Waziri Simbachawene:Maini mnazokula Nyie wananchi ndio hayo tu nakula sisi Mawaziri, Maisha ya sasa ni bora zaidi kuliko wakati wote uliopita

seedfarm

JF-Expert Member
Feb 9, 2020
260
2,654
Mheshimiwa Waziri Simbachawene ameyasema hayo Leo wakati akijibu maswali yanayohusiana na malalamiko ya tozo akiwa sambamba na Waziri wa Fedha Mheshimiwa Mwigulu Nchemba

Simbachawene amesema watu lazima watambue maisha yana badilika kila wakati na kwa sasa binadamu anamahitaji mengi sana kama simu na TV ambazo hazikuwepo wakati huo hivyo Leo watu wengi wanaishi maisha mazuri zaidi ukilinganisha na zile zama ambazo TV tulijazana kwa majirani kundi la watu kutazama

Simbachawene amesisitiza kwa sasa watanzania wana mahitaji mengi hivyo wananunua data au bundle, wanalipia ving'amuzi vya TV, Kuna luxiary nyingi sana kwa sasa ndio maana watu wanaona maisha màgumu lakini Kiuhalisia wakati huo zamani ndio maisha yalikuwa magumu zaidi hakukuwa na huduma bora kama za sasa

Simbachawene amesisitiza kuwa watu wasifikiri wao viongozi wanaishi tofauti au maisha mengine kwani Maini ya nyama ya ng'ombe anayenunua Yeye au Mawaziri ni yale yale ya buchani kama watu wengine wanayokula

Waziri Simbachawene amesisitiza lazima kwa dhama hizi kelele zikijitokeza mtandaoni mfano tozo zijibiwe kwa wakati kwani watu wakiacha kupotosha mambo ya uchumi wananchi watafikiri jambo hilo ni kweli, Amesisitiza mambo ya uchumi na Sera mtu sahihi wa kuliongelea ni Waziri wa Fedha na sio mtu mwingine

Simbachawene amesisitiza kuwa wakati huo watu walikuwa na maisha màgumu sana mfano Yeye alienda shule Mazengo Sekondari akiwa ana suruali moja tu lakini Leo vijiji vingi vya Tanzania watu angalau wanaweza hata kuvaa chacha au sandles za wazi shule

Waziri amehitimisha kuwa tozo zinazokusanywa ni kwa maslahi mapana ya Taifa na hivyo watu wanapoongelea maisha Leo magumu hawafanyi ulinganifu makini kwani kwa sasa maisha sio magumu bali mahitaji yameongezeka mfano watu wanataka kula milo mitatu na kupanda boda boda kwa kilomita moja, Miaka hiyo watu walitembea kwa miguu hivyo maisha yalikuwa magumu sana

Akichangia hoja hiyo kwa basha basha Waziri wa Fedha bwana Mwigulu Nchemba amesema hata Yeye anashangaa Leo hii watu wanakula robo kuku, au Nusu kuku lakini miaka ile mfano Yeye walikuwa watu 11 kwenye Familia moja hivyo kuku akipikwa wakigawa hata neno paja utalisikia tu kwani paja linaweza kugawanywa hata mara tano ili watu wale chakula

Mheshimiwa Mwigulu Nchemba amesisitiza kuwa hata Yeye ni maskini na anafahamu maisha kwani ndio amekuwa nayo kijijini hata Yeye hapendi kutoza watu kodi na pia hata Mheshimiwa Rais hapendi hilo lakini wananchi wana mahitaji muhimu wanayotaka yatekelezwe na jukumu hilo lote wameachiwa serikali mfano elimu bure, Afya kwa wananchi na Miundombinu ya kisasa
 
SAWA
 

Attachments

  • 20220830_080032.jpg
    20220830_080032.jpg
    176.3 KB · Views: 8
Mshamba huyo jimboni kwake watu wanateseka hakuna barabara mpaka kwenda huko Kibakwe, Rudi,mbuga,kinusi,matonya,galigali,winza,mang'arisa,kikuyu,ipera ni Bora utoke Mpwapwa uje Hadi Dom town uanze kuitafuta Mtera ndipo uingie kwa wapiga kura wake analingia uchawi wao Ila 2025 atatoka tu
 
Kwani kuna mtu kasema maini yanayofauti?yeye mafuta ya gari si anawekewa na serikali?atajilinganisha na Mtanzania wa kawaida?
 
Je, kwanza wao kama viongozi watakubali kuendeshwa kwenye gari za kawaida na je, pia watakubali posho za siku za wabunge zipungue hadi elfu 50?Wasione wao ndio wana nafasi ya kula mema ya nchi bila kuhojiwa.
 
Yaani kaaa kwa kutulia mtoto mdooooogoooo, mnuka jasho ,kubwa jinga lisilo na akili a.k.a MNYONGE, sasa kwa taarifa yako kila mwaka v-8 za billions 600 zinaagizwa, V-8 MOJA NI MILLIONS 500 SAWA NA KITUO CHA AFYA

Zinajazwa mafuta full tank, full Ac na hakuna kuzimwa hata kama boss yuko bar na mrembo wa bongo movie wanakula manyama na kushushia na ma wine toka ufaransa

Kaa kwa kutulia weweeeee unalalamika tozo unadhani watoto wako watsomea kwenye nini bila tozo? madarasa yatajengwaje? vituo vya afya vitajengwaje?

Najua mimacho umetolea kwenye v-8 , yees ni lazima kila mwaka model mpya ikitoka waheshimiwa waipate sababu wanaumiza sana vichwa kuwatumikia nyie wanuka jasho msio na shukrani

Mmeletewa hadi wachezaji toka brazil, argentina kwenye team iliyoko singida lakini bado hamna shukrani, hela yenyewe ndogo inayovamiwa kwenye vi account vyenu mnaiona nyiiingi wenyeeewe, LAZIMA MUUMIE LA SIVYO SHULE NA ZAHANATI HAKUNA NAMBA NYINGINE YA KUJENGA

UNAIJUA V-8 WEWEEEEEEEE? MTOOOOTO M-LITTLE, MNUKA JASHO, KUBWA JINGA



v81.JPG


v82.JPG


tozovx.jpg
 
Na Yale ma V8 ambayo yanaungurumoshwa siku nzima ndio hayo haya na sisi tunaotumia.

Hivi anadhan ni watanzania wa ngapi wana uwezo wa kununua hayo maini anayo kula yeye au hio robo kuku anauoingelea Madwlu wa ngapi wana weza I nunua
 
daah easy tu na watanzania wanakuelewa kabisa
hebu nenda afaganistan ukawajibu kijinga namna hiyo
 
Na Yale ma V8 ambayo yanaungurumoshwa siku nzima ndio hayo haya na sisi tunaotumia.

Hivi anadhan ni watanzania wa ngapi wana uwezo wa kununua hayo maini anayo kula yeye au hio robo kuku anauoingelea Madwlu wa ngapi wana weza I nunua
V8 na mwendokasi hazina tofauti mkuu, Akutukanaye hakuchagulii tusi
 
Kasema ukweli .LAKINI MIMI NAONA TUSIBIRI MAJIBU YA SENSA YA WATU NA MAKAZI .ITAKUWA UFUMBUZI MAANA KILA HUDUMA ITAKUWA WAZI .HAKUNA SIASA MAANA DATA ZITAKUWA SAHIHI HAKUNA TENA UJANJA UJANJA .MFANO MAHITAJI YA WAZEE TAYARI WATAKUWA WANAJULKANA NA HAWATASEMA NGOJA TUFANYE UPEMBUZI YAKINIFU.
 
Daah tuna viongozi wenye uwezo mdogo sana wakufikiri au Wamejaa dharau wakifahamu kuwa wanaolinzi dhidi ya raia.
Kwa viongozi tulionao nchi itaendelea kuwa maskini, na ipo siku watakosa uhuru wa kutembea uraiani na pesa wanazoiba itawalazimu wakazifanyie starehe nje ya Tanzania.
 
Mheshimiwa Waziri Simbachawene ameyasema hayo Leo wakati akijibu maswali yanayohusiana na malalamiko ya tozo akiwa sambamba na Waziri wa Fedha Mheshimiwa Mwigulu Nchemba

Simbachawene amesema watu lazima watambue maisha yana badilika kila wakati na kwa sasa binadamu anamahitaji mengi sana kama simu na TV ambazo hazikuwepo wakati huo hivyo Leo watu wengi wanaishi maisha mazuri zaidi ukilinganisha na zile zama ambazo TV tulijazana kwa majirani kundi la watu kutazama

Simbachawene amesisitiza kwa sasa watanzania wana mahitaji mengi hivyo wananunua data au bundle, wanalipia ving'amuzi vya TV, Kuna luxiary nyingi sana kwa sasa ndio maana watu wanaona maisha màgumu lakini Kiuhalisia wakati huo zamani ndio maisha yalikuwa magumu zaidi hakukuwa na huduma bora kama za sasa

Simbachawene amesisitiza kuwa watu wasifikiri wao viongozi wanaishi tofauti au maisha mengine kwani Maini ya nyama ya ng'ombe anayenunua Yeye au Mawaziri ni yale yale ya buchani kama watu wengine wanayokula

Waziri Simbachawene amesisitiza lazima kwa dhama hizi kelele zikijitokeza mtandaoni mfano tozo zijibiwe kwa wakati kwani watu wakiacha kupotosha mambo ya uchumi wananchi watafikiri jambo hilo ni kweli, Amesisitiza mambo ya uchumi na Sera mtu sahihi wa kuliongelea ni Waziri wa Fedha na sio mtu mwingine

Simbachawene amesisitiza kuwa wakati huo watu walikuwa na maisha màgumu sana mfano Yeye alienda shule Mazengo Sekondari akiwa ana suruali moja tu lakini Leo vijiji vingi vya Tanzania watu angalau wanaweza hata kuvaa chacha au sandles za wazi shule

Waziri amehitimisha kuwa tozo zinazokusanywa ni kwa maslahi mapana ya Taifa na hivyo watu wanapoongelea maisha Leo magumu hawafanyi ulinganifu makini kwani kwa sasa maisha sio magumu bali mahitaji yameongezeka mfano watu wanataka kula milo mitatu na kupanda boda boda kwa kilomita moja, Miaka hiyo watu walitembea kwa miguu hivyo maisha yalikuwa magumu sana

Akichangia hoja hiyo kwa basha basha Waziri wa Fedha bwana Mwigulu Nchemba amesema hata Yeye anashangaa Leo hii watu wanakula robo kuku, au Nusu kuku lakini miaka ile mfano Yeye walikuwa watu 11 kwenye Familia moja hivyo kuku akipikwa wakigawa hata neno paja utalisikia tu kwani paja linaweza kugawanywa hata mara tano ili watu wale chakula

Mheshimiwa Mwigulu Nchemba amesisitiza kuwa hata Yeye ni maskini na anafahamu maisha kwani ndio amekuwa nayo kijijini hata Yeye hapendi kutoza watu kodi na pia hata Mheshimiwa Rais hapendi hilo lakini wananchi wana mahitaji muhimu wanayotaka yatekelezwe na jukumu hilo lote wameachiwa serikali mfano elimu bure, Afya kwa wananchi na Miundombinu ya kisasa
Pumba tu zimeongelewa hapa
 
Back
Top Bottom