Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,763
- 4,313
Hayo yamesemwa leo Septemba mosi, 2021 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba katika mkutano wake na wanahabari akibainisha kuwa lengo ni kuangalia ustawi wa jamii.
“Tumeachia miamala zaidi ya milioni 29 kwa watu ambao wanatumiana kuanzia shilingi moja mpaka Sh999, watu wanaotumiana viwango vile tuliiachilia yote ile kwa sababu dira ya rais sio kukusanya hela tu anaangalia na ustawi wa jamii, amesema Nchemba.