Waziri Ndalichako amuondoa kazini Mkurugenzi VETA Nyanda za Juu Kusini

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amebaini mapungufu katika ujenzi wa chuo cha ufundi stadi (Veta) mkoa wa Rukwa na kuagiza kuondolewa katika nafasi yake mkurugenzi wa Veta Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Justine Rutta kutokana kwa madai ya kushindwa kusimamia ipasavyo ujenzi huo.

Pia amemwaagiza katibu mkuu wa wizara hiyo kuunda kamati ya kuchunguza mapungufu yaliyojitokeza katika mchakato mzima wa ujenzi wa chuo hicho, ikiwamo kuangalia kama thamani ya kazi liyofanyika inalingana na fedha ambazo Serikali imetoa hadi sasa.

Waziri huyo amechukua hatua hiyo kutokana na licha mkandarasi kulipwa zaidi ya Sh 2.1 bilioni na Serikali hadi sasa, lakini ujenzi wa mradi huo utakaonufaisha zaidi ya vijana 2,000 kusuasua.

Profesa Ndalichako alitoa maagizo ya kuondolewa mkurugenzi huyo baada ya kukagua ujenzi wa chuo hicho akiwa katika ziara yake ya kikazi mjini Sumbawanga mkoa wa Rukwa.

Katika ukaguzi huo, alibaini kuna ukiukwaji mkubwa wa mkataba baina ya Serikali na mkandarasi wa ujenzi wa chuo hicho kampuni moja ya China, ambapo licha ya Serikali kulipa fedha zaidi ya asilimia 25 kazi ipo kwa kiwango cha aslimia 25 wakati ilitakiwa kuwa imefikia asilimia 61.

Pia waziri huyo alibaini kampuni hiyo kutokuwa na vitendea kazi vya kutosha na muhimu na kutumia kampuni nyingine kuajiri wafanyakazi kinyume cha mkataba.

Awali, Rutta alieleza kuwa: “Mkandarasi huyo amekuwa na changamoto ya ukosefu wa fedha kutokana na Serikali kuchelewa kumlipa hali iliyosababisha ujenzi kusimama kwa zaidi ya miezi miwili.”

Alisema mradi huo ulianza kutekelezwa Septemba mwaka jana na unatarajiwa kukamilika Septemba mwaka huu na una thamani ya Sh 10.6 bilioni.
 
Wakati wametenga bajeti ya Bilioni 40 kujenga vyuo vinne vya VETA, mimi nilikuwa wa kwanza kukosoa nakusema kuwa pesa hizo ni kidogo sana kujenga vyuo vinne na wataishia kujenga vitu vya hovyo. Niliishauri serikali badala ya kujenga vyuo vinne vya VETA wangejenga kwanza vyuo viwili kwa hizo bilioni arobaini then watafute tena bilioni arobaini wajenge vyuo vingine viwili.
Yale niliyoyazungumza naona sasa yanatimia. Wametenga pesa kiduchu na kuishia kuweka wakandarasi wa kuokoteza. Haya ni makosa makubwa sana ya kimkakati. Serikali inabidi ikae kikao kulitafakari hili.
 
Wakati wametenga bajeti ya Bilioni 40 kujenga vyuo vinne vya VETA, mimi nilikuwa wa kwanza kukosoa nakusema kuwa pesa hizo ni kidogo sana kujenga vyuo vinne na wataishia kujenga vitu vya hovyo. Niliishauri serikali badala ya kujenga vyuo vinne vya VETA wangejenga kwanza vyuo viwili kwa hizo bilioni arobaini then watafute tena bilioni arobaini wajenge vyuo vingine viwili.
Yale niliyoyazungumza naona sasa yanatimia. Wametenga pesa kiduchu na kuishia kuweka wakandarasi wa kuokoteza. Haya ni makosa makubwa sana ya kimkakati. Serikali inabidi ikae kikao kulitafakari hili.
Mkuu huyu waziri anamuonea Mkurugenzi walidanganywa na Mkurugenzi wa TBA zile hostel za UDSM kuwa zitajengwa kwa bilioni kumi wakati haikuwa hivyo ona sasa.
 
Progress 25% hela iliyolipwa 25% shida iko wapi?
Nimecheka sana mkuu prof sielewi analaum nini,alitegemea mkandarasi ajenge kwa asilimia 75? Wakati amelipwa 25% isitoshe awamu hii wakandarasi hawana uhakika na malipo kama watayapata kwa wakati.
 
Nimecheka sana mkuu prof sielewi analaum nini,alitegemea mkandarasi ajenge kwa asilimia 75? Wakati amelipwa 25% isitoshe awamu hii wakandarasi hawana uhakika na malipo kama watayapata kwa wakati.
Wakandarasi huwa wanaenda kukopa na kuendelea na ujenzi...sasa awamu hii watakopa benki gani wakati benki zinapumulia kwa nyuma... wamemtoa kafara tu huyo mzee
 
Nimecheka sana mkuu prof sielewi analaum nini,alitegemea mkandarasi ajenge kwa asilimia 75? Wakati amelipwa 25% isitoshe awamu hii wakandarasi hawana uhakika na malipo kama watayapata kwa wakati.
Anatafuta sifa za kwa jiwe
 
Back
Top Bottom