Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,316
Habari za asubuhi members wa JF.
Kuna siku Jumamosi ile ya wiki iliyopita nikiwa ninafunga ubuyu kwenye mfuko na kuchomea na kibatari kwa ajili ya kwenda kuuza kwa wanafunzi pale shule ya Rutihinda nikasikia wimbo unaimbwa eti 'Tupo Bongo Bahati Mbaya' nikawauliza wadogo zangu niliokuwa nao karibu wakasema eti Kuna msanii anajiita Young Dar es Salaam (Young Dee) ndio ameimba tupo bongo bahati mbaya.
Na sasa kila kijana mpaka madereva wa boda boda wanaimba eti wapo hapa bongo bahati mbaya.
Waziri wa Habari, Vijana na Utamaduni, Mzee Mwakyembe pamoja na BASATA wanajua nyimbo kama hizi zinaua that sense of patriotism kwenye akili za vijana taratibu taratibu.
Vijana wanaanza kuichukia nchi wangali wadogo sana. Wanapandikizwa mentality mbovu na serikali inaona lakini bado wapo kimya tu hakuna wanachofanya. Sijui hawajausikia huu wimbo ama wameamua kuupotezea tu.
Ninawasilisha mada. Mimi mropokaji tu wahusika fanyieni kazi hili.
Kuna siku Jumamosi ile ya wiki iliyopita nikiwa ninafunga ubuyu kwenye mfuko na kuchomea na kibatari kwa ajili ya kwenda kuuza kwa wanafunzi pale shule ya Rutihinda nikasikia wimbo unaimbwa eti 'Tupo Bongo Bahati Mbaya' nikawauliza wadogo zangu niliokuwa nao karibu wakasema eti Kuna msanii anajiita Young Dar es Salaam (Young Dee) ndio ameimba tupo bongo bahati mbaya.
Na sasa kila kijana mpaka madereva wa boda boda wanaimba eti wapo hapa bongo bahati mbaya.
Waziri wa Habari, Vijana na Utamaduni, Mzee Mwakyembe pamoja na BASATA wanajua nyimbo kama hizi zinaua that sense of patriotism kwenye akili za vijana taratibu taratibu.
Vijana wanaanza kuichukia nchi wangali wadogo sana. Wanapandikizwa mentality mbovu na serikali inaona lakini bado wapo kimya tu hakuna wanachofanya. Sijui hawajausikia huu wimbo ama wameamua kuupotezea tu.
Ninawasilisha mada. Mimi mropokaji tu wahusika fanyieni kazi hili.
Infantry Soldier,
Msanii anatumia uhuru wake wa kikatiba wa kujieleza.
Ibara ya 18 ya katiba inasema.
18.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
(2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.
Sasa huyo msanii kwa kutoa mawazo yake amevunja sheria gani?
https://www.bugando.ac.tz/attachments/Katiba_ya_Tanzania.pdf