CHA The GREAT
JF-Expert Member
- Nov 11, 2010
- 651
- 853
Kwamba, kumekuwa na tabia ya watu kurusha picha/video za wafu, au marehemu kwenye mitandao ya kijamii kama vile facebook n.k.. Kadhalika, picha za watu walioathirika na magonjwa kama vile cancer na mengineyo ya kutisha. Binafsi, huwa sipendezwi na tabia hii ya Watanznia wenzangu, ya kurusha picha za wafu. Picha au video hizo zinarushwa si kwa idhini ya marehemu au ndugu na jamaa za marehemu, bali kwa kiherehere cha watu ambao akili zao zinawaza kuwa kila picha, kila tukio ni sawa kuwekwa kwenye mitandao ya kijamii.
Mheshimiwa Waziri, huko Westminster, Uingereza, kulitokea ajali ya moto kwenye jengo la Grenfell, tarehe 14/6/2017, ambapo iliripotiwa vifo vya watu wapatao 70. Kama tabia ya Watanzania wengi wanaotumia mitandao ya kijamii ilivyo, Mtanzania mwenzetu anayeishi huko, alijikuta akipiga picha ya watu waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo na kuziweka kwenye mtandao wa kijamii wa facebook. Mtanzania huyo kwa majina ya Omega Mwaikambo (43), kutokana na kitendo chake hicho, alijikuta kwenye mkono wa sheria, ambapo alishitakiwa na kuhukumiwa miezi mitatu jela kwa kitendo chake hicho ambacho kwa kweli si cha kiungwana.
Mheshimiwa Waziri, natambua wewe ndiye mwenye dhamana ya wizara inayohusika na mambo ya habari ambapo mitandao ya kijamii ni sehemu yake. Sina hakika na sheria yetu inasemaje juu ya vitendo vya watu kurusha picha ambazo ni za udhalilishaji, au kurusha picha za watu bila idhini ya watu husika, sina hakika sheria inasemaje juu ya watu wanaorusha picha za watoto wadogo kabisa ambao kimsingi hawatoi idhini ya picha zao kurushwa, sina hakika, sina hakika. Na kwa kuwa sina hakika, naomba wizara yako iliangalie hili la baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii kurusha picha za wafu au watu walioathirika na magonjwa, mfano cancer na mengineyo ili wachukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa walio na tabia kama hiyo.
Nawasilisha.
JUSTICE FOR GRENFELL: Man who posted grim Facebook photos of dead victims JAILED
Mheshimiwa Waziri, huko Westminster, Uingereza, kulitokea ajali ya moto kwenye jengo la Grenfell, tarehe 14/6/2017, ambapo iliripotiwa vifo vya watu wapatao 70. Kama tabia ya Watanzania wengi wanaotumia mitandao ya kijamii ilivyo, Mtanzania mwenzetu anayeishi huko, alijikuta akipiga picha ya watu waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo na kuziweka kwenye mtandao wa kijamii wa facebook. Mtanzania huyo kwa majina ya Omega Mwaikambo (43), kutokana na kitendo chake hicho, alijikuta kwenye mkono wa sheria, ambapo alishitakiwa na kuhukumiwa miezi mitatu jela kwa kitendo chake hicho ambacho kwa kweli si cha kiungwana.
Mheshimiwa Waziri, natambua wewe ndiye mwenye dhamana ya wizara inayohusika na mambo ya habari ambapo mitandao ya kijamii ni sehemu yake. Sina hakika na sheria yetu inasemaje juu ya vitendo vya watu kurusha picha ambazo ni za udhalilishaji, au kurusha picha za watu bila idhini ya watu husika, sina hakika sheria inasemaje juu ya watu wanaorusha picha za watoto wadogo kabisa ambao kimsingi hawatoi idhini ya picha zao kurushwa, sina hakika, sina hakika. Na kwa kuwa sina hakika, naomba wizara yako iliangalie hili la baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii kurusha picha za wafu au watu walioathirika na magonjwa, mfano cancer na mengineyo ili wachukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa walio na tabia kama hiyo.
Nawasilisha.
JUSTICE FOR GRENFELL: Man who posted grim Facebook photos of dead victims JAILED