Waziri Simbachawene tunataka vitambulisho vya taifa, udhibiti wa maoni ya watu mtandaoni utakuja mwisho

Tindo

JF-Expert Member
Sep 28, 2011
58,998
103,379
Ndugu yetu Simbachawene, inaonekana majukumu yako yamekushinda, sasa hivi umerukia utoaji wa maoni ya wananchi mitandaoni.

Ungetuonyesha kwanza ukamilikaji wa vitambulisho vya taifa kwa wananchi wote wenye kustahili, kisha ndio utake kuwafurahisha hao waliokuwa cheo kwa kudhibiti maoni ya wananchi.

Ifahamike mko madarakani kisheria, lakini bila ridhaa ya umma, kwani mko madarakani kwa uchaguzi uliokuwa wa kihayawani kuliko kawaida. Hali hii inawafanya kudhibiti uhuru wowote wa maoni ambao utaanika uhuni wenu uliowaingiza madarakani.

Unaweza kudhibiti magazeti, TV, redio nk, lakini kwenye mitandao huwezi maana ni technology iliyo nje ya uwezo wenu, na hila zenu za kutawala kwa shuruti.

Hivyo acha kusaka sifa za kijinga wakati umeshindwa kutupatia vitambulisho vya taifa wote tunaostahili.

Kwa taarifa yako ww unalipwa hela ya bure wakati huna tija yoyote, sasa ili kuhalalisha malipo makubwa bila tija, ndio unajifanya unataka kudhibiti uhuru wa kujieleza.
 
Ni bora waanze kudhibiti wajinga mitandaoni kuliko hivyo vitambulisho.
Wajinga, wahalifu na magaidi wanazidi kuongezeka wakiwa wanajificha kwenye kivuli Cha demokrasia
 
Ni bora waanze kudhibiti wajinga mitandaoni kuliko hivyo vitambulisho.
Wajinga, wahalifu na magaidi wanazidi kuongezeka wakiwa wanajificha kwenye kivuli Cha demokrasia

Uwezo pekee walio nao ni kuzima internet, ila hawana uwezo wowote wa kuzuia maoni asiyoyapenda. Technology kwa sasa iko nje ya uwezo wao. Wanaweza kudhibiti maeneo yanayotumia nguvu zaidi kuliko akili, ila haya yanayohitaji matumizi ya akili hawana uwezo huo.
 
Ni bora waanze kudhibiti wajinga mitandaoni kuliko hivyo vitambulisho.
Wajinga, wahalifu na magaidi wanazidi kuongezeka wakiwa wanajificha kwenye kivuli Cha demokrasia
Mjinga ni wewe na mawazo yako ya kipuuzi, sijui wa wapi wewe lakini utakuwa wakuja tuu
 
Back
Top Bottom