Waziri Prof. Maghembe ateua Wajumbe wa Bodi ya Ngorongoro (NCAA)

Hamza Temba

R I P
Feb 10, 2017
20
4
c0925e4eff03554c66f8effa481e4d4a.jpg
 
Nadhani umesikika leo:

Rais Magufuli amtumbua Vita Kawawa na kuvunja Bodi ya Tumbaku Tanzania.....Waziri Mkuu Kaagiza viongozi wa 'WETCU' Wakamatwe Haraka




Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora kuwakamata viongozi wanne wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Tumbaku (WETCU) pamoja na kufunga ofisi za chama hicho kupisha uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu.

Pia Waziri Mkuu amevunja Bodi ya WETCU pamoja na Bodi ya Tumbaku Tanzania - TTB kwa sababu ya kushindwa kusimamia zao hilo pamoja na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo jioni katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Isike Mwanakiyungi mkoani Tabora, ambapo amesema Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa TTB, Bw. Vita Kawawa pamoja na Mtendaji Mkuu wa Bodi hiyo Bw. Wilfred Mushi.

Viongozi wa WETCU ambao Waziri Mkuu ameagiza wakamatwe ni Mwenyekiti Bw. Mkandara Mkandara, Makamu Mwenyekiti Bw. Msafiri Kassim, Mkaguzi wa Ndani na Mhasibu Mkuu. Pia amewasimamisha kazi watumishi wa kitengo cha uhasibu wa chama hicho hadi uchunguzi utakapokamilika.

“Kuanzia sasa watumishi wote wa kitengo cha uhasibu pamoja menejimenti nimewasimamisha kazi pamoja na Mrajisi wa mkoa wa Tabora Deogratius Rugangila. Kamanda hakikisha ofisi hazifunguliwi kuanzia sasa hadi hapo timu ya ukaguzi itakapokamilisha kazi yake,”amesisitiza.

Waziri Mkuu amesema kwa muda mrefu wakulima wameteseka na zao hilo kukosa tija kwa sababu ya usimamizi mbovu wa viongozi wa ushirika na Bodi ya Tumbaku Tanzania jambo ambalo Serikali haiwezi kulivumilia.

Amesema “Hatuwezi kuwa na ushirika ambao hauwasaidii wanachama. WETCU walipokea sh. bilioni 15 ambazo walizikatia risiti na hazijaonekana. Pia waliwalipa wazabuni sh, bilioni 10 ambazo hawajazikatia risiti,”.

“Wakati wanachama ambao ni wakulima wakiendelea kutesema WETCU walinunua gari la sh. milioni 269 kinyume na maelekezo ya Mkutano Mkuu wa wadau ambao ulipitisha zitumike Shilingi milioni 40 tu,” amesema.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa chama hicho kimesababisha kupungua kwa uzalishaji kwa kiasi kikubwa kutokana na kuwa na menejimemti mbovu jambo ambalo limechangia wakulima wa tumbaku kukosa tija.

Amesema WETCU kimekithiri kwa matumizi mabaya ya fedha ambapo alitolea mfano suala la ukarabati wa ofisi tatu ikiwemo ya makao makuu ambayo ilipangwa ikarabatiwe kwa sh. milioni 33 wakatumia sh. milioni 170 na ofisi za Tabora na Urambo zilipangiwa sh. milioni tano kila moja na hazikukarabatiwa.

Pia Waziri Mkuu amepiga marufuku ununuzi wa mbolea kutoka nje ya nchi wakati ikiwa inazalishwa hapa nchini.
 
Inayo baraka kutoka kwa mfalme


Maghembe watch out Mimi ndio kila kitu ,kipa, beki ,kiungo,mshambuliaji ,kocha
 
Na NCA ni eneo wanaloishi watu (wafugaji wa asili ya Kimasai). Wengi wa wajumbe wa bodi ama ni watu wa "anti-poaching" au watu wanaoshabikia utaratibu wa kikoloni wa kuona wafugaji kama "threat" kwa mazingira. Bodi ya NCAA inapaswa kuundwa na watu wanaoamini katika "people-centered conservation". Ideologies za kutenganisha "human and nature" zitafanya jamii ya wafugaji kuwa-disadvantaged. Sasa kuna minong'ono kutoka kwa baadhi ya watu wenye fikra za kikoloni kwamba wakati umefika wa kuwaondoa Wamasai wanaoishi ndani ya eneo la Ngorongoro. Bodi ya namna hii ni bodi inayoonekana kwamba itabariki fikra za namna hiyo. Labda Aikande Kwayu na Ndugu Manongi wanaweza kuwa mtizamo endelevu. Ila hao wengine hamna kitu. Ifike wakati watu wa kujaza hizi nafasi wapatikane kwa utaratibu ambao ni competitive. Hii tabia ya kuteua wastaafu haitatusaidia.
 
Teh sasa huyo Kawawa na Diploma yake amepenyaje humo..? Huku kujuana huku.. Mshua wangu ulikuwa wapi wakati wazee wenzio wanakamata vitengo
 
Zungu Pule Ili jamii ya wafugaji isiwe disadvantaged lazima wakubali kubadilisha ufugaji wao kuwa wa kisasa wa mifugo michache na wenye tija. Binadamu na mifugo inaongezeka lakini ardhi haiongezeki.
 
*Vita Kawawa alitumbuliwa.. Naona Prof. Maghembe anampima JPM.. Ooohh shauri yake
 
hapo naona wengine ni wastaafu, ingekuwa vyema wangepumzika wale pensheni yao kwa utulivu....

waige mfano wa meck sadik... kuliko kung'ang'ana na nafasi za kuteuliwa
 
Zungu Pule Ili jamii ya wafugaji isiwe disadvantaged lazima wakubali kubadilisha ufugaji wao kuwa wa kisasa wa mifugo michache na wenye tija. Binadamu na mifugo inaongezeka lakini ardhi haiongezeki.

Ufugaji wa kisasa ukoje? Kama wanavyofuga wazungu? Unataka Wasukuma, Wabarbaig, na Wamasai wafuge kama Wazungu? Unanikumbusha Waziri Mkuu Mizengo Pinda alienda Dubai akaona shamba la ng'ombe kule (ng'ombe wamewekewa mpaka air conditioner na shower kupooza miili yao), akarudi Tz na kusema lazima wataalamu wetu wakajifunze kule ili na sisi tufanye kama wao. This flawed thinking, halafu tunaimba ngonjera za maendeleo. Ndio maana nasisitiza elimu inayotolewa mashuleni inahitaji mabadiliko makubwa. It's very European. Elimu yetu inapaswa kuendana na mazingira yetu. In other words, what is taught in schools should enable students relate to their environments. That's the only way education will contribute to the emancipation of our people from poverty. We must decolonize our knowledge before we can even talk of independence. Fikra za wataalamu wetu wengi sasa hivi hazielekezwi kwenye kuyaelewa matatizo yetu bali kwenye kufanya maisha yetu kufanana na yale ya wenzetu wa Ulaya, America, na baadhi ya nchi za Asia (In other words, our educated people (call them civilized people) are busy trying to apply imported solutions rather than focus on understanding problems for 90% of solutions lie in the correct definition of problems. Problems are never similar. European problems cannot be similar to African problems for many reasons. So, it's insane to have an education system focused on learning or cramming, to be specific, European solutions that were introduced to us through colonialism). This is not an easy argument to understand because you have been conditioned not to understand it. I mean, I am talking about epistemic violence - the one which makes it natural to discriminate against your own people in the name of development.

PS. You are invoking Malthusian argument. Read and you will see that the argument has been thoroughly debunked. If Malthus was right (this is to say, if you are right), the world could have perished long time ago.
 
Shida yetu kubwa ni kukataa kubadilika. Tunakabiliana vipi na kilichopo mbele yetu?

The traditional way of keeping livestock was made to correspond with the environment by then, population was small and most areas were free and available for grazing. It is obvious that with the increase in population there has also been an increase in the production of livestock demanding more grazing land. In early days livestock were kept mainly for pride and not symbol of wealthy. A lot more areas have been turned onto settlement areas, protected or reserved areas and farms. Quality of livestock was not an issue because livestock were not basically items for sale or product for trading. But with the changes in culture and business environment livestock are to be considered as units of wealthy and meant for business other than pride.

Since there is a shift in the value of livestock quantity and pride should no longer be the only motive for livestock keeping but quality as well. There are very limited lands available for grazing an ever growing numbers of livestock. The carrying capacity has been reduced tremendously as well, changes in the climatic condition, vegetation changes, overgrazing in many places and many other reasons has reduced the ability of land to produce quality pastures for livestock. It is now tradeoff between size of livestock herds and the available free land. While land size is static and we have limited ways to cause it to produce more there are millions of ways to reduce the size of the herds to fit the available free land. Protected areas do not only offer habitat for wildlife but are also important for ecosystem services which sustain all sorts of life on earth including the live of pastoralists and livestock itself. Number of livestock and herd size in Tanzania is alarming to the extent threatening ecosystems and biodiversity at large. For Tanzania to experience viable and sustainable economic development there has to be a way to clearly separate culture from economic production which requires economic principles.

Yes we cannot do everything the European way when we don’t resemble in any way, but that doesn’t necessarily mean that we must continue to do things Tanzanian way but against economic principles. It doesn't matter who wrote what the question is is it working? are we solving our problems? Kama ndio tuendelee kama kawaida kama sio na hatutaki kubadilika hatutabaki salama.



Ufugaji wa kisasa ukoje? Kama wanavyofuga wazungu? Unataka Wasukuma, Wabarbaig, na Wamasai wafuge kama Wazungu? Unanikumbusha Waziri Mkuu Mizengo Pinda alienda Dubai akaona shamba la ng'ombe kule (ng'ombe wamewekewa mpaka air conditioner na shower kupooza miili yao), akarudi Tz na kusema lazima wataalamu wetu wakajifunze kule ili na sisi tufanye kama wao. This flawed thinking, halafu tunaimba ngonjera za maendeleo. Ndio maana nasisitiza elimu inayotolewa mashuleni inahitaji mabadiliko makubwa. It's very European. Elimu yetu inapaswa kuendana na mazingira yetu. In other words, what is taught in schools should enable students relate to their environments. That's the only way education will contribute to the emancipation of our people from poverty. We must decolonize our knowledge before we can even talk of independence. Fikra za wataalamu wetu wengi sasa hivi hazielekezwi kwenye kuyaelewa matatizo yetu bali kwenye kufanya maisha yetu kufanana na yale ya wenzetu wa Ulaya, America, na baadhi ya nchi za Asia (In other words, our educated people (call them civilized people) are busy trying to apply imported solutions rather than focus on understanding problems for 90% of solutions lie in the correct definition of problems. Problems are never similar. European problems cannot be similar to African problems for many reasons. So, it's insane to have an education system focused on learning or cramming, to be specific, European solutions that were introduced to us through colonialism). This is not an easy argument to understand because you have been conditioned not to understand it. I mean, I am talking about epistemic violence - the one which makes it natural to discriminate against your own people in the name of development.

PS. You are invoking Malthusian argument. Read and you will see that the argument has been thoroughly debunked. If Malthus was right (this is to say, if you are right), the world could have perished long time ago.
 
Huyu Kawawa si kafumushwa juzi bodi ya tumbaku?

Pia dada yake alipenyezwa kugombea ubunge Africa mashariki akapigwa chini, wenzetu sijui wana bahati gani yaani wanaonekana wao tu ,sisi kutwa tunaandamana kumpongeza rais lakini familia zilezile zisijoandamana kumpongeza ndo wanateuliwa hata wakishamaliza kazi flani wanahamishiwa kwingine.
 
Back
Top Bottom