Kuna kiongozi wa CHADEMA amewahi kusema bungeni juu ya mwenendo wa kushughulikia mambo ya wizara ya uvuvi kwa operations. Pamoja na waziri Mpina kuitetea wizara yake, kumbukumbu yangu inaonesha hakuna operation ambayo imewahi kufanikiwa bila matatizo kwa wananchi, bahati mbaya wanaoendesha operation hizo huwa wanapewa kinga kwa uharifu wao hata kama ni nje ya kazi zao. Ilikuwa hivyo kwa Operation Tokomeza Sasa nimeishuhudia Operation Sangara ya bwana Mpina.
Nataka nizungumzie operation sangara ambayo imegeuka kuwa kichaka cha rushwa kwa kanda ya Ziwa. Kuna ufisadi bado unaendelea kwa jina la operation hiyo. Wilaya zote OCD na polisi wake, wakuu wa wilaya na maafisa uvuvi sasa wana mradi wa kudumu wa kuchukuwa rushwa.
Ninazo taarifa za ndani kutoka kwa afisa mwaminifu kwa ushuhuda wake kwa wilaya maarufu kwa uvuvi, Ukerewe. Bado nyavu aina ya makokoro zinatumika kinyume na Operation Sangara. Operation imekuwa ni mtaji kwa mkuu wa Wilaya, OCD na afisa uvuvi wa hamashauri. Polisi wanatumika hukusanya pesa toka kwa kila anayendesha uvuvi haramu na kuziwakilisha kwa OCD ambaye naye huwasiliana na mkuu wa wilaya. Polisi wamekuwa wakishinda barabarani kukusanya pesa kwa waendesha bodaboda wanaosafirisha samaki wadogo, wasioruhusiwa kuvuliwa.
Tatizo langu ni kwa viongozi wa serikali kama huyu mkuu wa wilaya ya Ukerewe na OCD. Inakuwaje aruhusu vitendo hivi haramu kuendelea badala ya kuzuia? Kibaya zaidi ukabila wa mkuu wa wilaya unatumika kujinasibu kwamba rais Magufuli ni ndugu yake. Ndiyo nini hiyo? Yaani mtu anakula rushwa kwa undugu na rais? Nadhani bado hatujapata watu wenye ubora wa kuwa wakuu wa wilaya.
Wakati haya yanatendeka, afisa usalama wa wilaya yupo. Je, anaripoti nini juu ya utendaji wa mkuu huyu wa wilaya? Je, ni mshirika ktk vitendo hivi? Matendo haya yote yanafanyika kwa kisingizio cha polisi wala rushwa, ukweli ni kwamba, polisi wameruhusiwa na wakuu wao kwa wilaya zote za kanda ya ziwa, Bunda, Musoma, Sengerema, Geita na ajabu hata Chato!
Nataka nizungumzie operation sangara ambayo imegeuka kuwa kichaka cha rushwa kwa kanda ya Ziwa. Kuna ufisadi bado unaendelea kwa jina la operation hiyo. Wilaya zote OCD na polisi wake, wakuu wa wilaya na maafisa uvuvi sasa wana mradi wa kudumu wa kuchukuwa rushwa.
Ninazo taarifa za ndani kutoka kwa afisa mwaminifu kwa ushuhuda wake kwa wilaya maarufu kwa uvuvi, Ukerewe. Bado nyavu aina ya makokoro zinatumika kinyume na Operation Sangara. Operation imekuwa ni mtaji kwa mkuu wa Wilaya, OCD na afisa uvuvi wa hamashauri. Polisi wanatumika hukusanya pesa toka kwa kila anayendesha uvuvi haramu na kuziwakilisha kwa OCD ambaye naye huwasiliana na mkuu wa wilaya. Polisi wamekuwa wakishinda barabarani kukusanya pesa kwa waendesha bodaboda wanaosafirisha samaki wadogo, wasioruhusiwa kuvuliwa.
Tatizo langu ni kwa viongozi wa serikali kama huyu mkuu wa wilaya ya Ukerewe na OCD. Inakuwaje aruhusu vitendo hivi haramu kuendelea badala ya kuzuia? Kibaya zaidi ukabila wa mkuu wa wilaya unatumika kujinasibu kwamba rais Magufuli ni ndugu yake. Ndiyo nini hiyo? Yaani mtu anakula rushwa kwa undugu na rais? Nadhani bado hatujapata watu wenye ubora wa kuwa wakuu wa wilaya.
Wakati haya yanatendeka, afisa usalama wa wilaya yupo. Je, anaripoti nini juu ya utendaji wa mkuu huyu wa wilaya? Je, ni mshirika ktk vitendo hivi? Matendo haya yote yanafanyika kwa kisingizio cha polisi wala rushwa, ukweli ni kwamba, polisi wameruhusiwa na wakuu wao kwa wilaya zote za kanda ya ziwa, Bunda, Musoma, Sengerema, Geita na ajabu hata Chato!