Mkuu Mtu Wa Kawaida, nimekumbuka kale kamwimbo ka marehemu Mbaraka Mwinshehe na Moro Jazz...
hilo woo woo
ulijidai wewe mbabe sana
leo umepigwa na kijana mdogo
aibu imekupata
kiko wapi
ulichokuwa ukijidi nacho
je ungepambana na mimi sasa
kilema ungekipata
Ooho kebehi na majivuno yako, yako wapi sasa
aibu imekupata.....
Wadau mpambano huu ataimbiwa mtu, maana siku hizi hakuna sera ni bifu!
- Unajua ndio maana nilisema mapema sana kwamba wote wagombea wawili walitakiwa kuondolewa, yaliyojiri kwenye huu uchaguzi ni aibu kubwa sana kwa taifa letu, mapesa ni mengi mno yaliyotumika kwa sababu ya uwt tu? Na haya mapesa yametolewa na wagombea wote wawili sio siri! Tena Mama Janet ndiye ametumia hela nyingi mno shame kwa wote wawili, lakini zaidi kwa Mama Janet shame on you!
- Yaani uenyekiti wa Umoja wa wanawake ambao zamani hata hatukujua kama huwa unagombewa maana mimi nilidhani Mama Sophia Kawawa ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa kudumu, sasa all over sudden imekua patashika mpaka wakuu wa taifa kuhusika, kulikoni? Haya mapesa kina Sophia na Mama Janet ya kutupa namna hii wanayatoa wapi? Ninasema hivi hizi hela za kumwaga namna hii kama karanga wanatoa wapi?
I can confirm kuwa SOFIA SIMBA kashinda pamoja na Janet Kahama kutumia zaidi ya dola milioni 2 lakini looks like fitna ya Sofia ilikuwa si mchezo...
Anyway kuja jambo lilitokea mle ndani na ni kosa la wasimamizi wa Janet ambalo atakuja kulijutia sana
ES hebu nicheki
Mkuu FMES umenikuna sana kwa hili infwakti hata mimi nilijua hivyo, nimeshangazwa sana eti kuna kampeni ya mtu kuwa mwenyekiti UWT........... Bado nacheka nikisoma post yako. Ni mambo ya aibu............ waziri anayesimamia uwt nyingine anatoa rushwa kama karanga. Hv huo uenyekiti UWT ni zadi ya uwaziri???????
Once you are the chairperson of UWT, you are automatically Mbunge. 2010 huna expense`yeyote ya kutafuta kura. Uko assured kuwa "employed " mpaka 2015.
Wadau,
Hivi Sophia Simba atapata wapi muda wa kufanya kazi zote kama Mbunge, waziri na mwenyekiti wa UWT?
Wakati mamilioni ya watu hawana kazi, hawa wengine wanahodhi vyeo na kushindwa ku deliver.