chakii
JF-Expert Member
- Sep 15, 2013
- 19,666
- 22,674
Habari wakuu,..
Huu ni muendelezo wa kauli tata za viongozi wetu juu sintofahamu kubwa iliyopo kati ya Serikali na kiwanda cha mfanyabiashara mkubwa Dangote.
Kauli hiyo ameisema Waziri mwenye dhamana ya viwanda, Bw Charles Mwijage.
Nimeshangaa kuona kiongozi kama huyu kukosa hata simple theory ya mambo ya uchumi, yaani suala la Demand/Supply/Price.
Ameshindwa kujua kiwanda cha Dangote kinachozalisha sementi kilifanya Suppy ya sementi uraiani kuwa kubwa, hali iliyopelekea Price au bei ya sementi hata kwa viwanda vingine kushuka kutokana na ushindani hivyo kupelekea watu wengi kumudu kununua sementi.
Badala yake ametujia na "NGONJERA" Ati kwamba sementi inapatikana tusijali, ameshindwa kutafakari kwamba baada ya Dangote kuondoka sokoni bei ya sementi iliyokuwa imeshuka itapanda na hata wananchi waliokuwa na matumaini ya kujenga watakwama.
Wananchi ndiyo tunaumia, tunaomba serikali imalize mvutano na huyu mfanyabiashara..
Chanzo : TBC Taifa.
Huu ni muendelezo wa kauli tata za viongozi wetu juu sintofahamu kubwa iliyopo kati ya Serikali na kiwanda cha mfanyabiashara mkubwa Dangote.
Kauli hiyo ameisema Waziri mwenye dhamana ya viwanda, Bw Charles Mwijage.
Nimeshangaa kuona kiongozi kama huyu kukosa hata simple theory ya mambo ya uchumi, yaani suala la Demand/Supply/Price.
Ameshindwa kujua kiwanda cha Dangote kinachozalisha sementi kilifanya Suppy ya sementi uraiani kuwa kubwa, hali iliyopelekea Price au bei ya sementi hata kwa viwanda vingine kushuka kutokana na ushindani hivyo kupelekea watu wengi kumudu kununua sementi.
Badala yake ametujia na "NGONJERA" Ati kwamba sementi inapatikana tusijali, ameshindwa kutafakari kwamba baada ya Dangote kuondoka sokoni bei ya sementi iliyokuwa imeshuka itapanda na hata wananchi waliokuwa na matumaini ya kujenga watakwama.
Wananchi ndiyo tunaumia, tunaomba serikali imalize mvutano na huyu mfanyabiashara..
Chanzo : TBC Taifa.