Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 9,482
- 14,347
Serikali imetolea tamko tatizo la mgawo wa umeme nchini na kutaja hatua sita za dharura ilizochukua katika kukabiliana na tatizo hilo sugu.
Akizungumza bungeni jana, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alitaja utekelezaji wa miradi ya umeme katika kipindi kifupi na cha kati kuwa moja ya hatua hizo zilizochukuliwa kumaliza tatizo hilo.
Waziri Ngeleja alitoa tamko hilo baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda, kumtaka afanye hivyo ili kumaliza kiu ya wabunge wa upinzani walioitaka Serikali itolee kauli suala hilo ili wananchi wajue hatima yake.
Februari 11 mwaka huu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe katika swali la nyongeza, alimtaka Waziri Ngeleja kutolea kauli tatizo la umeme, lakini Spika Makinda aliizima hoja hiyo akisema haingekuwa rahisi kwa Waziri huyo kuzungumzia suala hilo muhimu katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo.
Na jana baada ya kupata fursa ya kuzungumzia tatizo hilo la mgawo wa umeme Ngeleja alisema Serikali kwa kushirikiana na Tanesco imechukua hatua sita tofauti.
Ataja hatua hizo za dharura kuwa ni pamoja na kuhakikisha fedha za kununulia mafuta ya kuendeshea kituo cha kuzalisha umeme cha IPTL zinaendelea kupatikana kwa wakati ili kizalishe kiwango cha Megawati 80 ambacho ni cha juu.
Pia kuharakisha mchakato wa kukodi mitambo ya dharura yenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya megawati 260 endapo mvua za kutosha hazitanyesha kuwezesha ongezeko la umeme
unaotokana na maji na kutekeleza mpango wa kupanua miundombinu ya kusafuisha na kusafirisha gesi asilia kutoka visima vya Songosongo hadi Dar es Salaam.
Nyingine ni kuhakikisha miradi ya kudumu ya kuzalisha umeme ya Megawati 100 itakayofungwa Ubungo, Dar es Salaam kwa kutumia gesi asilia na mitambo ya megawati 60 itakayofungwa Mwanza kutumia mafuta mazito inakamilishwa kama ilivyopangwa Desemba 2011 na Januari 2012.
Ngeleja alitaja hatua nyingine kuwa ni kuendelea kutekeleza miradi ya kupunguza upotevu wa umeme kutoka asilimia 21 ya sasa hadi asilimia 15 kati ya mwaka 2011 na 2015, pamoja na Tanesco kusimamia mgawo wa umeme kwa umakini zaidi na kuhakikisha upatikanaji wa umeme katika shughuli za uzalishaji, sehemu nyeti za huduma za jamii, ulinzi na usalama.
Alisema kuwa wizara yake kwa kushirikiana na Tanesco inaendelea kusimamia utekelezaji wa programu ya kuongeza uwezo wa kuzalisha umeme katika kipindi kifupi cha 2011 hadi 2015 ili kuepusha tatizo la mgawo wa umeme siku za usoni ambapo alitaja miradi tofauti saba
Akizungumza bungeni jana, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alitaja utekelezaji wa miradi ya umeme katika kipindi kifupi na cha kati kuwa moja ya hatua hizo zilizochukuliwa kumaliza tatizo hilo.
Waziri Ngeleja alitoa tamko hilo baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda, kumtaka afanye hivyo ili kumaliza kiu ya wabunge wa upinzani walioitaka Serikali itolee kauli suala hilo ili wananchi wajue hatima yake.
Februari 11 mwaka huu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe katika swali la nyongeza, alimtaka Waziri Ngeleja kutolea kauli tatizo la umeme, lakini Spika Makinda aliizima hoja hiyo akisema haingekuwa rahisi kwa Waziri huyo kuzungumzia suala hilo muhimu katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo.
Na jana baada ya kupata fursa ya kuzungumzia tatizo hilo la mgawo wa umeme Ngeleja alisema Serikali kwa kushirikiana na Tanesco imechukua hatua sita tofauti.
Ataja hatua hizo za dharura kuwa ni pamoja na kuhakikisha fedha za kununulia mafuta ya kuendeshea kituo cha kuzalisha umeme cha IPTL zinaendelea kupatikana kwa wakati ili kizalishe kiwango cha Megawati 80 ambacho ni cha juu.
Pia kuharakisha mchakato wa kukodi mitambo ya dharura yenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya megawati 260 endapo mvua za kutosha hazitanyesha kuwezesha ongezeko la umeme
unaotokana na maji na kutekeleza mpango wa kupanua miundombinu ya kusafuisha na kusafirisha gesi asilia kutoka visima vya Songosongo hadi Dar es Salaam.
Nyingine ni kuhakikisha miradi ya kudumu ya kuzalisha umeme ya Megawati 100 itakayofungwa Ubungo, Dar es Salaam kwa kutumia gesi asilia na mitambo ya megawati 60 itakayofungwa Mwanza kutumia mafuta mazito inakamilishwa kama ilivyopangwa Desemba 2011 na Januari 2012.
Ngeleja alitaja hatua nyingine kuwa ni kuendelea kutekeleza miradi ya kupunguza upotevu wa umeme kutoka asilimia 21 ya sasa hadi asilimia 15 kati ya mwaka 2011 na 2015, pamoja na Tanesco kusimamia mgawo wa umeme kwa umakini zaidi na kuhakikisha upatikanaji wa umeme katika shughuli za uzalishaji, sehemu nyeti za huduma za jamii, ulinzi na usalama.
Alisema kuwa wizara yake kwa kushirikiana na Tanesco inaendelea kusimamia utekelezaji wa programu ya kuongeza uwezo wa kuzalisha umeme katika kipindi kifupi cha 2011 hadi 2015 ili kuepusha tatizo la mgawo wa umeme siku za usoni ambapo alitaja miradi tofauti saba