Waziri Mwijage: Hatutaruhusu wawekezaji wa Mitumba kuanzia sasa hivi

Bekabundime

JF-Expert Member
Aug 6, 2014
2,016
1,732
mwijage+px.jpg

Kuna vitu najiuliza sana kama kweli serikali ipo kwa ajili ya wanyonge na masikini, nimemuona WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji wa nchini Tanzania Mhe. Charles Mwijage ITV, kwenye taarifa ya habari eti anasema hatutaruhusu uwekezaji wa biashara ya mitumba tena, kuanzia sasa hivi.

Ameongeza kwa kusema kuwa 2019 ndio mwisho wa kuonekana mitumba Tanzania

Dah nimejiuliza sana hivi huyu ni Mtanzania kweli? hivi anajua familia za walalahoi wakulima zinaponea wapi? hivi amefika mikoani akaona watoto wa masikini wanaishije na kinachowasitiri ni nini? hivi anajua nguo mpya ya dukani hata yuniform inawashinda masikini kuinunua na wananunua mashati meupe ya mitumba na kuyapunguza ili mtoto avae?

Tukiacha vijijini hapa mjini anajua vijana wangapi wamejiajiri katika Mitumba?

Anataka kutuambia atakapo izuia hii biashara ana mbadala gani, hivi hii Serikali imekuja kwa ajili ya maskini kweli mbona kama kila siku huyu masikini ndio anaezidi kukomolewa?

Jamani wadau nyie mnalionaje hili?
 
Sijaona baya hapo alilosema... Target ni Tanzania ya Viwanda ambavyo vitapatikana kwa kuanza kuacha mitumba ili wawekezaji wazidi kujitokeza... Safi Mh.Mwijage
 
Mitumba ni zaidi ya nguo kwa sababu asilimia kubwa ya bidhaa na machinery tunazotumia ni mitumba pia. Sekta ya nguo na viatu vya mitumba ni sekta ambayo imeajiri vijana wengi sana mpaka vijijini, natumai kama serikali imeamua kuzuia mitumba kuanzia 2019 basi itakua na mpango kabambe wa kuajiri hawa vijana katika sekta mpya.
 
Ndio vinakuja sasa milango iko wazi, Kwan we unajua Mwatex, Urafuki vilikua vya nchi gani!? Kama iliwezekana zamani, Kwan sasa tushindwe!?.. One of the strategy ni kuanza na mitumba imeogopesha sana wawekezaji... Na jambo zuri wametaarifiwa mapema... tune weeps kukubali mabadiliko ili nchi isonge Mkuu...

Sent from my SM-J100FN using JamiiForums mobile app
 
Ndio vinakuja sasa milango iko wazi, Kwan we unajua Mwatex, Urafuki vilikua vya nchi gani!? Kama iliwezekana zamani, Kwan sasa tushindwe!?.. One of the strategy ni kuanza na mitumba imeogopesha sana wawekezaji... Na jambo zuri wametaarifiwa mapema... tune weeps kukubali mabadiliko ili nchi isonge Mkuu...

Sent from my SM-J100FN using JamiiForums mobile app
Kwa hiyo wewe unavaa kanga sio,kama unavaa kanga na kitenge sawa
 
Sijaona baya hapo alilosema... Target ni Tanzania ya Viwanda ambavyo vitapatikana kwa kuanza kuacha mitumba ili wawekezaji wazidi kujitokeza... Safi Mh.Mwijage
Natumaini ifikapo 2019 mwezi wa December kutakuwa na viwanda vya kutosha kuzalisha nguo zitakazokidhi hitaji la wenye kipato cha chini. Kwa wengi wetu tunaoishi kwa kutegemea mitumba kwa sababu ya unafuu wake tutaumia sana kama hapatakuwa na mbadala wa mitumba. Nafikiri tutarudi kwenye enzi za kuweka viraka kwenye nguo na yawezekana viongozi wa nchi hii wataifurahia hali hiyo.

Pia yawezekana vijana wetu ambao wanapata riziki kwa kupitia biashara ya nguo za mitumba wataongozwa na kuwezeshwa kuwa wabunifu ili kufanya shughuli zingine; ikishindika kufanya zilizo halali watafanya zilizo haram halafu wananchi watachukua sheria mokononi na kusitisha uhai wao. Je, yawezekana uongozi wa serikali ya awamu hii kufurahia hilo? Hasha, serikali yenye nia njema itakuwa makini katika kutekeleza azma ya Tanzania ya viwanda.

2019 haiko mbali. Yetu macho!
 
Wachina wamenufaika sana na Watanzania, sasa hivi tunawakaribisha hapa. Jambo zuri kuna hadi Mall inaitwa China Plaza... hii inaonesha ni jinsi gani TZ ina fursa sana.. Viwanda vitakuja tu na inawezekana kwa Tanzania yetu, mitumba mwisho 2019

Sent from my SM-J100FN using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom