Waziri Ndalichako: Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ni Himilivu. Agoma kupokea taarifa kuhusu ripoti ya CAG

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,444
7,808
Leo waziri wa nchi, ofisi ya waziri mkuu, Kazi, Ajira na wenye ulemavu akiwa Bungeni amekanusha mifuko ya hifadhi ya Jamii kutokuwa himilivu. Alipohojiwa na Esther Bulaya juu ya ripoti ya CAG kusema vinginevyo, ameendelea kushikilia msimamo wake kwa madai ripoti hiyo inaishia June 2021.

Waziri Ndalichako: Mheshimiwa mwenyekiti, jambo jingine ambalo wananchi wanalizungumzia ni uhimilivu wa mifuko, naomba nilihakikishie bunge lako tukufu kwamba mifuko hii bado ni himilivu, bado itaendelea kulipa mafao kwa wastaafu.

TAARIFA
Esther Bulaya:
Napenda nimpe taarifa mheshimiwa waziri, taarifa ya mkaguzi mkuu na mdhibiti wa Serikali amesema mifuko ina hali mbaya, sio himilivu na ipo kinyume na utaratibu wa ukwasi wa asilimia 40, mlipolipa trilioni 2 walau imefika asilimia 30.

PSSSF kwa miaka ya karibuni, mapato yake ya michango ni madogo kuliko mahitaji ya wazee wastaafu wanaotakiwa kulipwa, iko himilivu wapi?

Mwenyekiti: Mheshimiwa Profesa Ndalichako unapokea taarifa?

Prof. Ndalichako: Mimi siipokei hiyo taarifa kwasababu taarifa ya CAG ni ya mpaka Juni 2021.

Bulaya anaongea

Mwenyekiti: Nani amekuruhusu kuongea mheshimiwa Bulaya, hili ni Bunge.
 
Leo waziri wa nchi, ofisi ya waziri mkuu, Kazi, Ajira na wenye ulemavu akiwa Bungeni amekanusha mifuko ya hifadhi ya Jamii kutokuwa himilivu. Alipohojiwa na Esther Bulaya juu ya ripoti ya CAG kusema vinginevyo, ameendelea kushikilia msimamo wake kwa madai ripoti hiyo inaishia June 2021.

Waziri Ndalichako: Mheshimiwa mwenyekiti, jambo jingine ambalo wananchi wanalizungumzia ni uhimilivu wa mifuko, naomba nilihakikishie bunge lako tukufu kwamba mifuko hii bado ni himilivu, bado itaendelea kulipa mafao kwa wastaafu.

TAARIFA
Esther Bulaya:
Napenda nimpe taarifa mheshimiwa waziri, taarifa ya mkaguzi mkuu na mdhibiti wa Serikali amesema mifuko ina hali mbaya, sio himilivu na ipo kinyume na utaratibu wa ukwasi wa asilimia 40, mlipolipa trilioni 2 walau imefika asilimia 30.

PSSSF kwa miaka ya karibuni, mapato yake ya michango ni madogo kuliko mahitaji ya wazee wastaafu wanaotakiwa kulipwa, iko himilivu wapi?

Mwenyekiti: Mheshimiwa Profesa Ndalichako unapokea taarifa?

Prof. Ndalichako: Mimi siipokei hiyo taarifa kwasababu taarifa ya CAG ni ya mpaka Juni 2021.

Bulaya anaongea

Mwenyekiti: Nani amekuruhusu kuongea mheshimiwa Bulaya, hili ni Bunge.
Huyu bibi Ndalichako hadi wajukuu zake tumekuwa watu wazima ye bado ktk utumishi tu.Awachiye na wengine mweeh!
 
Waziri yupo sahihi kabisa ripoti hiyo ni ya zamani kuliko mazingira ya sasa. Hapa ndipo tunaona hilo kundi la BAWACHA bungeni
ni mzigo kwa taifa
 
Waziri yupo sahihi kabisa ripoti hiyo ni ya zamani kuliko mazingira ya sasa. Hapa ndipo tunaona hilo kundi la BAWACHA bungeni
ni mzigo kwa taifa
BAWACHA imeingiaje hapo mkuu...nikushauri jambo moja, Jenga tabia ya kujisikiliza kutoka moyoni kabla hujazungumza au kuandika kitu....you are too emotional!
 
Back
Top Bottom