Waziri Ndalichako, bado wanafunzi tunaibiwa Vyuoni, SUA na UDSM wamo

Zygot

JF-Expert Member
Apr 14, 2016
2,236
2,862
Bodi ya mikopo ya wanafunzi kwa kushirikiana na viongozi wa vyuo vikuu ilikuwa ikiiba pesa za wanafunzi hewa, walioacha masomo na hata waliofariki. Bahati mbaya hakuna hatua ya maana iliyochukuliwa.

Kuna mtindo mpya wa wizi. Vijana wetu wanapomaliza masomo na kufuatilia vyeti, huambiwa ulipokuwa mwaka wa kwanza hukulipa ada hii au gharama ile. Mtindo huu umekomaa vyuo vyote, binafsi nimeshawalipia vijana wawili Chuo Kikuu cha Kilimo, SUA na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, UDSM baada ya kudaiwa na ofisi ya uhasibu, ada za miaka mitatu iliyopita. Niliamini enzi hizi za kompyuta vyuo vinatunza kumbukumbu zake. Naiona hii ni makusudi. Kwa nini wadaiwe wote ada ya miaka mitatu iliyopita? Wengi wanalipishwa kwa mara ya pili kwa makusudi kabisa kwa madai kwamba chuo hakioni kumbukumbu.

Waziri wa Elimu bahati mbaya wewe umetokea chuoni. Yaonekana una urafiki binafsi na hawa maprofesa wenzako. Tunaomba uviangalie upya vyuo vikuu hivi. Siyo wasafi kama unavyoonesha. Bado wanaangaika kuwaibia wanafunzi na sisi wazazi tunaolipa ada hizo.
 
Kama vyuo havitunzi kumbukumbu naamini mwanafunzi au mzazi ana kumbukumbu. Ukiambiwa hujalipa, onyesha kumbukumbu zako to prove them wrong.
Kwanza hakuna chuo unachofanya UE bila kumaliza ada siku hizi. Hiyo registration tu mbinde. Ndio miaka mitatu iishe hujalipa kitu?

Kama analipiwa na bodi kuna kusign pesa zinapoingia. Kama anajilipia kuna receipts, bank slip n.k.n.k hakuna kitu kinaitwa Hela kutoonekana, Yaani system ipo clear sijui mtoa mada amekutanaje na tatizo hili?
 
Kwanza hakuna chuo unachofanya UE bila kumaliza ada siku hizi. Hiyo registration tu mbinde. Ndio miaka mitatu iishe hujalipa kitu?

Kama analipiwa na bodi kuna kusign pesa zinapoingia. Kama anajilipia kuna receipts, bank slip n.k.n.k hakuna kitu kinaitwa Hela kutoonekana, Yaani system ipo clear sijui mtoa mada amekutanaje na tatizo hili?
Au anaongelea kwa rasi simba!!!?
 
Kwanza hakuna chuo unachofanya UE bila kumaliza ada siku hizi. Hiyo registration tu mbinde. Ndio miaka mitatu iishe hujalipa kitu?

Kama analipiwa na bodi kuna kusign pesa zinapoingia. Kama anajilipia kuna receipts, bank slip n.k.n.k hakuna kitu kinaitwa Hela kutoonekana, Yaani system ipo clear sijui mtoa mada amekutanaje na tatizo hili?
Muda wa clearance wahasibu huwa wanahitaji risiti za malipo / registration forms za miaka yote uliyosoma wakijua kabisa lazima kuna waliopoteza hivi vitu na hapo ndipo balaa linapoanzia
 
Muda wa clearance wahasibu huwa wanahitaji risiti za malipo / registration forms za miaka yote uliyosoma wakijua kabisa lazima kuna waliopoteza hivi vitu na hapo ndipo balaa linapoanzia
Ni kweli mkuu, ila kila upande unawajibika kuwa na nakala ya malipo husika. Kama ulilipia benki kuna kumbukumbu zitakuwepo.Mlazimishe muhasibu akafuatilie benki.

Swali dogo umewezaje kumaliza miaka 3 bila kulipa hata senti (kama mtoa mada anavyodai?)

Narudia tena hakuna kitu kinaitwa Hela Haionekani kwenye system. Ningekuwa mtoa mada ningeenda hadi kwa VC hata kwa katibu mkuu wizarani, mbona wanapatikana simple tu siku hizi. Huyo muhasibu angejibu amemalizaje bila kulipa hata senti.

Siku hizi hamna Serekali za wanafunzi huko vyuoni? Enzi zetu Daruso ya Mtatiro na Bush hili sio tatizo kabisa.
 
Bodi ya mikopo ya wanafunzi kwa kushirikiana na viongozi wa vyuo vikuu ilikuwa ikiiba pesa za wanafunzi hewa, walioacha masomo na hata waliofariki. Bahati mbaya hakuna hatua ya maana iliyochukuliwa.

Kuna mtindo mpya wa wizi. Vijana wetu wanapomaliza masomo na kufuatilia vyeti, huambiwa ulipokuwa mwaka wa kwanza hukulipa ada hii au gharama ile. Mtindo huu umekomaa vyuo vyote, binafsi nimeshawalipia vijana wawili Chuo Kikuu cha Kilimo, SUA na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, UDSM baada ya kudaiwa na ofisi ya uhasibu, ada za miaka mitatu iliyopita. Niliamini enzi hizi za kompyuta vyuo vinatunza kumbukumbu zake. Naiona hii ni makusudi. Kwa nini wadaiwe wote ada ya miaka mitatu iliyopita? Wengi wanalipishwa kwa mara ya pili kwa makusudi kabisa kwa madai kwamba chuo hakioni kumbukumbu.

Waziri wa Elimu bahati mbaya wewe umetokea chuoni. Yaonekana una urafiki binafsi na hawa maprofesa wenzako. Tunaomba uviangalie upya vyuo vikuu hivi. Siyo wasafi kama unavyoonesha. Bado wanaangaika kuwaibia wanafunzi na sisi wazazi tunaolipa ada hizo.
Mkuu kabla ya kulipa ungeomba ushauri. Kumbukumbu hazionekani ndio lugha ya wapi? Malipo yote yanafanyika benki mngeenda kuomba.

Nenda kachukue hela zako aisee. Umelipa mara mbili.
 
Hata UDOM haka kamchezo kalikuwepo waliomaliza mwaka 2011 walikutana na huo mchezo na wengine walilazimika kulipa tena sijajua miaka ya mbele....
Dawa ni chuo kutoa receipts kwa kila mwanafunzi aliyelipiwa ADA na Bodi mara tu bodi wanapotuma pesa ya Ada chuoni badala ya kusign ile list ya majina....
Vinginevyo huu ujanjaujanja utaendelea tu..
 
Zygot, Kama vyuo havitunzi kumbukumbu naamini mwanafunzi au mzazi ana kumbukumbu. Ukiambiwa hujalipa, onyesha kumbukumbu zako to prove them wrong.
Chuo Kikuu kushindwa kutunza kumbukumbu ni makusudi. Wanafunzi wanahama mwaka mmoja hadi mwingine baada ya kutimiza masharti yote ikiwa ni pamoja na kulipa ada. Iweje mwanafunzi amalize mwaka wa 3, 4 au 5 ndo aulizwe ada ya mwaka wa kwanza?

Ni makusudi ili kutegeshea asiye na kumbukumbu, alipe mara ya pili, aibiwe.
 
Kwanza hakuna chuo unachofanya UE bila kumaliza ada siku hizi. Hiyo registration tu mbinde. Ndio miaka mitatu iishe hujalipa kitu?

Kama analipiwa na bodi kuna kusign pesa zinapoingia. Kama anajilipia kuna receipts, bank slip n.k.n.k hakuna kitu kinaitwa Hela kutoonekana, Yaani system ipo clear sijui mtoa mada amekutanaje na tatizo hili?
Nadhani mada inaonesha wizi wa makusudi. Hakuna suala la kutunza risiti au bank slip. Ziwepo zisiwepo wao wanawaachia wanafunzi waoneshe. Ktk maelefu lazima wanabahatisha wale ambao hazionekani na hapo ndo suala la ufisadi linaanzia.
 
Muda wa clearance wahasibu huwa wanahitaji risiti za malipo / registration forms za miaka yote uliyosoma wakijua kabisa lazima kuna waliopoteza hivi vitu na hapo ndipo balaa linapoanzia
Nadhani ni kundi la wizi linalojaribu kutikisa wanafunzi. Hakika ktk maelfu ya wanafunzi lazima wapo waliopoteza. HAta hivyo kwa kijana wa mwaka wa kwanza anapoanza chuo hatagemei kudiwa risiti miaka mitatu ijayo. Hawa ni wezi tu kama walivyozoea.
 
Bila shaka ni uzembe wa taasisi usika huwezi kumwambia mtu kuwa hajalipa karo wakati mwanafunzi anapolipa ada lazima apeleke peinislipu ya benki isitoshe vyuo kunakuwa na mfumo wa kutunza kumbukumbu mimi binafsi naona ni uzembe tu wa watendaji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
we unadhani wote ni kidato cha nne hapa?
Mkuu tutake radhi wenye dv 5, jf ni ya wote. Unaweza kuwa huna ni ambaya lakini hii comment yako itawaumiza zaidi walioshia drs la saba. Wengine hawakupenda kuishia hapo ila maisha na aina ya walimu huenda vikachangia. Tujaribu kuwa tunacomment bila kuonesha hata chembe za ubaguzi hata kqma kwetu hatuoni tatizo.
 
Huo mchezo ni common sanaa, hapo wapigaji ni muhasibu, dean wa fedha na Dvc hao ndio wanaelewa mchezo mzima.

Am not sure kama mbaka sasa kwa mfumo huu wa control number kama bado wanapiga.
 
Mkuu tutake radhi wenye dv 5, jf ni ya wote. Unaweza kuwa huna ni ambaya lakini hii comment yako itawaumiza zaidi walioshia drs la saba. Wengine hawakupenda kuishia hapo ila maisha na aina ya walimu huenda vikachangia. Tujaribu kuwa tunacomment bila kuonesha hata chembe za ubaguzi hata kqma kwetu hatuoni tatizo.
Siyo matusi. Angalia JF ina forums ngapi? Kila mtu anachangia anapoweza. Usipoelewa cha kuchangia ndo mwanzo wa mabishano yasiyo na mwisho, hakuna kuelewana. Kama hujawahi shuhudia kinachotokea kwenye mifumo ya chuo kikuu, kwa nini uchangia mjadala wa aina hiyo?

Ndo maana mimi sichangii mjadala wa uchawi na mambo ya waganga wa kienyeji.
 
Siyo matusi. Angalia JF ina forums ngapi? Kila mtu anachangia anapoweza. Usipoelewa cha kuchangia ndo mwanzo wa mabishano yasiyo na mwisho, hakuna kuelewana. Kama hujawahi shuhudia kinachotokea kwenye mifumo ya chuo kikuu, kwa nini uchangia mjadala wa aina hiyo?

Ndo maana mimi sichangii mjadala wa uchawi na mambo ya waganga wa kienyeji.
Nikuulize tu kidogo. Unauhakika kuwa wote wanaochangia pumba ni wale ambao hawakufika chuo kikuu?

Mimi na div 5 yangu tukikutana na lipumba wa sasa naweza kumtoa knock out kwenye mambo ya msingi, sanasana atanizidi maswali ya hesabu pekee. Kuna watu wana phd lakini akili zao wanazijua wenyewe. Elimu sio kigezo cha kuwa na iq kubwa.
 
Nikuulize tu kidogo. Unauhakika kuwa wote wanaochangia pumba ni wale ambao hawakufika chuo kikuu?

Mimi na div 5 yangu tukikutana na lipumba wa sasa naweza kumtoa knock out kwenye mambo ya msingi, sanasana atanizidi maswali ya hesabu pekee. Kuna watu wana phd lakini akili zao wanazijua wenyewe. Elimu sio kigezo cha kuwa na iq kubwa.
Usione ajabu kumzidi Lipumba au mimi mwenyewe kwa hayo uliyoyaita ya msingi. Kuna mambo hayahitaji kukaa darasani. Ni sawa na mnyama ngiri kuweza kukimbia kuliko binadamu, siyo kwa sababu amesoma sana juu ya riadha au kambi ya olympic, ni maumbile!
 
Usione ajabu kumzidi Lipumba au mimi mwenyewe kwa hayo uliyoyaita ya msingi. Kuna mambo hayahitaji kukaa darasani. Ni sawa na mnyama ngiri kuweza kukimbia kuliko binadamu, siyo kwa sababu amesoma sana juu ya riadha au kambi ya olympic, ni maumbile!
Hatushindani kiongozi, nilitaka kutoa mtazamo wangu juu ya kauli yako ya "kidato cha nne"
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom