Waziri Sophia Simba - Mwenyekiti Mpya UW-CCM (Taifa)

Msiwasahau wanaosimama na kuunga mkono hoja za wenzao, wao kila wasimamapo anaunga mkono au kukubaliana na fulani. je hao wana points, au wanadandi points?
 
Waziri Sophia Simba aanza kuchunguzwa

2008-12-27 15:06:04
Na Joseph Mwendapole na Muhibu Said

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesema tuhuma za rushwa zinazomkabili Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, zitafanyiwa uchunguzi na ikithibitika hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake.

Wakati CCM ikitoa kauli hiyo, Simba amegoma kutoa ufafanuzi kuhusu tuhuma zinazomkabili zilizolalamikiwa na mgombea mwenzake wa nafasi ya Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa chama hicho, Janeth Kahama, alipotakiwa na Nipashe kufanya hivyo jana.

Kahama, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Desemba 20, mwaka huu, aliwasilisha rasmi malalamiko kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akimtuhumu Waziri Simba kuwa ametoa hongo ya sh.100,000 kila mjumbe wa Mkutano Mkuu ili wampe kura.

Akizungumza na Nipashe jana, Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa, Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati, alisema kwa kuwa chama hicho kinapinga vikali vitendo vya rushwa na kila mwanachama anapotuhumiwa lazima achunguzwe.

Chiligati alisema anaamini kuwa kama malalamiko hayo yamemfikia Mwenyekiti wa chama, Rais Jakaya Kikwete atatumia vyombo vya dola ama kamati za maadili ndani ya CCM kuchunguza.

``CCM haifumbii macho suala la rushwa hata kidogo, kila mwanachama akipata tuhuma tunachunguza na kuchukua hatua, sasa hili la Sofia Simba kama kweli limefika kwa Mwenyekiti wetu naamini yuko makini sana na anaweza kuamua kuagiza vyombo vya dola au kamati za maadili za chama kuchunguza,`` alisema Chiligati.

Uchaguzi wa UWT, unatarajiwa kufanyika Januari 7 ,2009 na wagombea watakuwa Janeth Kahama, Sofia Simba na Joyce Masunga.

Katika barua yake kwa Mwenyekiti wa chama hicho ambaye ni Rais Jakaya Kikwete, Kahama analalamika kuwa Sofia Simba na wapambe wake wamekuwa wakiitumia Ikulu kuwaomba kura wajumbe wa Mkutano Mkuu.

Kahama ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum, amewasilisha malalamiko yake kupitia barua yenye kumbukumbu namba JBK/01/08 ya Desemba 20 mwaka huu, iliyopelekwa kwa Rais Kikwete.

Nakala ya barua hiyo ambayo Nipashe inayo, imepelekwa kwa Katibu Mkuu wa UWT na Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba.

Makamba alipoulizwa na gazeti hili kama amethibitisha kupokea barua hiyo alikiri kuipokea.

Simba anadaiwa kutoa hongo hiyo kupitia kadi alizochapisha na kusambazwa na Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo. Kadi hizo zina picha, jina na sahihi ya Waziri Simba, Kalenda ya 2009 na nembo ya CCM.

Waziri Simba alipotakiwa jana kutoa ufafanuzi kuhusu tuhuma hizo, hakukiri wala kukanusha badala yake alisema kwa ufupi: ``Sina neno.``

Alipoulizwa ni kwa nini anasema hana neno, Waziri Simba alisema kwa jazba: ``Sina neno hasa kwa (gazeti la) Nipashe, kwa sababu siku zote mmekuwa mkiniandika bila kufanya utafiti. Hivyo, sitaki kusema na mtu yoyote wa Nipashe full stop na usinipigie tena (simu)``.

SOURCE: Nipashe
 
Waziri Sophia Simba aanza kuchunguzwa

2008-12-27 15:06:04
Na Joseph Mwendapole na Muhibu Said

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesema tuhuma za rushwa zinazomkabili Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, zitafanyiwa uchunguzi na ikithibitika hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake.

Wakati CCM ikitoa kauli hiyo, Simba amegoma kutoa ufafanuzi kuhusu tuhuma zinazomkabili zilizolalamikiwa na mgombea mwenzake wa nafasi ya Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa chama hicho, Janeth Kahama, alipotakiwa na Nipashe kufanya hivyo jana.

Kahama, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Desemba 20, mwaka huu, aliwasilisha rasmi malalamiko kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akimtuhumu Waziri Simba kuwa ametoa hongo ya sh.100,000 kila mjumbe wa Mkutano Mkuu ili wampe kura.

Akizungumza na Nipashe jana, Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa, Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati, alisema kwa kuwa chama hicho kinapinga vikali vitendo vya rushwa na kila mwanachama anapotuhumiwa lazima achunguzwe.

Chiligati alisema anaamini kuwa kama malalamiko hayo yamemfikia Mwenyekiti wa chama, Rais Jakaya Kikwete atatumia vyombo vya dola ama kamati za maadili ndani ya CCM kuchunguza.

``CCM haifumbii macho suala la rushwa hata kidogo, kila mwanachama akipata tuhuma tunachunguza na kuchukua hatua, sasa hili la Sofia Simba kama kweli limefika kwa Mwenyekiti wetu naamini yuko makini sana na anaweza kuamua kuagiza vyombo vya dola au kamati za maadili za chama kuchunguza,`` alisema Chiligati.

Uchaguzi wa UWT, unatarajiwa kufanyika Januari 7 ,2009 na wagombea watakuwa Janeth Kahama, Sofia Simba na Joyce Masunga.

Katika barua yake kwa Mwenyekiti wa chama hicho ambaye ni Rais Jakaya Kikwete, Kahama analalamika kuwa Sofia Simba na wapambe wake wamekuwa wakiitumia Ikulu kuwaomba kura wajumbe wa Mkutano Mkuu.

Kahama ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum, amewasilisha malalamiko yake kupitia barua yenye kumbukumbu namba JBK/01/08 ya Desemba 20 mwaka huu, iliyopelekwa kwa Rais Kikwete.

Nakala ya barua hiyo ambayo Nipashe inayo, imepelekwa kwa Katibu Mkuu wa UWT na Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba.

Makamba alipoulizwa na gazeti hili kama amethibitisha kupokea barua hiyo alikiri kuipokea.

Simba anadaiwa kutoa hongo hiyo kupitia kadi alizochapisha na kusambazwa na Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo. Kadi hizo zina picha, jina na sahihi ya Waziri Simba, Kalenda ya 2009 na nembo ya CCM.

Waziri Simba alipotakiwa jana kutoa ufafanuzi kuhusu tuhuma hizo, hakukiri wala kukanusha badala yake alisema kwa ufupi: ``Sina neno.``

Alipoulizwa ni kwa nini anasema hana neno, Waziri Simba alisema kwa jazba: ``Sina neno hasa kwa (gazeti la) Nipashe, kwa sababu siku zote mmekuwa mkiniandika bila kufanya utafiti. Hivyo, sitaki kusema na mtu yoyote wa Nipashe full stop na usinipigie tena (simu)``.

SOURCE: Nipashe

Sasa mkuu nadhani sio rahisi kwa mtuhumiwa kusema lolote kuhusu tuhuma zinazomuhusu. Sie tusubiri hiyo hao CCM watatoa uamuzi gani kuhus ili sakata la uongozi
 
Mama Simba anaonekana anajiamini sana, kuna mahali pazito anaegemea. Kwa vile tuhuma za rushwa ni tuhuma nzito, hata CCM wakizithibitisha, sio kutamchafulia Mama Simba pekee bali chama chao na serikali ya JK. Kuliko kuchafua wataona bora wamkane Mama Kahama aonekane muongo, kwani atafanya nini zaidi ya kuishia kulia. Yaliyomkuta Nape aliyaona. Bado Mama Kahama anaamini kwenye ukweli ambao kwa CCM ni dhambi. Sophia Simba atapeta uenyekiti UWT na kansa ya rushwa itakuwa ndio inaenea mwiili mzima wa CCM tayari kwa 2010.
 
Waziri Sophia Simba aanza kuchunguzwa

.................................. ``Sina neno.``

Alipoulizwa ni kwa nini anasema hana neno, Waziri Simba alisema kwa jazba: ``Sina neno hasa kwa (gazeti la) Nipashe, kwa sababu siku zote mmekuwa mkiniandika bila kufanya utafiti. Hivyo, sitaki kusema na mtu yoyote wa Nipashe full stop na usinipigie tena (simu)``. [/U][/I]
SOURCE: Nipashe



Atasema tu. Ameshakalia msumari huyu. Tusubiri. Kwani Nipashe ndiyo walioandika barua ya malalamiko kwa Kikwete!
 
Mama Simba anaonekana anajiamini sana, kuna mahali pazito anaegemea. Kwa vile tuhuma za rushwa ni tuhuma nzito, hata CCM wakizithibitisha, sio kutamchafulia Mama Simba pekee bali chama chao na serikali ya JK. Kuliko kuchafua wataona bora wamkane Mama Kahama aonekane muongo, kwani atafanya nini zaidi ya kuishia kulia. Yaliyomkuta Nape aliyaona. Bado Mama Kahama anaamini kwenye ukweli ambao kwa CCM ni dhambi. Sophia Simba atapeta uenyekiti UWT na kansa ya rushwa itakuwa ndio inaenea mwiili mzima wa CCM tayari kwa 2010.

Mkuu CCM hasa Kikwete huwa hatabiriki.Utakuja shangaa huyo mama simba atakapopigwa chini na mama kahama kupeta kama madai yake ni ya kweli.
 
Sasa wametoboa siri za vibahasha!:eek:

Itakuwa vigumu kwangu 2009 kuwapa marafiki na hata wakuu wangu, kadi za masimasi na nyu yia:mad:

Hii ni vizuri ndani ya CCM na kwenye siasa za uchaguzi. Watajirekebisha
 
- Pamoja na kuwawakilisha wananchi bungeni, kazi ya msingi ya wabunge bungeni ni kuongea kwanza, and then matendo the question ni mbunge anaongea nini? Kwa mfano tumewasikia mbunge Dr. Slaa akiongea na mbunge Serukamba akiongea pia, sasa unahitaji kuwa professor kweli kujua nani kati ya wabunge hawa anaongea nonesense na nani anaongea kama wajibu wa wa uwakilishi bungeni unavyotakiwa? Wabunge ni lazima waongee wananchi ndio tutaamua nani anahitaji kunyamaza iwapo ni pumba tupu kama za Serukamba.

- Hawa kina Sophia Simba ndio wanaomuharibia jina rais, kujifanya wanamjua sana na atawalinda kumbe ni wapuuzi wa akili na wanatuharibia mpaka jina la chama, ni kweli ametoa hizo hela maana kuna mjumbe mmoja amenitumia hako ka-karatasi kake tayari nimempa mjumbe mmoja wa cc, sasa huyu sheria ichukue tu mkondo wake maana yeye ndiye waziri wa Usalama, sasa kama anahusika na kutoa rushwa taifa tutamuamini nani hasa? Huyu naye ni kupeleka Kisutu tu, halafu wote wawili wapigwe chini maana kile kitendo cha kutiana masingi ya vidole mbele ya wananchi ni aibu kubwa sana kwa wote wawili fukuza wote wasipewe hiyo nafasi.

- The bottom line, rais aondoe huu ubunge wa bure now!
 
Mkuu FMES,

Umenena. Mie kwa kweli sometimes simuelewi Muungwana. Mheshmiwa na all necessary tools at his disposal lakini bado ni butu tu. Hivi anashindwa kuwauliza UWT kuhusu hili la rushwa na kumtupilia huyu mama mbali kabisa na serikali yake?

Saa nyingine mie sielewi wabongo tupo vipi!
 
Wanawake wamfitinisha Waziri Simba na Kikwete

jk_63.jpg

Mwandishi Wetu Januari 7, 2009
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

Vita yake na Janeth Kahama yazidi kupamba moto​

WAKATI Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) ukitarajia kupata mwenyekiti wake mpya wiki hii, kumekuwapo na hujuma dhidi ya demokrasia itakayofanikisha mchakato wa kumpata mwenyekiti huyo, Raia Mwema imebaini.

Miongoni mwa mambo yaliyoibuka ni kutajwa kwa Rais Jakaya Kikwete kumuunga mkono mmoja wa wagombea wa naasi hiyo, Waziri wake wa Utawala Bora, Sophia Simba, madai ambayo yameshindwa kuthibitishwa na uongozi wa juu wa CCM uliopelekewa.

Pamoja na kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Sophia Simba ni Mbunge wa Kuteuliwa na Rais, nafasi ambayo inatafsiriwa kuwa imetokana na kuwa kwake karibu na Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Kikwete.

sophia_1.jpg

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Sophia Simba​

Mbali ya kutajwa kwa Rais Kikwete ambaye ndiye atakayefungua rasmi mkutano wa UWT leo Jumatano, tuhuma za rushwa na kuchafuana kwa wagombea ni mambo yaliyotawala kampeni za kuelekea uchaguzi wa jumuiya hiyo yenye nguvu ndani ya chama tawala.

Baadhi ya wapambe wamefikia hatua ya kusambaza ujumbe wa maneno kupitia simu za mkononi za baadhi ya wajumbe wakitumia ugonjwa wa mmoja wa wagombea kama sababu ya kutaka asichaguliwe kushika nafasi hiyo ya uongozi wa UWT. Nafasi hiyo inawaniwa pia na wabunge wa Viti Maalumu Janet Bina Kahama na Joyce Masunga.

Wagombea kupitia wapambe wao inadaiwa wanahujumu mkondo wa demokrasia ya mmojawao kuchaguliwa kumrithi mwenyekiti anayemaliza muda wake, Anna Abdallah.

Inadaiwa kuwa baadhi ya washiriki wa kampeni za wagombea hao walilazimika kusafiri na baadhi ya wajumbe kuelekea Dodoma katika kile kilichoelezwa kuwa kuwathibiti wasibadili mawazo ya kumchagua mgombea wa kundi wanalounga mkono.

Wajumbe waliojikuta wakisafiri na wapambe wa wagombea hao ni pamoja na wanaotoka katika baadhi ya mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Wajumbe wengine kutoka mikoa ya Kusini walijikuta wakizuiwa kwa muda jijini Dar es Salaam katika kile kinachoweza kuelezwa kuwa ni "kuwekwa sawa."

Baadhi ya wajumbe wamejikuta wakigharimiwa huduma za malazi jijini Dar es Salaam, kabla ya kuelekea mjini Dodoma kupiga kura.

Uchunguzi zaidi umebaini kuwa wajumbe hao wamekuwa hodari katika kutoa ushirikiano ili kupewa rushwa na wapambe wa wagombea hao.

Habari kutoka mjini Dodoma zinaeleza kuwa wapambe wa baadhi ya wagombea waliwasili mjini hapo siku kadhaa, baadhi ya wagombea waliwasili mjini hapo siku kadhaa kwa ajili ya kuwapokea wajumbe wapiga kura.

Lakini wakati wapambe hao wakiwa wamewasili Dodoma kabla ya wajumbe kuwasili, washindani wao walilazimika kusafiri hadi katika mikoa wanakotoka wajumbe hao na kusafiri nao kuelekea Dodoma.

Kilele cha uchaguzi huo kinafikiwa wakati wagombea Sophia Simba na Mbunge wa Viti Maalumu, Janet Kahama wakiwa katika mvutano na mchuano mkali.

Kumekuwapo na malalamiko kutoka katika kila upande kuhusiana na kuchezeana ‘rafu' na zaidi ni kambi mbili za Janet Kahama na ile ya Waziri Simba.

kahama_1.jpg

Mbunge wa Viti Maalumu, Janet Kahama​

Janet Kahama kama ilivyo kwa Joyce Masunga ni wabunge wa Viti-Maalumu na ukweli ni kwamba mchakato wa kupata wabunge wa aina hiyo huhusisha ushindani ikiwa ni pamoja na kupigiwa kura na wajumbe maalumu katika mikoa wanakogombea.

Hata hivyo, madai kwamba Waziri Simba ametumwa na mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete kugombea nafasi hiyo yamekwishakanushwa.

Madai hayo si mara ya kwanza kutajwa, yamewahi kujitokeza katika kinyang'anyiro cha viongozi wa juu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) pia.

Mara kadhaa, Rais Kikwete mwenyewe amesikika akikanusha madai hayo. Lakini wakati Waziri Simba akiwa katika mazingira hayo, mgombea Janet Kahama naye anadaiwa kuungwa mkono na mwenyekiti anayemaliza muda wake, Anna Abdallah.

Haijafahamika ni kwa nini Anna Abdallah amuunge mkono mgombea huyo, lakini inawezekana ni imani yake kuwa mama huyo aliyepishana naye miaka mitatu kiumri (Anna akiwa mkubwa zaidi) ataweza kuongoza umoja huo kwa tija zaidi.

Lakini licha ya kuwapo kwa madai hayo, Anna Abdallah hakuwahi kusikika hadharani akiyapinga, lakini pia hakuna ushahidi wowote unaothibitisha kuwa anamuunga mkono Janet Kahama.

Wakati wagombea hao wakiwa na mazingira hayo, mgombea mwingine Joyce Masunga naye anatajwa kuwa na kigogo anayemuunga mkono.

Baadhi ya wajumbe wa UWT wanadai kuwa anaungwa mkono na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba.

Tofauti na wenzake hao wawili, Masunga amekuwa akiendesha kampeni za kimya kimya, na kwa wanasiasa wengine waliozoea mikikimiki ya kampeni wanadai kuwa mwenendo wa kampeni za mgombea huyo zinaweza kumwangusha.

Anna Abdallah anaondoka madarakani baada ya kuongoza UWT kwa miaka 14. Aliingia madarakani mwaka 1994, akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Sophia Kawawa, aliyefariki dunia.

Kwa mujibu wa wachambuzi wa masuala ya kisiasa, endapo mmojawapo kati ya Sophia au Kahama atashinda kiti hicho, uongozi wake huenda ukakabiliwa na changamoto nyingine ndani ya umoja huo.

Kuna uwezekano mkubwa changamoto hizo zikawa zinaibuliwa na kundi la mshindani atakayeshindwa ili hatimaye kuthibitisha kuwa ilikuwa ni makosa kwa mhusika kuchaguliwa kutokana na uwezo duni kiutendaji.

Hali hiyo inatabiriwa kwa kuwa wito wa kuvunja makundi ndani ya CCM umekuwa ukipuuzwa licha ya wito huo kutolewa na viongozi wa juu, akiwamo Mwenyekiti wa Taifa, Rais Kikwete.

Nafasi ya Uenyekiti wa UWT kama ilivyo kwa jumuiya nyingine za chama hicho, ina umuhimu wa pekee kutokana na anayeshika nafasi hiyo kuingia moja kwa moja katika vikao vya Halmashauri Kuu na Kamati Kuu.

Kuwa mjumbe wa Kamati Kuu CCM mwaka mmoja kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 kuna umuhimu mkubwa kisiasa, si tu kwa mjumbe husika bali pia kwa wanasiasa wengine wakiwamo wagombea wa nafasi za kisiasa katika dola ikiwamo Urais na Ubunge.

Ni kwa ajili hii wanasiasa wengi makini wametupa karata zao katika uchaguzi wa UWT kama walivyofanya katika uchaguzi wa Umoja wa Vijana (UVCCM) uliokuwa na makeke mengi na ule wa Jumuiya ya Wazazi, ambao umeshindwa kufanyika kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo makundi ndani ya chama hicho tawala.

Uchaguzi huo umetanguliwa na mkutano wa Baraza Kuu la UWT lililoketi Jumanne, wiki hii.

Miongoni mwa mambo yaliyopitiwa katika mkutano huo wa Baraza Kuu ni pamoja na kupitia ripoti ya utendaji ya umoja huo katika kipindi kilichopita.
 
Najua leo Dodoma Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wanachagua Mwenyekiti wao. Napenda wale wenye kunusa huko watupe updates iwapo Sophia Simba amtamshinda Hasimu wake mama Kahama...
 
Last edited by a moderator:
Wakuu hakuna mwenye taarifa yoyote ya huu uchaguzi au matokeo yatatolewa kesho? Wale Kina Simba na Kahama wote wamegombea au wametolewa kwenye kugombea?
 
Chanzo changu cha uhakika kinasema Waziri Simba kapigwa chini huku JK mwenyewe akitia mkono wake.
Mwenyekiti mpya wa UWT ni mama Kahama.
 
Wakuu hakuna mwenye taarifa yoyote ya huu uchaguzi au matokeo yatatolewa kesho? Wale Kina Simba na Kahama wote wamegombea au wametolewa kwenye kugombea?

Mkuu Mtu Wa Kawaida, nimekumbuka kale kamwimbo ka marehemu Mbaraka Mwinshehe na Moro Jazz...

hilo woo woo
ulijidai wewe mbabe sana
leo umepigwa na kijana mdogo
aibu imekupata

kiko wapi
ulichokuwa ukijidi nacho
je ungepambana na mimi sasa
kilema ungekipata

Ooho kebehi na majivuno yako, yako wapi sasa
aibu imekupata.....

Wadau mpambano huu ataimbiwa mtu, maana siku hizi hakuna sera ni bifu!
 
Back
Top Bottom