Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,024
- 13,821
Waziri Silaa ametoa maagizo hayo leo tarehe 16 Desemba, 2024 wakati akizindua Bodi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), jijini Dar es Salaam.
Amesema kuwa maagizo hayo yanakuja kufuatia maelekezo mahsusi yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 10 Desemba, 2024, Ikulu ndogo ya Tunguu Zanzibar wakati wa hafla ya uapisho wa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Naibu Makatibu Wakuu na Mabalozi kuhusu usimamizi wa shirika hilo kujiendesha kibiashara.
"Nia ya Rais ni kuona uwekezaji huu mkubwa unaleta tija nchini." Amesema Waziri Silaa na kuongeza;
"Shirika hili likiendeshwa vyema lina uwezo wa kusaidia sekta nyingine, kwa sababu wizara yetu ni wezeshi katika mawasiliano, hivyo wizara nyingine na Taasisi zinaitegemea katika kukuza sekta zao za TEHAMA."
Bw. Nchimbi amemshukuru Waziri Silaa kwa utayari alioonesha na kuahidi kuwa bodi itatoa ushirikiano kwa wizara wakati wote itakapokuwa inatekeleza majukumu yake.