Waziri Stephen Wassira Yuko Likizo Igunga?

Apr 11, 2011
14
5
Ndugu zangu wanajf nimekuwa nikifuatilia uwepo wa Waziri Stephen Wassira kule Igunga kataka kusaidia kampeni za Chama Cha Magamba yaani CCM ili kiweze kuchukua kiti kilichaoachwa na mmoja wa mapacha watatu ndani ya CCM. Taarifa nilizonazo ametumwa na Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Mara na atakuwepo kwa kipindi chote cha kampeni. Je napenda kufahamu Stephen Wassira kama Waziri ambaye ni mahiri kulala bungeni atakuwa likizo ya kikazi?

Je aliyemteua kwenye nafazi ya uwaziri amemruhusu tena kwa malipo kuwepo Igunga kwa muda wote wa kampeni? Je hii likizo ya aina hii ipo kwa mujibu wa sheria?ambaye anaufahamu wa misingi ya sheria na taratibu za viongozi wa serikali hii ya magamba kama ilivyo kwa Wasira imekkaje?
 
Waziri ni mtendaji wa serikali, sasa anapokuwa kwenye kampeni za chama...
 
Ndugu zangu wanajf nimekuwa nikifuatilia uwepo wa Waziri Stephen Wassira kule Igunga kataka kusaidia kampeni za Chama Cha Magamba yaani CCM ili kiweze kuchukua kiti kilichaoachwa na mmoja wa mapacha watatu ndani ya CCM. Taarifa nilizonazo ametumwa na Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Mara na atakuwepo kwa kipindi chote cha kampeni. Je napenda kufahamu Stephen Wassira kama Waziri ambaye ni mahiri kulala bungeni nasikia hata chooni au bafuni akiwa anaoga atakuwa likizo ya kikazi?nasikia aliyemteua kwenye nafazi ya uwaziri amemruhusu tena kwa malipo kuwepo Igunga kwa muda wote wa kampeni.Je hii likizo ya aina hii ipo kwa mujibu wa sheria?ambaye anaufahamu wa misingi ya sheria na taratibu za viongozi wa serikali hii ya magamba kama ilivyo kwa Wasira imekkaje?

Mkuu sorry for saying this...Nchi hii haiongozwi kwa taratibu na sheria,inaongozwa na mawazo ya watu wachache wajanja..na imewai kusemwa ni familia za watu saba tu ndio wanaongoza hii nchi......
 
kwani tunayo serikali? Iko wapi? Inafanya nini?
Mungu atusaidie tupate serikali, then mambo mengine yataendelea vizuri
 
Nchi hii haiongozwi kwa sheria, unaongozwa kwa ma tukio.
 
Kumbe Wasira naye katia timu????? Sasa amebakia nani maana hata mzee wetu Mangula ilibidi wampigie magoti lakini ndio hivo CCM maji ya shingo tu Igunga.
 
nchi hii haiongozwi kwa sheria, unaongozwa kwa ma tukio.

umenena vema mzee, ni sawa na wakristo wa leo, ukitaka kuwaibia, wewe usitumie biblia au tumia biblia kwa kuchukua mistari ambayo ni irelevant to the contex halafu tumia miujiza/mazingaombwe, utawakamta wengi sana.

Ndivyo serikali ya ccm ilivyo. Mtu ni waziri anaacha kazi za taifa anaenda kupiga siasa. Hii si haki ingawa sishangai. Kwani uwaziri wa wasira ni sawa na hakuna waziri
 
Mimi niko huku Gombe National Park........naangalia wanyama katika kudumisha utalii wa ndani....siataki siasa kwa sasa

12.jpg
 
Kuna post humu ndani zimechakachuliwa baada ya kuona kwamba zinavuka mipaka ya kistaarabu. Lakini Mods wangeziacha ili wengine waone upumbavu wa wenzao wanaodhani afya njema, na ukamilifu wa miili na akili zao ni uwezo wao. Shame on you!
 
Mimi niko huku Gombe National Park........naangalia wanyama katika kudumisha utalii wa ndani....siataki siasa kwa sasa

12.jpg

Watu wengine huwa mnapenda kuwavunja wenzenu mbavu, sasa huyu aliyeko Gombe ni nani teeeh....teeh...... Heri mimi sijamtaja.What about huyo anayekonyeza hapo juu kushoto....aaahahaa...aaaahaha.
 
Mimi niko huku Gombe National Park........naangalia wanyama katika kudumisha utalii wa ndani....siataki siasa kwa sasa<br />
<br />
<img src="http://muller.lbl.gov/travel_photos/africawildlifefolder/AfricaWildlifeFolder-Images/12.jpg" border="0" alt="" />
<br />
<br />
Hapo mkubwa imekaa vyema katika kutupa picha za vivutio tunavyojivunia Tz. Endelea kuwakilisha huko mbugani ili mimi naenda Igunga kushuhudia siasa.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom