Hamza Temba
R I P
- Feb 10, 2017
- 20
- 4
Nadhani umesikika leo:
Rais Magufuli amtumbua Vita Kawawa na kuvunja Bodi ya Tumbaku Tanzania.....Waziri Mkuu Kaagiza viongozi wa 'WETCU' Wakamatwe Haraka
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora kuwakamata viongozi wanne wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Tumbaku (WETCU) pamoja na kufunga ofisi za chama hicho kupisha uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu.
Pia Waziri Mkuu amevunja Bodi ya WETCU pamoja na Bodi ya Tumbaku Tanzania - TTB kwa sababu ya kushindwa kusimamia zao hilo pamoja na matumizi mabaya ya fedha za umma.
Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo jioni katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Isike Mwanakiyungi mkoani Tabora, ambapo amesema Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa TTB, Bw. Vita Kawawa pamoja na Mtendaji Mkuu wa Bodi hiyo Bw. Wilfred Mushi.
Viongozi wa WETCU ambao Waziri Mkuu ameagiza wakamatwe ni Mwenyekiti Bw. Mkandara Mkandara, Makamu Mwenyekiti Bw. Msafiri Kassim, Mkaguzi wa Ndani na Mhasibu Mkuu. Pia amewasimamisha kazi watumishi wa kitengo cha uhasibu wa chama hicho hadi uchunguzi utakapokamilika.
“Kuanzia sasa watumishi wote wa kitengo cha uhasibu pamoja menejimenti nimewasimamisha kazi pamoja na Mrajisi wa mkoa wa Tabora Deogratius Rugangila. Kamanda hakikisha ofisi hazifunguliwi kuanzia sasa hadi hapo timu ya ukaguzi itakapokamilisha kazi yake,”amesisitiza.
Waziri Mkuu amesema kwa muda mrefu wakulima wameteseka na zao hilo kukosa tija kwa sababu ya usimamizi mbovu wa viongozi wa ushirika na Bodi ya Tumbaku Tanzania jambo ambalo Serikali haiwezi kulivumilia.
Amesema “Hatuwezi kuwa na ushirika ambao hauwasaidii wanachama. WETCU walipokea sh. bilioni 15 ambazo walizikatia risiti na hazijaonekana. Pia waliwalipa wazabuni sh, bilioni 10 ambazo hawajazikatia risiti,”.
“Wakati wanachama ambao ni wakulima wakiendelea kutesema WETCU walinunua gari la sh. milioni 269 kinyume na maelekezo ya Mkutano Mkuu wa wadau ambao ulipitisha zitumike Shilingi milioni 40 tu,” amesema.
Waziri Mkuu ameongeza kuwa chama hicho kimesababisha kupungua kwa uzalishaji kwa kiasi kikubwa kutokana na kuwa na menejimemti mbovu jambo ambalo limechangia wakulima wa tumbaku kukosa tija.
Amesema WETCU kimekithiri kwa matumizi mabaya ya fedha ambapo alitolea mfano suala la ukarabati wa ofisi tatu ikiwemo ya makao makuu ambayo ilipangwa ikarabatiwe kwa sh. milioni 33 wakatumia sh. milioni 170 na ofisi za Tabora na Urambo zilipangiwa sh. milioni tano kila moja na hazikukarabatiwa.
Pia Waziri Mkuu amepiga marufuku ununuzi wa mbolea kutoka nje ya nchi wakati ikiwa inazalishwa hapa nchini.
Kila siku ni walewale ,utadhani wengine hawapo,wakitoka huku wanapelekwa kule,wakitoka kule wanarudishwa huku,mtu ana diploma anapewa ulaji kila sehemu utadhani hakuna wengine ,hapa wengine wanasafiria nyota za baba zao.Huyu Kawawa si kafumushwa juzi bodi ya tumbaku?
Zungu Pule Ili jamii ya wafugaji isiwe disadvantaged lazima wakubali kubadilisha ufugaji wao kuwa wa kisasa wa mifugo michache na wenye tija. Binadamu na mifugo inaongezeka lakini ardhi haiongezeki.
Ufugaji wa kisasa ukoje? Kama wanavyofuga wazungu? Unataka Wasukuma, Wabarbaig, na Wamasai wafuge kama Wazungu? Unanikumbusha Waziri Mkuu Mizengo Pinda alienda Dubai akaona shamba la ng'ombe kule (ng'ombe wamewekewa mpaka air conditioner na shower kupooza miili yao), akarudi Tz na kusema lazima wataalamu wetu wakajifunze kule ili na sisi tufanye kama wao. This flawed thinking, halafu tunaimba ngonjera za maendeleo. Ndio maana nasisitiza elimu inayotolewa mashuleni inahitaji mabadiliko makubwa. It's very European. Elimu yetu inapaswa kuendana na mazingira yetu. In other words, what is taught in schools should enable students relate to their environments. That's the only way education will contribute to the emancipation of our people from poverty. We must decolonize our knowledge before we can even talk of independence. Fikra za wataalamu wetu wengi sasa hivi hazielekezwi kwenye kuyaelewa matatizo yetu bali kwenye kufanya maisha yetu kufanana na yale ya wenzetu wa Ulaya, America, na baadhi ya nchi za Asia (In other words, our educated people (call them civilized people) are busy trying to apply imported solutions rather than focus on understanding problems for 90% of solutions lie in the correct definition of problems. Problems are never similar. European problems cannot be similar to African problems for many reasons. So, it's insane to have an education system focused on learning or cramming, to be specific, European solutions that were introduced to us through colonialism). This is not an easy argument to understand because you have been conditioned not to understand it. I mean, I am talking about epistemic violence - the one which makes it natural to discriminate against your own people in the name of development.
PS. You are invoking Malthusian argument. Read and you will see that the argument has been thoroughly debunked. If Malthus was right (this is to say, if you are right), the world could have perished long time ago.
Huyu Kawawa si kafumushwa juzi bodi ya tumbaku?