Waziri Simbachawene, kama umekiri Wasomi hawawezi na hawapendi kushika Silaha, kwanini huwa mnawalazimisha waende Mafunzo ya JKT?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,518
108,793
Wakati GENTAMYCINE nikisubiri Jibu lako Waziri Simbachawene nitoe tu Ushauri wa bure kwa Viongozi na Watu maarufu nchini hebu ajirini Wasemaji wenu ili wawe wanawafichia Mapungufu yenu ya Kiuwasilishaji kwa kuna Kauli zingine huwa mnazitoa na kutupa hata Mashaka kama kweli mlipita Shuleni na Vyuo Vikuu.
 
Intelijensia ilibaini kuna viashiria vya uvunjifu amani - Polisi aisiye msomi.


Tanzania: Wasio wasomi ndio wanaintelijensia
Majuu: Wasomi ndio wanaintelijensia
 
Sehemu pekee tu Waziri Simbachawene aliyonikosha na GENTAMYCINE namshukuru sana ni Kuamua kumpa rasmi Uraia Mchezaji wa Simba SC na Taifa Stars Kibu Denis ambaye kuna Klabu Moja yenye Roho Mbaya Tanzania nzima (nimeisahau Jina) baada ya Wao Kumkosa wakazusha si Raia wakisahau hata Kocha wao wa Vijana na Mmoja wa Kiongozi wao Mwandamizi wote Kiasili si Raia wa Tanzania.
 
Simbacheweni alikua utingo kwenye mabasi ya urafiki ya Joseph Chove ruti ya mpwampwa - dodoma unategemea aongee nini Mkuu?
 
Hivi kwani wanasiasa wa hapa ni sawa na wanasiasa wa nchi zingine?

Kwamba rais wa hapa ni sawa na hao marais wengine tunaowasikiaga kwenye maredio?

Yaani namaanisha mfano PM wa hapa ni sawa na PM wa EU au Asia? nk.

Sasa, kama hayo maswali juu majibu yake ni 'hapana' basi sina tatizo, lakini kama majibu ni 'ndio',

Naomba kuuliza:
Ni kauli gani ambayo ikitolewa na mwanasiasa inaweza kumlazimisha aachie ngazi? Either kwa kujua alivyokosea au kushinikizwa na umma. Au ndio kila kitu mpaka aliyemteua mtu aamue.

Kiulweli hii kauli haina afya ka waliotajwa na hata tulio na ndugu walioko huko tunajisikia vibaya kwa kauli hii
 
Simbacheweni alikua utingo kwenye mabasi ya urafiki ya Joseph Chove ruti ya mpwampwa - dodoma unategemea aongee nini Mkuu?
Mkuu huwezi amini umenifanya nicheke mpaka nimemgonga kwa bahati mbaya Abiria wa Pembeni yangu katika Daladala ambaye alikuwa amesinzia na Kutoa Miudenda tu.
 
Hivi kwani wanasiasa wa hapa ni sawa na wanasiasa wa nchi zingine?
Mkuu kwa kujua kuwa Kanda ya Ziwa inatoa mno Watu Intelligent ( Einstein ) ukianzia na Mkoa 'Uliobarikiwa' wa Mara ( Musoma ) na mingineyo sikudhani kuwa mwana Kanda ya Ziwa Waziri Simbachawene angekuja na Boko la namna hii.

Nimesikitika...!!
 
Kaongea ukweli, kwani tangu huko nyuma waliokuwa wanapata nafasi hiyo elimu yao ilikuwa ya kawaida tu. Ukiona polisi ana elimu kubwa ni ama alijiendeleza akiwa ndani ya utumishi huo au aliingia akiwa na elimu kubwa kutokana na hitaji la nafasi hiyo kutokana na polisi kuwa na vitengo vingi vyenye kuhitaji taaluma mbalimbali.

By the way hata darasa la saba anaweza kuwa polisi na akafanya majukumu ya ulinzi na usalama wa raia vema. Huko nyuma ilikuwa si rahisi mhitimu mwenye elimu kubwa kukimbilia kazi ya upolisi, siku hizi wanakimbilia kutokana na urahisi wa kupata ajira hiyo kuliko kukaa mtaani huku una elimu ya kutosha.

Kwanza kazi ya upolisi si kazi legelege ni kazi ya nguvu na mapambano inapobidi, ni lazima uajiri wenye moyo na kazi hiyo. Wenye elimu kubwa wanaringia elimu zao na wanadharau kazi ya upolisi.
 
Polisi waendelee kuajiri hao wanaodhaniwa wana elimu ndogo, kwani suala elimu kubwa na ndogo ni mchakato tu wa kupata fursa ya kusoma, kuna ambao wanatamani kupata elimu ya chuo kikuu lakini kutokana mchakato wake kuwa na vikwazo na vizuizi vingi kitaaluma wengi huishia njiani,

hawafiki elimu ya juu inayotakiwa hasa. Haijulikani kuna siri gani elimu ya juu kuchagua wachache ikiwa wengi wanaitaka elimu hiyo.

Ifahamike kuwa mwanafunzi haendi shuleni\chuoni kufeli, kule ni kupata maarifa na stadi tu, haya matokeo na upuuzi mwingine kutangaziana kufeli na kufaulu ni namna tu ya kupata idadi ndogo ya watakaoruhusiwa kuendelea na masomo ya juu.

Hata hawa wanaoachwa bado wana akili nyingi kupata ajira wanayoomba. Usomi ni kupata taarifa, stadi na maarifa ya kufanya kazi fulani na kutatua changamoto zinazoikabili jamii.

Kwa hiyo hakuna askari mwenye elimu kubwa na ndogo katika utekelezaji wa majukumu yao. Vyeo walivyo navyo ni itifaki tu ili kazi ifanyike kwa ufanisi na weledi.
 
Division 32
FB_IMG_1634026238191.jpg
 
Lengo kubwa kabisa la kuanzishwa kwa JKT haikuw kwa ajili ya kuwaanda vijana kuwa askari.
 
Back
Top Bottom