Naibu waziri wa Viwanda na Biashara amewadhalilisha waandishi wa habari, kwa kuwahadaa wasafiri toka Singida Mjini hadi Ilongero, Kama Km 30 hivi tena katika barabara mbovu sababu ni tope na hakuna lami na sasa kuna mvua. Amewahadaa akaonane nao eti alikuwa na kikao cha kuzungumza na wadau wa elimu. Baada ya kubaini kuwa angeulizwa maswali kuhusu kudanganya kuwa anasomesha watoto aliondoka kinyemela, waandishi wakashinda mchana kutwa baadaye wakaambiwa hayupo. Tangu kuchapishwa habari za yeye kudhalilisha watoto kwa kuwapeleka Arusha kwa kuwaonyesha wazungu, huku akiwa na Uraia wa nchi mbili anaingia kinyemelanyemela. Poleni waandishi wa Singida