Waziri Mpango: Serikali ipo katika majadiliano ya IMF kuhusu ripoti ya Tanzania

Kwa ile report serikali ina hoja. Ukubwa wa hii habari umetokana na dhana ya serikali kuificha lakini content zake ni za kawaida maana ndio mijadala yetu ya kila siku.
 
Wataalam wa imf wamewasikiliza kina zzk na lissu badala ya kusikiluza wataalam wa serikali ndio maana kina lissu na zzk wanafurahia.

Wataalamu wa serikali wameacha weledi wamegeuka wapika data kwa kigezo cha uzalendo uchwara.
 
Kama kuna kitu nimejifunza kutokana na hii mijadala kuhusu ripoti za IMF na hata ile ya CAG, sisi watanzania ni wazuri sana kwenye kushabikia lakini wavivu/wagumu sana kwenye kutafuta taarifa sahihi. Kwa mfano:

1. Kuna baadhi ya watu wanashupalia kuwa IMF wanaandaa taarifa kuhusu hali ya uchumi wa nchi ilhali tuna wataalamu wetu ndani ya nchi ambao wanaweza kufanya hivyo. Je tunajua hata hizi taarifa zinatayarishwa vipi? Mbona hili liko wazi kwenye tovuti yao? https://www.imf.org/external/about/econsurv.htm

Sehemu ya taarifa hiyo:
Country surveillance
Country surveillance is an ongoing process that culminates in regular (usually annual) comprehensive consultations with individual member countries, with discussions in between as needed. The consultations are known as "Article IV consultations" because they are required by Article IV of the IMF's Articles of Agreement. During an Article IV consultation, an IMF team of economists visits a country to assess economic and financial developments and discuss the country's economic and financial policies with government and central bank officials. IMF staff missions also often meet with parliamentarians and representatives of business, labor unions, and civil society.

The team reports its findings to IMF management and then presents them for discussion to the Executive Board, which represents all of the IMF's member countries. A summary of the Board's views is subsequently transmitted to the country's government. In this way, the views of the global community and the lessons of international experience are brought to bear on national policies. Summaries of most discussions are released in Press Releases and are posted on the IMF's web site, as are most of the country reports prepared by the staff."

Huu ni utaratibu kwa kila nchi mwanachama wa IMF.

2. "Hakuna nchi mwananchama wa IMF, amepata maendeleo kwa kufuata ushauri wa IMF". Kweli inamaanisha nchi zote 189 ambazo ni wanachama wa IMF hakuna hata moja iliyoendelea kiuchumi? Ujerumani, Marekani, Uchina,nk. ni wanachama wa IMF na wao hawajaendelea?! Unadhani hizo taarifa wanazotoa ndio zinadidimiza/kukuza uchumi au zinaakisi uchumi uliodidimizwa/kukua?

3. "Wasitupangie uchumi wetu"

Kazi ya IMF siyokukupangia uchumi wa nchi ila kutathmini hali yake uchumi na kushauri kiutaalamu. Nchi inamaamuzi ya kufuata huo ushauri au la. Ila IMF inawajibu na mamlaka (kupitia mikataba iliyotiwa sahihi na nchi mwanachama) kutathmini na kutoa ripoti yake kwa utaratibu uliokubaliwa. Ikiwa walitoa ushauri nchi ifanye ABC ila nchi ikafanya EFG na bado uchumi ukaonyesha matokeo chanya kutokana vigezo vya tathmini, basi IMF hawawezi kupinga matokeo hayo. Hata wanavyovitathimni viko wazi kabisa kwenye tovuti yao

What does the IMF look at?
  1. Exchange rate, monetary, and fiscal policies.
  2. Financial sector issues assessment..which enables the IMF and the World Bank to gauge the strengths and weaknesses of countries' financial sectors.
  3. Assessment of risks and vulnerabilities stemming from large and sometimes volatile capital flows
  4. Institutional and structural issues: developing, implementing, and assessing internationally recognized standards and codes in areas crucial to the efficient functioning of a modern economy such as central bank independence, financial sector regulation, and policy transparency and accountability.
Hayo ni kwa uchache tu.

"Je inawezekana IMF wamekosea/wanapotosha? Iweje mwaka jana projection ilikuwa juu na mwaka huu ripoti inaonyesha projection imeshuka sana?": Maswali yanayolenga kufahamu zaidi kuhusu taarifa au ripoti hizi ni muhimu kuliko vijembe tunayorushiana. Tathmini ya kitaalamu hupingwa kwa tathmini ya kitaalamu, tena kwa uwazi wa hali ya juu.

Ila jamani kama ligi za kimataifa tunazishindwa basi ni bora kujiengua kulikoni kulialia hovyo kuwa tunaonewa kwasababu ni "watoto wa kambo tusiotaka mpira wetu uchezewe"
 
Wataalam wa imf wamewasikiliza kina zzk na lissu badala ya kusikiluza wataalam wa serikali ndio maana kina lissu na zzk wanafurahia.
1079439
 
Uzi huu sijawaona wale watu wa hovyohovyo kutoka Lumumba vipi kunani
Ripoti ya imf imeandikwa kwa lugha ya kiingereza. Ingekuwa ya kiswahili mbona wangeshakuwa wakati kama pilipili kichaa. Mimi namshukuru sana mwl nyerere kuruhusu English kuwa lugha mojawapo maofisini vinginevo wangetusumbua sana hawa lumumba.
 
Something must have gone wrong somewhere. Haiingii kichwani ndani ya miezi mitatu hesabu ziteremke kutoka wastani kwa mwaka wa 7% hadi 4% bila kuwa na tukio kubwa (janga) lililotokea, hususani vita au "a big natural disaster". Tetemeko la Kagera kamwe haliwezi kuwa sababu. So what had happened in that period to justify for that sharp decline of these statistics? Ndiyo maana wajumbe toka IMF wako hapa kwa majadiliano na maafisa wetu wa BoT.

Tukumbuke katika kipindi hiko kulitokea mabadiliko ya uongozi wa juu wa BoT baada ya Gavana wake, Prof Ndulu kustaafu kwa mjibu wa sheria. Inawezekana hand-over ilikuwa haijakamilika vizuri wakati maofisa wa IMF walipotutembelea. Tuwe na subira ukweli utajulikana baada ya tathmini mpya ndani ya siku 14 kama alivyoahidi Mh. Mpango.
Aisee tuta mengi
 
Waziri wa Fedha, Dkt. Phillip Mpango amelieleza Bunge leo mjini Dodoma kuwa Serikali iko katika majadiliano na IMF kuhusu ripoti ya Tanzania na kuna siku 14 za kujadiliana kufuatia wataalamu waliotumwa awali kutozingatia hoja za upande wa Serikali kama ulivyo utaratibu.
14 day's not far Mpango😎
 
Hii sitaki, nataka inayofanywa na serikali yetu itatufikisha pabaya, muda ni mwalimu mzuri sana !
 
Watanzania ni watu wa ajabu sana.

Bado mu miongoni mwa nchi masikini duniani halafu mnabishania ripoti ya uwezo wa kukopesheka?!

Mnataka kukopa nini?
 
Viongozi wachumia tumbo..mafisadi wanaogopa kuanikwa wazi,..kama mwajiamini kwanini muogope sasa..ndio mana Ripoti ya CAG mmetulia tuli kama hamuioni kumbe mjaa ufisadi..

Mwogopeni Mungu,Ogopeni kodi za wavuja jasho wa Tz.
Simamieni haki na kweli...mjisahihishe

Nchi yetu sote hii.

Uzi unaongelea IMF wewe unaongelea CAG!

Hivi huwa mnaelewa hata kinachojadiliwa ni nini? Au mradi muandike tu? Eti kwa kuwa tu sasa unamiliki kisimu kinachokuwezesha kuandika kwenye mtandao.
 
Inawezekana nikawa sina uweledi wa juu ya uwasilishaji wa taarifa za nchi katika jumuiya yeyote ya kimataiafa, ila naamini taarifa itabakia kuwa taarifa pindi baada ya kutayarishwa na kukidhi vigezo vya kuwa taarifa na kukabishiwa kwa upande husika ambao ndio wataichapisha au kuisoma na kuifanyia kazi kimya kimya. Kinachonishangaza ni kuwa kuna wataalamu ambao walitumwa awali na hawakuzingatia hoja za serikali kama ulivyo utaratibu? hapa kidogo kina ukakasi

Taarifa lazima iwe na vyanzo vyake ambavyo vinaaminika, kisha zinakusanywa pamoja na taarifa nyengine na kutengenezwa taarifa mama, sasa unaposema kuna wataalamu hawakua upande wa serikali ni kwamba taarifa haikuwa sahihi, au kuna data ambazo zinakinzana na yanayozungumzwa kwenye vyombo vya habari, hansad za bunge, kwenye tovuti za serikali au vp?

Ifike mahali kama kuna weusi tukubali kwamba mambo ni meusi na sio kusema mambo meupe wakati kabisa unaona kuna mambo meusi nyomi yametamalaki ndani yake. Hakuna binaadamu aliye kamili chini ya jua, na kama ulikuwa na nia njema ila hujafanikiwa basi amini katika vitabu vitakatifu kwamba kila zama na kitabu chake na ukiona jambo halijatimia basi jua wakati wake bado.

Au taarifa hizi ziliandikwa kwa mother tongiyo sasa wanataka kuziandika kwa kiingereza ndo wanapaeleka wataalamu wa kuzitengeneza? Ashindwaye pia ni mume toa taarifa watu wazione au ndo kama za Alhaj Asad wakataka kuficha ukweli naye akarusha bomu la Hiroshima mjini Dodoma mambo yakatindinganya.

Unataka kukopa nini?
 
Na ijulikane hao wataalamu ni wahuni wahuni, nadhani watafukuzwa kazi, maana IMF inaihitaji Tanzania zaidi ili kutukopesha, sasa inasikitisha zzk na uongo wake akidhani eti ni vyema kuwanyenyekea mabeberu, kwa IMF na world bank ni institutions nyonyaji sana!!!
Comedy inaanzia hapa " kazi, maana IMF inaihitaji Tanzania zaidi ili kutukopesha" Nacheka mpaka nasinzia walahi
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom