Waziri Mwigulu Nchemba apiga marufuku safari za nje kwa wote waliotajwa kwenye sakata la mchanga

Beira Boy

JF-Expert Member
Aug 7, 2016
17,895
25,944
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba apiga marufuku safari za nje ya mipaka ya nchi kwa wote waliotajwa kwenye sakata la mchanga isipokuwa kwa kibali maalum kutoka Serikalini.

======

Hakuna uzalendo zaidi ya kulinda rasilimali za Taifa, Hakuna utetezi wa wanyonge zaidi ya kulinda rasilimali zao. Hongera sana Mh.Rais kwa uzalendo wa vitendo kwa Taifa letu.

Naelekeza wote waliotajwa kuhusika hakuna kutoka nje ya mipaka ya nchi yetu isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini. Vyombo vitekeleze maagizo ya Rais kwa utimamu.

Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi.
12/06/2017
 
50093213d2d322eb509b310173c8eac9.jpg
 
June 12, Rais Magufuli amekabidhiwa ripoti ya pili ya mchanga wa madini ambayo imebaini uwepo wa mikataba mibovu inayoitia hasara serikali, ambapo kamati imetoa mapendekezo 21 ikiwemo kuchukuliwa hatua kwa wote waliohusika na ubadhirifu huo.

Ripoti iliyonifikia muda huu kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amewazuia wote waliotajwa kwenye ripoti hiyo kutoka nje ya mipaka ya Tanzania hadi vyombo vya dola vitakapofanya kazi yake kwa mujibu wa agizo la Rais JPM.

Waziri Mwigulu amesema “Hakuna uzalendo zaidi ya kulinda rasilimali za Taifa, Hakuna utetezi wa wanyonge zaidi ya kulinda rasilimali zao. Hongera sana Mh. Rais kwa uzalendo wa vitendo kwa Taifa letu

Naelekeza wote waliotajwa kuhusika hakuna kutoka nje ya mipaka ya nchi yetu isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini. Vyombo vitekeleze maagizo ya Rais kwa utimamu. Waziri Mwigulu Nchemba
 
"Mwiguru" ana mamlaka gani ya kupiga marufuku safari za watu.
Mambo ya nje ndio wangenyanganya passport zao ndio ningewaelewa.

Haya tuambie mwiguru ndio nani.
Niko nakusanya data kamili tarifa kamili naleta mkuu usiogope
 
Atakuwa ametumwa kufanya hivyo kwa serikali hii sidhani kama waziri mwenye dhamana ya ulinzi anaweza speed ya 4g
 
"Mwiguru" ana mamlaka gani ya kupiga marufuku safari za watu.
Mambo ya nje ndio wangenyanganya passport zao ndio ningewaelewa.

Haya tuambie mwiguru ndio nani.
Hujui kama passport zinatolewa wizara ya mambo ya ndani idara ya uhamiaji ambayo mwigulu nchemba ndo waziri wake? Sasa mambo ya nje inahusikaje tuhabarishe,, yani nyie bana ni kupinga kila kituuu mnatia aibu
 
Kwa hiyo kama anau wezo wakupiga marufuku basi atakaye taka kwenda nje amuombe kibali
 
Wazir wa mambo ya dan ya nchi mheshimiwa mwigulu nchemba amempongeza muheshimiwa rais kwa kaz nzur anazofanya na jitihada kubwa za kupambana na wahujumu uchumi

Vilevile amepiga marufuku kutoka nje ya mipaka na safali za nje kwa wote waliohusika na kutajwa kwenye sakata la mchanga
 
Back
Top Bottom