Waziri Prof. Ndalichako awapiga mkwara mzito Viongozi wa TBA

Miaka hii 5 hakuna cha PPP wala private sectors, hizi private sectors zinapumulia mipira awamu huu
 
Hebu mwambieni huyo Ndalichako kuna fedha aligawa Kwa baadhi ya shule zilizofanya vizuri mwaka Jana,zimefanyiwa nini na wakuu?
Inasadikika wakuu wameziweka matumboni mwao
 
Ukweli kuhusu TBA.

1/Uwezo wao kiutendaji ni duni sana. Wana watumishi wachache, wataalamu wachache na vifaa vya kudumu vichache. Kuwarundikia kazi nyingi na huku ukitegemea kukamilika kwa wakati ni kujidanganya.

2/Utaalamu na uzoefu wa ujenzi wa kisasa TBA hawana na hawawezi kabisa. Miradi mingi waliyojenga imeharibika baada ya muda mfupi mno.

3/Wajenzi binafsi hupenda kushirikisha kandarasi za makampuni tofauti tofauti ili kuharakisha kazi na kupata ubora mzuri, jambo hilo limepigwa marufuku na serikali kufanywa na TBA.

4/Gharama za ukadiriaji wa majenzi wanazopewa TBA kutoka serikalini ni za chini sana. Serikali inatoa pesa kidogo na hapo hapo inategemea mambo makubwa, mazuri na haraka.(Mfano hai ni yale majengo ya pale UDSM)

5/Pesa nyingi wanazopewa TBA ili kujenga majengo mapya huwa wanakimbilia kulipia mapengo ya madeni ya vifaa kwa kazi zilizopita ambazo zilitumia pesa zao za ndani nyingi kupita maelezo. (Mfano ni ule ujenzi wa Hostel za UDSM ambapo makisio ya Magufuli ni kutumia Bilioni 10 tu, wakati uhalisia ni kuwa TBA walitumia zaidi ya Bilioni 50, sasa jiulize tu, hizo bilioni zaidi ya 40 TBA walizitoa wapi na watazirejeshaje?)

6/Sehemu kubwa ya pesa za Kandarasi wanazolipwa TBA zinakwenda kutumika katika kulipa gharama za ndani za uendeshaji wa TBA(Posho za viongozi wake, safari nk) pamoja na usimamizi wa miradi wanayoijenga, na kiasi kidogo sana ndio kinatumika kununua vifaa na malighafi za kisasa na kulipa vibarua au wataalamu wazuri wa kukodi katika ujenzi, katika hali hiyo miradi karibu yote ya TBA itaendelea kusuasua daima.

7/Baadhi ya wataalamu wa kukodiwa wa ujenzi wanaombwa na TBA kuja kujenga majengo yao hulipwa pesa kidogo sana. TBA inafanya hivyo ili kubakia na ziada ya kutosha kwa kuwa kandarasi zao kutoka serikalini huambatana na malipo duni yasiyoendana na uhalisi wa gharama za ujenzi wa kisasa.
 
Hii style ya serikali kujiingiza Kwenye ujenzi badala ya usimamizi ilishashindwa Lakini serikali Hii inalazimisha. Yaani badala ya kwenda mbele tunarudi nyuma. Very sad
 
Mradi wa mloganzila ni mradi mkubwa na waheahima ktk taifa letu, maendeleo yake yanapaswa yafuatiliwe na kusimamiwa kwa ukaribu sana ili isije kuhujumiwa na wasio penda maendeleo.
 
Waziri wa Elimu, Joyce Ndlichako ametembelea mradi wa ujenzi wa madarasa, Hostel na ofisi kwa ajili ya chuo kikuu cha Muhimbili Kampasi ya Mloganzila ambapo baada ya kutembelea mradi huo hakuridhishwa na maendeleo ya ujenzi huo ambao unasimamiwa na wakala wa majengo Tanzania 'TBA'.

Kutokana na kutoridhishwa huko ametoa wiki moja vifaa vya ujenzi viwe vimefika na mafundi wa kutosha waongezwe vinginevyo amemuagiza katibu Mkuu wa wizara hiyo kuangalia namna ya kuvunja huo mkataba


Mama naona hajui kuwa bosi wake ni mpigaji kupitia TBA
 
Sekta binafsi wengi hawa wazawa nao walijenga vitu visivyo imara. Kuna chuo flani cha umma miaka ya 2004 hadi 2008 walijenga Theatre Halls za ajabu. Miezi michache tangu kuzinduliwa zilitokea nyufa.

Tuna tatizo na wahandisi wengi wazawa kuwa na uwezo mdogo kwenye ufanyaji kazi kwa vitendo. Kuanzia usimamizi hadi utendaji kazi wenyewe.
mmh

sio kweli
 
January 21, 2018
Wana-Jamiiforums tushuhudie video wenyewe site /eneo la "ujenzi" ulivyo ktk mradi wa hosteli zilizo chini ya chuo kikuu cha tiba Muhimbili MUHAS hospitali ya Mlongazila. Ujenzi huo wa hosteli, jengo la maakuli, maabara na jengo la mafunzo umekwama kwa sasa.

Mfumo wa kikazi serikalini umefeli kwa kuingiza siasa ktk kazi za kitaalamu. Naona waziri wa elimu amechambua kitaalamu matatizo ya wakala wa ujenzi wa serikali TBA KUPEWA kazi kisiasa huku uwezo wa kutimiza miradi hiyo kwa wakati TBA hawana.

Kazi kwake waziri wa ujenzi kumshauri Rais na waziri Mkuu kubadilisha mfumo wa utendaji serikalini.

 
Siyo kosa la TBA lakini...

Wao walikua wasimamizi zaidi kuliko wajenzi... Ghafla wamepewa tenda za ujenzi, hawakujiandaa...


Ni sawa leo hii TAMESA ipewe tenda kubwa kubwa za kutengeneza magari yote Tanzania nzima, patakua hapatoshi...


Cc: mahondaw
 
Huyu mama naona sasa anataka pishana na Ngosha...

Not knowing what is behind TBA....

Atapigwa figisu la hatari ang'olewe...
 
Basically TBA walikuwa wasimamizi. Sasa Magu kawafanya wajenzi wakubwa. Hawakuwa tayari kwa hilo. Kati ya usimamizi na ujenzi wachague moja.
Pamoja na kuongezewa majukumu wamenyimwa kibali cha kuajiri, kwahiyo wanastaff wachache sana ambao wanatisha kuwa wasimamizi na wakaguzi zaidi na sio wajenzi
 
Basically TBA walikuwa wasimamizi. Sasa Magu kawafanya wajenzi wakubwa. Hawakuwa tayari kwa hilo. Kati ya usimamizi na ujenzi wachague moja.
Hata hivyo msimamizi (regulayor) wa kanuni za ujenzi na majengo anapogeuka mjenzi nani atamsimamia yeye? Incase ikitokea kavurunda kwenye ujenzi huo nani atamwajibisha wakati yeye ndo msimamizi mwenyewe? Lakini huyu msimamizi (TBA) anayesimamia wajenzi na majengo kumbe yeye mwenyewe hana weledi wa taaluma hiyo huwa anawasimamiaje hao wajenzi? TBA ifumuliwe na kujengwa upya!
 
Kwa hatua alizochukua waziri mkuu ....basi ile issue ya yule dogo aliyetoa picha za expansion joint kwenye hostel za udsm alikuwa sahihi kabisa.....TBA waliboronga

Ova
 
Kwa hatua alizochukua waziri mkuu ....basi ile issue ya yule dogo aliyetoa picha za expansion joint kwenye hostel za udsm alikuwa sahihi kabisa.....TBA waliboronga

Ova
TBA ina staff wachache sana kama hujui mkuu, pia chama ndiyo kinapatia huko hela ya kununua wapinzani.
 
Back
Top Bottom