Waziri Salome Mbatia afariki dunia, maswali yaibuka!

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,888
Nimepata habari muda huu huu kwamba ajali mbaya imetokea Wilani Njombe , na katika ajali hiyo Mh.Salome Mbatia amefariki. Mtoa taarifa hakuweza kunieleza zaidi maana alikuwa na wasi wasi ila kasema miongoni mwa walio fariki ni waziri Salome Mbatia .

Mengine nitayasema kwa kadiri nitakavyo weza kuyapata .
 
Habari nilizozipata sekunde kadhaa zilizopita ni kuwa Ajali nyingibe Mbaya imetokea huko Iringa, iliyomhusisha Salome Mbatia.

Habari zinasema kwamba amefariki dunia!
Bado tunaendelea kufuatilia jinsi ilivyotokea!
 
tusubiri tusikie zaidi manake tusije kutoa pole na pengine yupo hai.

invisible......hebu twambie khabari hii.

mkuu umeanza kuelewa sasa ?

hapa jamvini tumepunguza sana credability, kwa kuleta habari ambazo baadae zinakuja bainika kuwa si za kweli.

wacha tusubiri kwana, hatuwezi kusema si kweli wala ni kweli hadi tuzithibitishe kwa vyanzo vingi au kwa wale ambaowanaaminika kuwahawajawahi kutudanganyana
 
Mtu wa Pwani test yako ni nzito sana "mtu anayeaminika au ambaye hajawahi kutudanganya" Mkuu hiyo ni kali.
 
Hapa hadhi bado iko juu ila unaweza wewe pekee ndiye umejipunguzia credibility ama hutaki kuelewa . Habari hizi nimezipata kwa mtu muhimu sana aliyekuwa katika mmojawapo wa misafara akielekea Songea na yuko katika eneo la tukio hilo. Katika watu walio kufa kathibitisha kwamba Ndugu Salome kafariki na mengine atanipa kadiri muda unavyo enda .
 
mkuu umeanza kuelewa sasa ?

hapa jamvini tumepunguza sana credability, kwa kuleta habari ambazo baadae zinakuja bainika kuwa si za kweli.

wacha tusubiri kwana, hatuwezi kusema si kweli wala ni kweli hadi tuzithibitishe kwa vyanzo vingi au kwa wale ambaowanaaminika kuwahawajawahi kutudanganyana

mtu wa pwani......

mie napenda sana jinsi invisible anavyojibu hoja ndio maana nikasema hii habari afuatilie kwa makini.

so far nimewasiliana na washikaji bongo naona hawana taarifa hizo but bado mapema na wao wanajaribu kuulizia zaidi.wanasubiri taarifa ya habari CHANNEL 10 ya saa 1900.
 
Waziri Salome Mbatia amefariki katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Kibena Factory (kati ya Makambako na Njombe)saa 11 kasorobo jioni ya leo. Pamoja naye wamefariki watu wengine wawili. Waziri alikuwa katika gari dogo aina ya Nissan ambalo liligongana na Lori la Fuso lilikuwa limeshehena mbao. Lori hilo liliangukia gari hilo dogo na kuwaua watu hao papo hapo. Ninavyoandika hivi, bado wanajaribu kuitoa miili ya marehemu...
 
Du! Mambo yamekuwa siyo mambo.

Hali inaelekea kubaya sana, inabidi kujiuliza kulikoni?
Mungu awape nguvu za Kustahimili!
 
sasa habari iaminini na nnatanguliza samahani sana kwako lunyungu maana wewe hasa habari zako zina walakin

inna lillahi wa innna ilayhi rajiiun

mola ndie alietupa na mola ndie aliechukua.
mola ape subira wanafamilia yake, ndugu na jamaa zake, rais wa jamhuri ya muungano, viongozi wote wa vyama na serikali. hasa mawaziri wenziwe na wabunge wenziwe
 
Ni kweli Mwanakijiji maana kuna ndugu mmoja yuko hapo hapo anasema hali ni mbaya sana .
 
viongozi ni binadamu wa kawaida tu, kama mtashangaa viongozi kufa kwa ajali sidhani kama itakuwa vizuri kutoshangaa wananchi wanaokwisha kila siku kwa ajali ya gari !
 
nitawaletea taarifa toka eneo la tukio as they become available.. kwa vile bado wako kwenye shughuli ya kunasua miili viongozi wa Polisi hawapatikani na hawajaweza kuzungumzia lolote kwa kirefu. Nilichoweza kupata ni hiyo confirmation ya habari ya Lunyungu na niomba Mods mchukue hayo niliyoongezea na kuyaingiza kwenye original threat ya Lunyungu ...

KLH News.. inamtandao wa kutosha kuthibitisha habari mahali popote Tanzania, tukifanya makosa ya hapa na pale ni udhaifu wetu, lakini hii haina shaka hata kidogo.
 
mwaka huu ni mzito, maana sijui nisemeje, wengine wataanza kushangiria sasa hivi, ila nnawaomba kwa hili tuache na tuhuzunike ni msiba wetu sote na ajali haina bwana wala bibi na wala haina chama. kwa hili tuungane kuonesha huzuni zetu.

pia tukae kujiuliza kwa nn tanzania sasa kuna ajali nyingi na zaidi viongozi? kuna nini? somo gani tunalipata hapa?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom