Waziri Simbachawene amwagiza IGP kuwapangia kazi nyingine matrafiki wenye vitambi. Je, ni kosa askari kuwa na kitambi?

Mkuu umenichekesha Sana kinaweza ingilia vp utendaji mkuu...

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuingiliaje utenda kazi mkuu au kuleta uzembe na usingizi kazini?
Kuna namna nyingi mkuu..

1. Wewe Unaongea na bosi wako hujampa hata mkono, tayari kishamsukuma..

2. Barabarani, unasimamisha gari kusoma vibali, leseni, bima n.k unamsogelea dereva chini tayari ushamsaidia kufuta bonnet,

3. Ofisini umekaa kwenye kiti, chenyewe kinatakaa kikae kwenye meza,

4. Mda mwingine hata Afande anaweza akuulize..
Mbona hujachomekea?....
Kumbe mkanda umefunikwa na tumbo..

5. Unaenda uwani fasta, lakini kuitafuta bakozi ufungue mkanda mpaka uiname ukipush juu kwanza, la sivyo unajikojolea...

6. Unaendesha gari, tumbo tayari linasukuma usukani, alieoko pembeni yako naye tayari lipo kwenye dashboard,

7. Unapiga Salute, mguu haufiki juu inavyotakiwa maana chenyewe kinausukuma chini,

8. Unaenda kula mgahawani, unatoka tayari kilishanawa kwenye sink, kimepangusa meza, kishaonja mchuzi.

9. Kila baada ya mda inatakiwa uchungulie kama shati halijachomoka au au hakija fungua kifungo cha shati, Ndio maana Maana wenye vitambi kila saa unaona ana seti mkanda na kushika shika tumbo.

10. Unaitwa, unatakiwa ukimbie, chenyewe kinacheza dance,

Yaani kwa ufupi kinaweza kikukosanishe na mtu.

Wakuu ni nyingi sanaa, hapo nimezungumzia mazingira ya kazi, kwa ufupi tuepuke hii kitu...
 
Huwa nakuelewa sana "Retired". Ila nimeshangaa kuona unapinga hili. Kuna watumishi wakiwa na vitambi hatuwezi kuhoji wala kushangaa. Lakini kwa Askari kuwa na Kitambi haipendezi hata kidogo na ni ishara ya mtu mvivu na Mzembe. Askari anatakiwa kuwa Mwepesi.
Tunaweza ku draw conclusions nyingi!
1. Hakuna mazoezi ya kijeshi ya kutosha polisi na hivyo kuwe program ya kuwavunja mifupa na mazoezi kuondoa mafuta
2. Wanashiba sana bila mazoezi kutokana na kula rushwa
3 Au ni wagonjwa, which is most unlikely
 
Waafrika tuna asili ya unene...aache ujinga. Mimi nilipokuwa chini ya miaka 30 nilikuwa nawacheka sana watu wenye vitambi...nilikuwa nawaita manyama uzembe.

Ila sasa kitambi changu karibia kinagusa chini, GYM zote nimemaliza hadi yale madawa ya Forever Living yanaitwa C9.

Kama hayajakukuta shukuru Mungu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Piga malimao,tangawizi na maji ya moto kila siku.Acha kunywa maji ya baridi au vinywaji vya baridi.Baada ya muda urudi utusimulie kama kitambi hakijaisha...
 
Ninachokumbuka mimi mzee ametumikia JW
Lakn alikuw ananimbia askari inatakiw kula mwa nidhamu (kula kula hovyo haitakiwa akiw njiani na kwenye migahawa hasa wakiw katk uniform)
Sasa kizazi hiki unawez kuta hawa ndugu zetu anakula kwenye vibanda asubuh amepga chai nyumbn akiw saiti tena anapg supu na machapat+ Soda au bia
Mchanga kapg zake wali/ugali nyama nusu + bia jion kidogo chips kuku Akirud nyumbn anakula tena , ucku anatoka anaend grosali ya karbu na kwake anapga bia zake 5 anaend kulala wew kwann kitamb kiseje tuuu
NB:- ila wengine miili yako kitambi ni kama asili maana kuna watu wana maisha tyt lakn kitambi hichooo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waziri Simbachawene amemwagiza IGP kuwaondoa trafiki wote wenye vitambi na kuwapangia kazi nyingine.

Najiuliza, ipo sheria inayokataza trafiki kuwa na kitambi? Shughuli ya utrafiki Ni ngumu kuliko majukumu ya OCD, OCS na RPC?

Natamani awamulike pia hao, ila pia tofauti na utrafiki kazi zilizobaki polisi zote ngumu na nzito hivyo sidhan Kama Kuna kitengo kinachofaa zaidi

Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Geogre Simbachawene, amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro, kuwaondoa askari wa Usalama Barabarani wenye vitambi na kuwapangia kazi nyingine kwani wamekosa sifa. Ametoa kauli hiyo wakati wa Kongamano la Usalama Barabarani lililofanyika jijini Dodoma lililoandaliwa na TAMWA kwa kushirikiana na Asasi za Kiraia zinazochochea mabadiliko ya Sheria ya Usalama Barabarani ya mwaka 1973.

"Wapo trafiki wanastahili kuondolewa kwa kukosa sifa ya kuwa trafiki! Kwa mfano wa trafiki wa Gairo wana vitambi! Askari anakuwaje na kitambi? Namuagiza IGP kuwaondoa askari wote wenye vitambi na kuwapangia kazi nyingine, amesema Waziri Simbachawene.

Waziri Simbachawene ameongeza kwa kusema kuwa wapo askari wasio waadilifu wanaotumia sare na kofia zao kula rushwa. "Wapo askari wa usalama barabarani ambao wamegeuza 'crown', sare nyeupe na kofia kudai rushwa kutoka kwa bodaboda, malori na kirikuu!! Naelekeza trafiki kufanya kazi kwa weledi! tuache kusimamia sheria kwa mazoea!”, amesisitiza

Amesema kuwa ajali zimekuwa zikigharimu serikali kurekebisha miundombinu, kufanya uokozi na kupoteza nguvu kazi ya taifa. "Ajali hizi zimekuwa zikiigharimu serikali kurekebisha miundombinu, kufanya maokozi na kupoteza nguvu kazi ya taifa.

Vilevile, Waziri Simbachawene amesema kuwa wapo madereva wanaendesha magari wakiwa wamelewa; wapo watembea kwa miguu wanavuka barabara wakiwa wamelewa; wapo madereva wanaendesha mwendokasi hatarishi katika maeneo ya makazi ya watu au yasiyoruhusiwa na alama za barabarani.

Katika kongamano hilo Waziri Simbachawene aliahidi kwamba mapendekezo hayo ya maboresho ya Sheria yaliyotolewa na wadau yatapelekwa Bungeni baada ya mchakato ndani ya Serikali kukamilika. "Serikali kupitia wizara yangu ipo katika mchakato wa kurekebisha Sheria ya Usalama Barabarani 1973, ili iweze kuendana na mahitaji ya sasa", amesema Simbachawene

"Kongamano la usalama barabarani ni siku muhimu sana ya kukumbushana kuhusu masuala mbalimbali ya usalama barabarani. Masuala hayo ni pamoja na kuwakumbusha madereva juu ya kuwa waangalifu na kuzingatia sheria", amehitimisha Waziri Simbachawene.

Ripoti ya usalama barabarani ya Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) iliyotolewa mwaka 2018, inabainisha kuwa Sheria za Tanzania zina upungufu katika kudhibiti usalama barabarani, ikiwemo kuruhusu kiwango kikubwa cha ulevi kwa madereva bila kujali uzoefu wa dereva katika kazi husika.

Tanzania imeweka ukomo wa kilevi kuwa ni 0.08g/dl lakini WHO inaeleza kuwa dereva mwenye kiwango hiki cha ulevi anakua hatarini kupata ajali mara nne zaidi ya yule ambaye hajatumia pombe kabisa. WHO pia wanashauri kuwa ni vizuri ukomo wa ulevi ukawa ni 0.05g/dl kwa madereva wazoefu na 0.02g/dl kwa madereva wapya wasio na uzoefu.
Keshokutwa atasema askari wenye vichwa vikubwa waondolewe jeshini, maana vichwa vikubwa vinakuwa havienei kwenye kofia
 
Polisi na wanajeshi wanakuwa na masaa ya mazoezi ya viungo kila wiki, haya yanahesabiwa katika masaa yao ya kazi. Kitambi ni ushahidi kuwa mmiliki alipokea pesa bila kufanya mazoezi ya viungo kwa mujibu wa mkataba.
Hao wanaamkia mabarabarani usiku usiku kuwahi 'tip'hata zile siku ambazo ni za mazoezi wao hawaendi.

Heshima bandia wanazopewa na madereva wenye mapungufu barabarani pamoja na rushwa zinawafanya waamini kuwa adabu hizo ni za kweli na kupokea pesa bila kutoa ni haki yao ya kudumu!

Kwanini kitambi kisifutuke, tena bila kujali mhusika ana cheo gani!

Trafik police kumpangia kazi nyingine, yaani akalinde benki, kutuliza ghasia, kukabiliana na majambazi uso kwa uso ni sawa na kumfukuza kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waafrika tuna asili ya unene...aache ujinga. Mimi nilipokuwa chini ya miaka 30 nilikuwa nawacheka sana watu wenye vitambi...nilikuwa nawaita manyama uzembe.

Ila sasa kitambi changu karibia kinagusa chini, GYM zote nimemaliza hadi yale madawa ya Forever Living yanaitwa C9.

Kama hayajakukuta shukuru Mungu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu dawa ya asili ya kuondoa kitambi mbona inaeleweka na ni rahisi sana?

Weka pembeni uboss kamata jembe mwenyewe bila kujihurumia, pamoja na mazoezi ya kawaida, miezi 6 ni mingi tatizo litaisha.

Mwili ukirudi kawaida usibweteke, maana kitarudi kwa kasi ya upepo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Obesity Warning for Police Officers: Police officers are law-abiding citizens who wear a uniform to enforce the laws. They have the right to remain obese, but it can and will be used against them in the line of duty. This study discusses the need for police departments to institute programs that prepare and maintain healthy officers who can perform their jobs well throughout their careers. The study reveals the absolute need for police officers to be physically and mentally fit and argues that obese and unfit officers are dangers to themselves and to the public. Recommendations are made for police departments and officers to utilize in recruiting and training future officers and in educating veteran officers in order to maintain healthy and fit police officers. Although society is responsible for the kind of police it chooses to have, but policing is a physically demanding occupation and too important to be left to the unfit individuals"
Waziri yuko sahihi,tafiti zimefanyika vitambi kwa polisi ni hatari na aibu. Na kwanini vitambi viwe kwa traffic tu? Tujiulize. Jibu ni rahisi, rushwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Polisi na wanajeshi wanakuwa na masaa ya mazoezi ya viungo kila wiki, haya yanahesabiwa katika masaa yao ya kazi. Kitambi ni ushahidi kuwa mmiliki alipokea pesa bila kufanya mazoezi ya viungo kwa mujibu wa mkataba.
Neno 'Mmiliki' 😂😂😂😂
 
Nakumbuka kaka yangu RIP alipokua anasomea udaktari waliulizwa swali "Obesity is malnutrition, discuss'
Kwa kweli trafiki wengi ukiwakagua utakuta ndani mle sio nyama ila ni kinyesi kilichochacha, kama umeshakua karibu na choo ambacho trafiki yuko ndani anashusha mzigo utanielewa ba utajua barakoa si mpaka korona
 
Tunaweza ku draw conclusions nyingi!
1. Hakuna mazoezi ya kijeshi ya kutosha polisi na hivyo kuwe program ya kuwavunja mifupa na mazoezi kuondoa mafuta
2. Wanashiba sana bila mazoezi kutokana na kula rushwa
3 Au ni wagonjwa, which is most unlikely
Haaahaa!! Yote hayo ndiyo majibu hasa. Ila Polisi wakiamua kufuata Misingi ya uaskari nadhani inawezekana kumaliza suala la vitambi na kubaki tu wale wagonjwa.

Jana imebidi ni Google kuangalia obesity & overweight kwa Askari. Nikakuta kumbe wenzetu weupe wanayo sheria kabisa na ikionekana imeshindikana kuendana na kanuni hiyo unaweza hata kuachishwa Nazi.
America, China, Europe, India nk
 
Wao ni watu lkn kulingana na kazi yao waliojichagulia hawapaswi kuwa na vitambi. Na kwanini uwe na ulaji mbovu wenye kusababisha mafuta ya ziada yasiyohitajika ikiwa wewe ni askari? Askari hapaswi kuwa na kitambii ataclow vipi vitani na mtambi ka zigo la mwizi?
Wenye vitambi si Askari pekee
 
Mheshimiwa Waziri. Umefanya utafiti wa kutosha kabla ya kufikia huo uwamzi ? Je ni kweli Vitambi vinahusiana na utendaji duni wa Kazi ya Traffic Police. Kama Traffic Police wa Gairo ni wazembe ni tu lakini siyo sababu ya vitambi. Wapo wasivyo navyo lakini ni wazembe na wapo wanavyo lakini ni wachapa Kazi mwanzo mwisho.
 
Wanatakiwa kuwa fiti muda wote, vitambi sijui wanatoa wapi!!!
 
Back
Top Bottom