Waziri Mwinyi alimsadia Matiko Matare(daruso leader) kukwepa kwenda JKT

Mwikimbi

JF-Expert Member
Mar 8, 2008
1,762
825
WAKUU HUU NI UKWELI NA CHANZO NI MIMI MWENYEWE, UKIPENDA PIA WAULIZE JAMES MBATIA, MOSENA NYAMBABE NA WENGINE WALIOKUWA VIONGOZI DARUSO NA ARISO 1989-1992

Mwaka 1991 katika hali ya kushangaza tulipata habari kuwa Rais wa daruso wakati huo Matiko matare amekamatwa na serikali na kuwa alikuwa apelekwe kwenye kambi moja ya JKT, kwa kuwa alijiunga na chuo kikuu bila kupitia JKT kwa mujibu wa sheria. kilichomponza matiko matare ni kuwa yeye alikuwa amejiuinga kwa masomo ya diploma ya ualimu chuo cha ualimu korogwe , kulikuwa na program ya miaka mitatu, miaka 2 ya kwanza unasoma masomo ya sekondari na mmoja uliobaki unasomea ualimu. Matiko aliamua kuacha baada ya miaka miwili ya kwanza na kuamua kujiunga na UDSM

kilichotokea asubuhi siku iliyofuata, Tuliunda kamati na kuamua kwenda kwa aliyekuwa waziri wa elimu sasa marehemu Jakson Makweta. nakumbuka alikuwa anakaa maeneo ambayo kwa sasa nimekuja kujua ndo osterbay, nyuma ya kanisa kuu la St Peter. tulikaribishwa vema uJumbe wetu na tukamweleza waziri kuwa tumekuja kumpongea waziri kwa kumkamata Matiko Matare ili aende jeshini kwa mujibu wa sheria. nakumbuka pia mheshimiwa Mbatia alikuwa sehemu ya ujumbe ule.

waziri alifurahi sana na akatukaribisha chai, na kushukuru kwa jinsi upeo wetu ulivyokuwa juu(mkumbuke kuwa Matiko alikuwa ni mwiba kwa serikali hasa kwa waziri mkuu wa wakati huo matiko Joseph Warioba0. hili nitakuja kuandika makala baadaye yaani mchango wa Matiko Matare katika siasa za mabadiliko katika nchi hii. furaha ya waziri Makweta kwa kuunga mkono kwetu kwa matiko kupelekwa JKT kwa nguvu haikudumu sana, kwani muda mfupi na hasa baada ya kunywa chai ya waziri ilikuja mada ya pili, ni lini Matiko ma angeplekwa JKT? bila shaka waziri akajibu haraka haraka kuwa hata leo leo mkitaka, ndipo lilipofuata swali au ushauri wa marehemu idrisaa kuwa , mheshimiwa waziri umejibu vema na sawa, ila itakuwa vema Matiko Matare akamsubiri Husein Ali Hassan Mwinyi mwananfunzi aliyekuwa anasoma Chuo kikuu cha Uturuki ili wote waende JKT kwa kuwa huyu naye alikuwa amechenga kwenda jeshini kwa mijibu wa sheria. Husein ndo huyu waziri wa ulinzi n JKT na mtoto wa rais Mwinyi ambaye aliamua kwa makusudi kumkwepesha mwanaye kwenda JKT kwa mujibu wa sheria na leo anateuliwa kuwa waziri kusismamia kile alichokwepa na kukikana.

kuna madudu mengi, lakini ndo maana tunasema kila siku kuwa wanaohubiri uzalendo ni wale walioshindwa kuutumikia, anaweza kusimamia JKT aliyoikana mwenyewe na kutorokea uturuki?! tunajua zaidi kuwa hakuwa na passes za kutosha kusoma UDSM kwa kuwa hakufanya vizuri katika masomo yake ya PCB hili atalijibu mwenyewe.
 
Ngoja waje wenye nchi yao bwana.....Utasikia maneno yao " Unamtukana rais wa awamu ya pili na muasisi wa familia ya kina hussen mwinyi kupitia mtoto wake"
 
Katika habari hii hapo juu sikumailizia, baada ya makweta kuobwa husein hassan mwinyi arudishwe toka uturuki ili aende na matare jkt, tuliambiwa turudi chuoni na kuwa angefuatilia, tulirudi chuoni tukakuta matare ameachiwa naikawa ndo mwisho wa matare na mwinyi kwenda jkt kwa mujibu wa sheria
 
Nina wasiwasi wewe ni mzushi au una lako jambo. Kwa kumbukumbu zangu wakati ule ulikuwa ukikamatwa kwa kuwepa kwenda JKT, basi ulikuwa unapelekwa moja kwa moja kwenye kambi mojawapo ya JKT. Hebu tufafanulie Matiko alipokamatwa alipelekwa kambi gani ya jeshi? Na kama kweli alipelekwa huko ilikuwaje akarudi masomoni? Ni wakati gani katika hiyo process uamuzi ulifanyika kwamba aachiwe arudi masomoni ili amsubiri Hussein Mwinyi aje ndio waende pamoja. Na kulikuwa na uhusiano gani kati ya Matiko na Hussein Mwinyi ambao ulikuwa ni kikwazo cha mmoja kutokwenda kutumikia JKT mpaka mwingine awepo pia?

Mleta mada naomba majibu.

Tiba
 
Katika habari hii hapo juu sikumailizia, baada ya makweta kuobwa husein hassan mwinyi arudishwe toka uturuki ili aende na matare jkt, tuliambiwa turudi chuoni na kuwa angefuatilia, tulirudi chuoni tukakuta matare ameachiwa naikawa ndo mwisho wa matare na mwinyi kwenda jkt kwa mujibu wa sheria

Yaani sielewi ni kwa nini mtu arudishwe kutoka masomoni eti tu kwa kuwa alitakiwa kwenda JKT. Kwa nini hakusubiriwa arudi ili akamatwe na kupelekwa huko JKT? Nini ulikuwa msingi wa ombi lenu la kutaka Matiko na Hussein kwenda JKT kwa wakati mmoja?

Tiba
 
nina wasiwasi wewe ni mzushi au una lako jambo. Kwa kumbukumbu zangu wakati ule ulikuwa ukikamatwa kwa kuwepa kwenda jkt, basi ulikuwa unapelekwa moja kwa moja kwenye kambi mojawapo ya jkt. Hebu tufafanulie matiko alipokamatwa alipelekwa kambi gani ya jeshi? Na kama kweli alipelekwa huko ilikuwaje akarudi masomoni? Ni wakati gani katika hiyo process uamuzi ulifanyika kwamba aachiwe arudi masomoni ili amsubiri hussein mwinyi aje ndio waende pamoja. Na kulikuwa na uhusiano gani kati ya matiko na hussein mwinyi ambao ulikuwa ni kikwazo cha mmoja kutokwenda kutumikia jkt mpaka mwingine awepo pia?

Mleta mada naomba majibu.

Tiba

unaweza kuwatafuta niliowataja kwenye mada akina mbatia watakupa maelezo ya uhakika, ni ukweli mtupu lakini kwa kuwa nyie ni watu wa kununulika huwezi kuamini, la maana nimewasilisha hapa tena baada ya kusoma uzi mwingine kwenye jukwaa hili kuhusu waziri huyu kukwepa jkt, nimetoa mchango wangu ni juu yako kuendeleaa kutetea uovu
 
Katika habari hii hapo juu sikumailizia, baada ya makweta kuobwa husein hassan mwinyi arudishwe toka uturuki ili aende na matare jkt, tuliambiwa turudi chuoni na kuwa angefuatilia, tulirudi chuoni tukakuta matare ameachiwa naikawa ndo mwisho wa matare na mwinyi kwenda jkt kwa mujibu wa sheria

Katika habari yako umedhihirisha kuwa binadamu ni selfish by nature. Kama sheria ya nchi ilimtaka kila muhitimu wa high school au college kwenda jeshini, mbona mliishia hapo? Huoni na wewe umejiweka kwenye kundi la wasio wazalendo?
 
1987 -1990 vuguvugu la mageuzi katika vyuo vyetu vikuu lilikuwa juu kuliko sasa, kulikuwa na agenda ya kuchangia elimu(cost sharing), ujio wa vyama vingi , na kuuawa kwa azmio la arusha na akina mwinyi kule zenj.

Matiko matare(udsm), huesin kimaro(muhimbili), na pale ardhi university(institute) kwa wakati huo walikuwepo akina mshana, komu, george, mwakajilege ambaowalisimama kidete sana kuhusu hili, wengi wa hawa walifukuzwa vyuo,kwa visingizio mbalimbali, hivyo serikali ilitumia kisingizio cha matiko kutokwenda jkt ili afukuzwe chuo kunyamazisha mageuzi.
 
unaweza kuwatafuta niliowataja kwenye mada akina mbatia watakupa maelezo ya uhakika, ni ukweli mtupu lakini kwa kuwa nyie ni watu wa kununulika huwezi kuamini, la maana nimewasilisha hapa tena baada ya kusoma uzi mwingine kwenye jukwaa hili kuhusu waziri huyu kukwepa jkt, nimetoa mchango wangu ni juu yako kuendeleaa kutetea uovu

Mkuu Mwikimbi, nia yangu sio kutetea uovu hata kidogo. Ingekuwa vizuri kama ungetupatia majibu ya maswali uliyoyauliza kuliko kunisukuma kwenda kuwauliza kina Mbatia otherwise haukuwa na sababu ya kuuleta huu uzi hapa. Ningependa ujibu maswali yangu kwanza halafu tuendelee na huu mjadala. Nafikiri umeileta hii mada hapa ili ijadiliwe sio?

Tiba
 
1987 -1990 vuguvugu la mageuzi katika vyuo vyetu vikuu lilikuwa juu kuliko sasa, kulikuwa na agenda ya kuchangia elimu(cost sharing), ujio wa vyama vingi , na kuuawa kwa azmio la arusha na akina mwinyi kule zenj.

Matiko matare(udsm), huesin kimaro(muhimbili), na pale ardhi university(institute) kwa wakati huo walikuwepo akina mshana, komu, george, mwakajilege ambaowalisimama kidete sana kuhusu hili, wengi wa hawa walifukuzwa vyuo,kwa visingizio mbalimbali, hivyo serikali ilitumia kisingizio cha matiko kutokwenda jkt ili afukuzwe chuo kunyamazisha mageuzi.

Kama kumbukumbu zangu ni sahihi Matiko aliondolewa chuoni baada ya serikali kumuondolea "Bursary" na yeye hakuweza kujigharimia mwenyewe kuendelea na masomo. Hakuondoka Mlimani kwa kuwa serikali ilitumia kutokwenda kwake JKT kumfukuza chuo. Kwa taratibu za chuo angeweza kuahirisha masomo kwa mwaka mmoja akaenda JKT na akarudi kuendelea na masomo baada ya kumalizana na JKT. Suala la kutokwenda JKT haikuwa sababu ya Matiko kuondolewa chuo kikuu.

Tiba
 
1987 -1990 vuguvugu la mageuzi katika vyuo vyetu vikuu lilikuwa juu kuliko sasa, kulikuwa na agenda ya kuchangia elimu(cost sharing), ujio wa vyama vingi , na kuuawa kwa azmio la arusha na akina mwinyi kule zenj.

Matiko matare(udsm), huesin kimaro(muhimbili), na pale ardhi university(institute) kwa wakati huo walikuwepo akina mshana, komu, george, mwakajilege ambaowalisimama kidete sana kuhusu hili, wengi wa hawa walifukuzwa vyuo,kwa visingizio mbalimbali, hivyo serikali ilitumia kisingizio cha matiko kutokwenda jkt ili afukuzwe chuo kunyamazisha mageuzi.

Hivi kweli kuna mtu anaeweza kubisha hata ushuhuda anaoutoa mtu aliyekuwepo kwenye tukio? Ni vema kujua kuwa vuguvugu la vyama vingi bila liliwaghalimu watu wengi sana ingawa sio vizuri kuwataja watu kama akina Hussein Kimaro, Mbatia, Komu pamoja na Kitwana Kondo!!! Matiko kwa ushujaa wake hakuogopa kuibana serikali kiasi kwamba they almost killed him.
 
Kama kumbukumbu zangu ni sahihi Matiko aliondolewa chuoni baada ya serikali kumuondolea "Bursary" na yeye hakuweza kujigharimia mwenyewe kuendelea na masomo. Hakuondoka Mlimani kwa kuwa serikali ilitumia kutokwenda kwake JKT kumfukuza chuo. Kwa taratibu za chuo angeweza kuahirisha masomo kwa mwaka mmoja akaenda JKT na akarudi kuendelea na masomo baada ya kumalizana na JKT. Suala la kutokwenda JKT haikuwa sababu ya Matiko kuondolewa chuo kikuu.
Tiba

Mlete thread ana half information na wewe Tiba hakuna unachofahamu/kumbuka. Mimi nilikuwepo enzi hizo za Matare akiwa RAIS wa DARUSO. Ningekuwa na mda ningeandika kwa kirefu mkasa mzima
Kwanza mojawapo ya madai yetu ilikuwa ni kwanini Dr.Hussein Mwinyi hakwenda JKT kwa MUJIBU wa SHERIA na badala yake baba yake Rais Mwinyi akamukimbizia Uturuki kusoma MD.
Pili Mantare Matiko alifukuzwa UDSM kwasababu ya mgomo wa1990 uliokuja kuitwa "matusi ya nguoni".
Tatu wakati tunarudishwa chuoni 1991, akina Mantare na Mbatia hawakurudi, serikali iliwafukuza kwa kile kilichondaiwa ndio walikuwa viongozi wa mgomo.
Aidha wakati tunarudishwa chuo ,UDSM haikuwa tena chini yaWizara ya Elimu. Mwinyi kwa mara ya kwanza aliunda Wizara ya Elimu ya juu ambayo Waziri wake wa kwanza alikuwa Benjamin Mkapa na PS wake Dr Gharib Bilal. Huo ndio ulikuwa mwanzo wa Dr. Bilal kuingia siasa kwani Mwinyi alimtoa direct UDSM.
Hakuna ujumbe wowote uliokwenda kumuona Makwete, kwasababu UDSM haikuwa tena chini ya Makwete (Wizara ya Elimu)
 
ni kumbukumbuku nzuri ya harakati za daruso wakati huo,ila ina chengachenga,hivi mwanaharakati mwingine bazigiza yuko wapi sasa?
 
Mlete thread ana half information na wewe Tiba hakuna unachofahamu/kumbuka. Mimi nilikuwepo enzi hizo za Matare akiwa RAIS wa DARUSO. Ningekuwa na mda ningeandika kwa kirefu mkasa mzima
Kwanza mojawapo ya madai yetu ilikuwa ni kwanini Dr.Hussein Mwinyi hakwenda JKT kwa MUJIBU wa SHERIA na badala yake baba yake Rais Mwinyi akamukimbizia Uturuki kusoma MD.
Pili Mantare Matiko alifukuzwa UDSM kwasababu ya mgomo wa1990 uliokuja kuitwa "matusi ya nguoni".
Tatu wakati tunarudishwa chuoni 1991, akina Mantare na Mbatia hawakurudi, serikali iliwafukuza kwa kile kilichondaiwa ndio walikuwa viongozi wa mgomo.
Aidha wakati tunarudishwa chuo ,UDSM haikuwa tena chini yaWizara ya Elimu. Mwinyi kwa mara ya kwanza aliunda Wizara ya Elimu ya juu ambayo Waziri wake wa kwanza alikuwa Benjamin Mkapa na PS wake Dr Gharib Bilal. Huo ndio ulikuwa mwanzo wa Dr. Bilal kuingia siasa kwani Mwinyi alimtoa direct UDSM.
Hakuna ujumbe wowote uliokwenda kumuona Makwete, kwasababu UDSM haikuwa tena chini ya Makwete (Wizara ya Elimu)
kudos!
 
Hilo linawezekana, ni kweli pia watoto wa wakubwa wengi walikwepa kwenda JKT kwa kutumia nafasi za wazazi wao. Tena wengine waliletewa vyeti nyumbani na tuliweza kujiunga nao vyuo vikuu bila kikwazo. Wengine walipelekwa makambi ya mjini kama Mlalakuwa ama Mgulani ambapo palikuwa hakuna karinyekarinye zozote wala mafunzo ya kijeshi na matumizi ya silaha (Kwata 1 - 102). Ukitafuta orodha yao ni wengiingawa wengine wanavyeti ila hawajawahi kukanyaga kwenye kambi za jeshi kwa mafunzo.
 
Back
Top Bottom