Bandamwagaz
Member
- Feb 19, 2020
- 18
- 36
(PICHANI): Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, akisalimiana na Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Pwani, SSP Mhandisi Joseph Shilinde, Mjini Kibaha, leo, wakati alipokua safarini akitoka Dar es Salaam kuelekea Jijini Dodoma.
Waziri huyo amemaliza ziara yake jijini Dar es Salaam ambapo alitembelea Magereza ya Mkoa huo na aliwataka Magereza waendelee kujitegemea na waongeze kasi ya uzalishaji. Pia alilitaka Jeshi la Magereza Mkoa huo, kuanzisha kilimo cha Mboga za Majani na Matunda ili kuendelea na kasi ya uzalishaji katika Magereza Nchini.
Akiwa njiani kuelekea Jijini Dodoma, leo, alipofika Maili Moja Kibaha, Mkoani Pwani alisalimiana na Mkuu wa Usalama Barabarani na kuwapongeza askari wa Usalama Barabarani kwa kazi nzuri na kuwataka waendelee kuchapa kazi kwa weledi.
Waziri huyo amemaliza ziara yake jijini Dar es Salaam ambapo alitembelea Magereza ya Mkoa huo na aliwataka Magereza waendelee kujitegemea na waongeze kasi ya uzalishaji. Pia alilitaka Jeshi la Magereza Mkoa huo, kuanzisha kilimo cha Mboga za Majani na Matunda ili kuendelea na kasi ya uzalishaji katika Magereza Nchini.
Akiwa njiani kuelekea Jijini Dodoma, leo, alipofika Maili Moja Kibaha, Mkoani Pwani alisalimiana na Mkuu wa Usalama Barabarani na kuwapongeza askari wa Usalama Barabarani kwa kazi nzuri na kuwataka waendelee kuchapa kazi kwa weledi.