Waziri Simbachamwene ametudhalilisha Polisi

Japo wote wanafanana na walioishi form four na kupata division four. Kiongozi wenu wa juu ndio shahidi wa hili.
Simbachawene alishakamatwa na polisi akiwa waziri wa TAMISEMI kwa makosa ya usalaama barabarani aluposhuka tu alianza kuwaambia askari namaana huoni bendera? Wakamwambia tatizo siyo bendera tatizo ni mwendokasi sehemu ambayo hairuhusiwi JPM alimwambia lipa faini umeyataka mwenyewe acha askari wafanye kazi yao tangu kipindi hicho ana chuki na askari polisi! Idara ya polisi siyo kwamba ni idara ambayo ina wafanyakazi walioishia kidato cha nne wapo wenye elimu kubwa! Kama idara nyingine.
 
Kauli aliyoitoa jana kwamba jeshi la polisi halihitaji watu wenye ufaulu mkubwa kwasababu kazi ya polisi ni kucheza gwaride na kuilinda Benki ni ya udhalilishaji sana.

Mimi wiki kadhaa nyuma niliponea chupuchupu kufa kwa kipigo, baada ya wananchi kujua Mimi ni polisi.

Maumivu hayajaisha bado nakuja kutukanwa na waziri wangu.

Watoto wangu wanajua Mimi nilikuwa nakuwa wa kwanza darasani, na pia wanajua kuwa mtihani wa form 4 nilipata one ya point 7.

Kauli ya waziri imesababisha watoto wangu waniulize maswali magumu ikiwemo kuniomba vyeti vya taaluma ili wapime Kati yangu na waziri nani ni muongo.

Waziri Simbachamwene tuombe radhi ASAP
Heheheh njagu bana
 
Back
Top Bottom