Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
Waziri wa Habari na Mawasiliano ya teknolojia ya Habari Nape Nnauye ni miongoni mwa waliofika uwanja wa Nyamagana kuungana na RC Mwanza, Injinia Robert Gabriel na Waombolezaji wengine kuaga miili ya Waandishi 6 waliofariki kwenye ajali jana.
Natoa siku saba kuanzia leo kwa waajiri wote, kama kuna mwanahabari aliyefariki dunia kwenye ajali hii uwe umemlipa na taarifa za malipo yake yafikishe kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza. Tambueni tu leseni zenu ziko kwangu.
Ni siku ngumu kidogo kwangu, ni shughuli yangu ya kwanza hadharani baada ya kuaminiwa kwenye dhamana hii, ni shughuli ngumu kwa sababu tumekuja kwenye jambo gumu ambalo ni pigo kwa tasnia yetu ya habari, kwa kanda ya Ziwa na nchi yetu
Tupitie ajali zote zilizohusisha wanahabari kwenye misafara, viongozi wangu wameniagiza tuwaombe wenzetu wa jeshi la polisi watuletee ripoti za ajali hizi tuone kwanini zinagusa wanahabari na tuchukue hatua ya kuwalinda
Pia soma > Simiyu: Watu 14 wafariki dunia kwenye ajali katika msafara wa Mkuu wa Mkoa Mwanza
Natoa siku saba kuanzia leo kwa waajiri wote, kama kuna mwanahabari aliyefariki dunia kwenye ajali hii uwe umemlipa na taarifa za malipo yake yafikishe kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza. Tambueni tu leseni zenu ziko kwangu.
Ni siku ngumu kidogo kwangu, ni shughuli yangu ya kwanza hadharani baada ya kuaminiwa kwenye dhamana hii, ni shughuli ngumu kwa sababu tumekuja kwenye jambo gumu ambalo ni pigo kwa tasnia yetu ya habari, kwa kanda ya Ziwa na nchi yetu
Tupitie ajali zote zilizohusisha wanahabari kwenye misafara, viongozi wangu wameniagiza tuwaombe wenzetu wa jeshi la polisi watuletee ripoti za ajali hizi tuone kwanini zinagusa wanahabari na tuchukue hatua ya kuwalinda
Pia soma > Simiyu: Watu 14 wafariki dunia kwenye ajali katika msafara wa Mkuu wa Mkoa Mwanza