu kinaanza upya? Mbona analipa madeni ya nyuma kila mwezi? Huyu ni Raisi wa wote hata ambao hawakumchagua.
 
Leo tena waziri wa Afya bi Ummy Mwalimu ameendelea "kujibu" report ya CAG.Waziri Ummy anasema eneo la deni la matibabu ya nje lililotajwa na CAG sio la awamu ya Tano,bali ni mrundikano wa madeni ya miaka ya nyuma,na hivyo serikali ya awamu ya tano isibebeshwe kana kwamba deni hilo limepatikani ndani ya miaka miwili ya uongozi wa awamu ya Tano.

Waziri Ummy anasema ili kukabiliana na deni hilo,serikali ya awamu ya tano kupitia wizara yake imesitisha ulipaji wa deni hilo mpaka wapate uhakiki,kwamba hili deni za zaidi ya mabilioni linahusisha nini hasa?Serikali inataka kujua kama deni hilo ni mjumuisho wa dawa,malazi na "Consultation Fee?".Serikali itakapojiridhisha basi ndio itaanza kulipa deni hilo.

Maana kuna uwezekano mtu akaondoka hapa kama kiongozi wa serikali,anasema anakwenda kutibiwa moyo,lakini kumbe anakwenda kupata huduma ya kupandikiziwa mimba sababu ya matatizo ya uzazi,kitu ambacho katika "packages" ya matibabu yanayofadhiliwa na serikali nje ya nchi,hili la kupandikizwa mimba sio sehemu ya "packages" hizo.

Hii kujibujibu ni kutaka kusema hii serikali haina wezi??Kwanini wanavunja utaratibuuu?Halafu kila mtu akija anasema "Sehemu kubwa ya hii report ya CAG ni ya miaka ya nyuma,hadi July 2017,lakini baada ya hapo,serikali ya awamu ya tano imebadilisha sana mambo".Kwanini wanaitoa serikali ya Awamu ya Tano katika hizi tuhuma za CAG.

Mimi nimepapenda hapo tu!
je wewe?
 
hilo ni deni la serikali ya ssm, hawawezi kukwepa mabaya na kukumbatia ma
zuri aliyoacha JK, by the way kuna mtu alikaa India 3months badaye akakaa 4months..naomba kuishi hapo
Baya zaidi akamnyima mwenzie haki yake ya msingi akiwa kama kiongoz na mtumishi wa kibonge.
 
Hadi kilaza ummy mwl nae anajifanya kupangua hoja za CAG???.......ifike kipindi hawa maprofessor watulie tu pale udsm waachie vilaza waendeshe nchi
Mkuu ni kweli, siasa za nchi hii zinawafaa akina Bajaj. Mlangwa, msukuma na wengineo. Kwa hao wanazuoni ni kujidhalilisha tu.
 
You my Teacher anamtetea Mzee, unakumbuka You my Teacher ulimsemea Mwali kwa mzee kuwa hakuheshimu sasa Mwali amepata kazi kubwa kanda ya Afro.
You my Teacher ulikutana na Mwali kwenye mkutano kule nchi flani na ukamwambia yaliyopita yamepita, kumbe ule umbea wako You my Teache ulikuwa baraka kwa msichana Mwali.

You my Teacher mzee hatakuwa na hii nafasi milele.
Imenipa shida kung'amua hii tafsida, hatimaye nimeweza! Hii inji hii ina mambo!
 
barafu Kuna mambo mengine yanayoendelea ndani ya serikali hii ukiyajua utatamani kutukana hadharani. Huyu mama anaongea utafikiri yupo kwenye ukumbi wa Taarabu.

Suala la madeni utetezi wa kusema sio wa serikali hii ni upumbavu mkubwa na huu sio utetezi, tatizo serikali hii hailipi madeni si ya ndani wala nje sabb ipo taabani kifedha.

Jambo lingine toka lini serikali inajibu hoja za ukaguzi bungeni kupitia mawaziri? Utaratibu wa miaka yote Afisa Masuuli (katibu mkuu) ndiye mjibu hoja kupitia vikao vya PAC hili la mawaziri kujibu ni kutaka kuficha uovu wa serikali hii ili Wabunge wawe mabubu
 
Wewe barafu punguza kurefusha mdomo mnataka muongee pekee yenu...mueneze uongo na hamtaki watu wajibu hoja.....mnataka nyie muongee peke yenu wengine wasiseme......Lazima watoe maelezo kwa sababu kuna hatua zimesha chukuliwa sio lazima kuwasubiri makatibu wakuu...
Kwakuwa mliligeuza hili jambo ni la kisiasa hasa ninyi na hamtaki wenzenu waongee mtulie sasa watu wajibu hoja kama sio za kweli mseme sio kujificha kwenye kichaka cha makatibu wakuu

1. Nendeni mkaukate mdomo wa barafu Kimbelembele sana huyu.
2. Hivi huko nyuma ilikuwa serekali ya chama gani ?
 
So what?Hapa hapahitaji blablaa,bali ni kulipa tu.Mbaya zaidi ni kwamba usimamizi ni mbovu,haiingii akilini eti oooo mtu anaweza kusema anaenda nje ya nchi kutibiwa moyo kumbe anaenda kupandikiza mimba.Inamana mtu anaamua tu kwenda nje bila kufata taratibu?Siku za nyuma mlitueleza kuwa mtu hawezi kwenda nje ya nchi bila kibali toka muhimbili.
 
Back
Top Bottom