Waziri Nape: Muswada wa Sheria ya Ulinzi wa Data Binafsi upo katika hatua za mwisho

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
617
1,799
1647266442412.png

Waziri wa Habari, Nape Nnauye, leo Jumatatu, amesema muswada wa Sheria ya Ulinzi Binafsi, uko katika hatua za mwisho “hii ni sheria muhimu sababu vinginevyo uwekezaji utakuwa mgumu. Sio kwa sababu kulikuwa na kurekodi rekodi watu, hapana lakini ni kwa sababu ya kutunza faragha.”

Nape ametoa kauli hiyo leo Jumatatu, tarehe 14 Machi 2022, jijini Dar es Salaam, akielezea mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Samia, iliyoingia madarakani Machi mwaka jana, kufuatia kifo cha Hayati John Magufuli.

Mbunge huyo wa Mtama kupitia CCM, amesema katika kipindi hicho mahusiano ya kimataifa na sekta zilizo chini ya wizara yake yameimarika.

“Serikali inaendeleza mashirikiano baina ya nchi, kikanda na kimataifa, kati ya sekta ya mawasiliano kupitia tume za pamoja za mashirikiano pamoja na jumuiya za mashirika ambayo Tanzania ni mwanachama. Wote tutakubaliana tunaposema ameifungua nchi,” amesema Nape.

Katika hatua nyingine, Nape amesema Serikali imetumia Sh. 93.5 bilioni, kwenye ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano, ikiwemo ujenzi wa minara 12 kwenye maeneo ya mipakani na kupeleka huduma za mawasiliano kwenye Hifadhi ya Burigi Chato, mkoani geita.

Pia, fedha hizo zimetumika kupeleka huduma hizo kwenye ofisi 10 za halmashauri za wilaya, ujenzi wa minara 42 kwenye visiwa vya Zanzibar, kuongeza uwezo wa minara 127 kutoka teknolojia ya 2G kwenda 3G na 4G.

Nape amesema, Serikali imetenga Sh. 170 bilioni, kwa ajili ya ujenzi wa mkongo wa taifa, wakati Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limetoa Sh. 3.7 bilioni kwa ajili ya kufikisha miundombinu ya mawasiliano katika mradi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere, mkoani Pwani.

PIA SOMA:
- Dkt. Ndugulile: Sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi inakuja
 
Waziri wa Habari, Nape Nnauye, leo Jumatatu, amesema muswada wa Sheria ya Ulinzi Binafsi, uko katika hatua za mwisho “hii ni sheria muhimu sababu vinginevyo uwekezaji utakuwa mgumu. Sio kwa sababu kulikuwa na kurekodi rekodi watu, hapana lakini ni kwa sababu ya kutunza faragha.”
Good
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Muswada wa Sheria ya Ulinzi Binafsi, uko katika hatua za mwisho akifafanua “hii ni Sheria muhimu sababu vinginevyo uwekezaji utakuwa mgumu. Sio kwasababu kulikuwa na kurekodi rekodi Watu, hapana lakini ni kwasababu ya kutunza Faragha.”

Haki hii ya Faragha ipo kwa mujibu wa Ibara ya 16 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wadau mbalimbali ikiwemo JamiiForums wamekuwa wakihamasisha kutungwa kwa Sheria ya kulinda na kuhifadhi Faragha
 
Nappe huenda ndio waziri bora kwa sasa, jamaa anafanya kazi kwa vitendo.
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Muswada wa Sheria ya Ulinzi Binafsi, uko katika hatua za mwisho akifafanua “hii ni Sheria muhimu sababu vinginevyo uwekezaji utakuwa mgumu. Sio kwasababu kulikuwa na kurekodi rekodi Watu, hapana lakini ni kwasababu ya kutunza Faragha.”

Haki hii ya Faragha ipo kwa mujibu wa Ibara ya 16 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wadau mbalimbali ikiwemo JamiiForums wamekuwa wakihamasisha kutungwa kwa Sheria ya kulinda na kuhifadhi Faragha

Serikali haifungwi na sheria zozote inapofika kitu kinaitwa usalama wa nchi
 
Serikali haifungwi na sheria zozote inapofika kitu kinaitwa usalama wa nchi
Sawa lakini sio kwenda kuchungulia emails za watu au kurekodi mazungumzo ya watu ovyo ovyo kwa sababu za kisiasa , lazima kuwe na sababu ya muhimu na vigezo lazima vitumike na kwa ruhusa maalum kisheria, sio mwenyekiti wa CCM au mkuu wa wilaya anaamua tuu na kurusha sababu ya usalama wa Taifa ili kuingilia data za watu, tujitambue
 
Back
Top Bottom