Prof Koboko
JF-Expert Member
- Aug 15, 2020
- 350
- 2,549
Kinachonishangaza ni kuona ndugu yangu huyu ambaye naamini ni msomi wa sheria leo anaamua kugeuka makusudi mbele ya umma wa watanzania bila hata kuogopa na kuzingatia maadili ya kazi yake.
Nataka niulize swali, hivi si ndio huyu huyu Simbachawene alikuwepo wakati wa kutunga katiba mpya awamu ya 4 chini ya Jaji Warioba? Alishindwa nini wakati ule kusema kuwa Wananchi hawahitaji katiba mpya? Kwenye bunge la katiba alipiga kura ya nini kupata katiba iliyopendekezwa kama mjumbe?
Hivi ninyi viongozi ni lini mtaacha kuwa vigeugeu? Hamumuogopi hata Mungu wenu?
Bora Mhe Rais alitoa msimamo wake kuwa anaimarisha uchumi kwanza lakini hakukataa katiba mpya. Hawa wasaidizi wake wakati mwingine ni wanaisumbua tu jamii na wanamwangusha kwa kujipendekeza kwake.
Waziri mzima msomi wa sheria unasimama unasema kuwa wananchi hawahitaji katiba mpya? Huu ni sawa na usaliti wa taifa, viongozi wetu wajifunze.
Nataka niulize swali, hivi si ndio huyu huyu Simbachawene alikuwepo wakati wa kutunga katiba mpya awamu ya 4 chini ya Jaji Warioba? Alishindwa nini wakati ule kusema kuwa Wananchi hawahitaji katiba mpya? Kwenye bunge la katiba alipiga kura ya nini kupata katiba iliyopendekezwa kama mjumbe?
Hivi ninyi viongozi ni lini mtaacha kuwa vigeugeu? Hamumuogopi hata Mungu wenu?
Bora Mhe Rais alitoa msimamo wake kuwa anaimarisha uchumi kwanza lakini hakukataa katiba mpya. Hawa wasaidizi wake wakati mwingine ni wanaisumbua tu jamii na wanamwangusha kwa kujipendekeza kwake.
Waziri mzima msomi wa sheria unasimama unasema kuwa wananchi hawahitaji katiba mpya? Huu ni sawa na usaliti wa taifa, viongozi wetu wajifunze.