Waziri mmoja ni Raia wa Marekani: Gazeti la Dira

Titan, Masanja, Mwakatare na Sophist mimi naona mawazo yenu yamepitwa na wakati sana!!!

Kuna wanaosema eti Dual citizenship wafanyabiashara watakimbiza pesa nje je ni mfanya biashara gani ambae hawezi kukimbiza pesa nje kwasababu ya uraia. Hapa Marekani mtu yeyote anaweza kufungua account ya bank hata kama si raia, mtu yeyote anaruhusiwa kununua nyumba hata kama si raia!!! sasa mkisema kwasasa wafanyabishara hawapeleki pesa nje kwasababu ya uraia si ukweli kabisa, hata kuna Mawaziri na maraisi wana account nje. Hivyo hii hoja si ya kweli na niya ushabiki maana haina mfano zaidi ya maneno tu.

Hoja nyingine ni kwamba watu watafaidika! je watafaidika na nini? ambacho kwa sasa hawawezi kufaidika je Tanzania itawapa nini hawa watu walioko nje wafaidike?. Hakuna faidi yeyote nchi yetu ni masikini sababu kubwa ni ndugu na jamii. Kama Ndugu zako na mababu wawezikwa Tanzania ni vigumu kuomba visa ya kwenda kuangalia geneza la ndugu zako na ndiyo maana nimesema hii ni kwa watu waliozaliwa Tanzania na wenye wazazi Tanzania. Sasa nyie mnasema kama nina mtoto kazaliwa hapa na atakuwa raia wa marekani kuanzia siku ya kwanza na mimi nikitaka kumpa nyumba yangu kwa uzee haitawezekana na nyumba iende kwa serikali!!! je huyu mtoto au mimi nimefanya kosa gani bali kuwa nje.

Je Watanzania pesa zinazotoka Tanzania kuja kwa watu wanaoishi nje na pesa zinazoingia Tanzania kwa watu wanaoishi nje zipi ni nyingi?? na mnavyosema faida ni zipi hasa? mimi naona faidi ni kwa Tanzania na siyo kwa mtu anayeishi nje. Mimi nikija Tanzania serikali inanisaidia nini kuliko hapa Marekani?? Hakuna msaada wowote watu wa nje tunaoupata kutoka serikalini na sababu kubwa ya kuja na kutuma pesa Tanzania ni kwasababu ya uzawa na ndugu kama wazazi, wajomba, n.k

Kama hamna sababu ya msingi basi tukubaliane ni uivu tu na kutowapenda watanzania wanaoishi nje. Kitendo cha kusema kunawafanyabishara watakimbiza pesa si kweli kwani kunawafanyabishara wangapi wana account nje je mnafikiri Baresa, Mengi, n.k hawanapesa nje au wakitaka kwenda nchi yeyote wanaenda hata kama kuishi na kwa pesa yao wanapewa mpaka uraia.

Fikirieni nchi na si ubinafsi. Mnavyosema itamfaidisha vipi Mtanzania wa kawaida je nyie mnamsaidia vipi Mtanzania wa kawaida! kuna kidu gani ambacho wewe unafanya cha kuisaidia Tanzania kuliko mimi?

Tukubali wengi wetu ni wavivu wa kufikiri. Watanzania wakipata dual citizenship kuna faida kubwa 90% kuliko 10% hasara ya kufikirika tu kutokana na wachache ambao hawaepukiki hata kwa kutokuwa na dual citizenship. Mataifa yaliyoruhusu mfumo huo yananufaika zaidi na kujenga uchumi mkubwa katika nchi zao kwani raia waliopo nje ya nchi zao ni kiungo kuzuri cha biashara huria.
  • China - Wachina wamejaa sana nchi za nje na hivyo wanasaidia kupata soko la bidhaa zao nchi za nje, kama USA, Europe nk.
  • Philipine - Pesa ya kigeni inayoingia nchini homo kiasi kikubwa mno kinachangiwa na raia wao walioko mataifa ya nje.
  • Marekani - Imeweza kujenga uchumi wake kutokana na wahamiaji, licha ya wahaniaji kuchota pesa lakini muda wanaoishi huko husaidia kujenga uchumi wa nchi kwa mkondo wa ajira.
  • Mataifa ya West Afrika - Yamekuwa na kiungo kizuri cha kufanya biashara na mataifa ya nje kutokana na raia wake kuwa huru katika uraia.
  • Kenya na Uganda - Tanzania tunahangaika kuzifukuzia nchi hizo kiuchumi lakini hatuzikuti ina tunaishia wao wana mbinu za kibiashara na kiuchumi na hivyo tutabaki kuweka vipingamizi kwa watanzania wenzetu na kuwaacha wakenya na waganda kuja kuchuma kwetu.
Katika mengi watanzani tuko nyuma miaka 20 ndio tunakuja kuzinduka wakati wenzetu wameshapiga hatua kubwa sana katika mengi. Tatizo wengi wetu hatuna wivu wa kimaendeleo ila wivu wa kimapokeo, hili ndilo tatizo. Na siasa za ujamaa ndizo zilizotuharibu akili wengi wetu, na madhara yake ndio hayo.

Ulimwengu wa sasa ni global village, sasa watanzania wenzetu wanaturudisha kwenye zama za analog wakati ulimwengu wa global village ni wa digital. Inachosha na kukatisha tamaa, kwani jitihada za kujenga uchumi si kulalamikia kodi tu, kuna njia nyingi sana na zile tunazopuuza na kuzidhara ndizo wenzetu wanazotumia kupiga hatua mbele.
 
Jamani hapo kwa Mheshimiwa Chami mwaka wa kuzaliwa umekosewa au vipi! Kazaliwa 1954 shule kaanza 1974 kwa maana hiyo alianza darasa la kwanza akiwa na miaka 20!?
 
Mzee kwa China hapo umechapia kabisa. Taratibu za uraia China ni very complicated kuliko Marekani na Tanzania. Sema mengine mkuu ila suala la China liache kabisa na usilitolee mfano.

Tatizo la Watanzania ni ushabiki na uivu na ndiyo maana nchi yetu haiendelei. Je ni kwanini hatuna Dual Citizenship mpaka sasa

Nchi za ulaya, India, China, Nigeria, Mexico, USA etc zina ruhusu Dual je sisi ni kwanini hatuna, je tuna kitu gani special na hizi nchi nyingine hazina??. Kama mtu ni mzawa au ni mtoto wa mzawa sioni sababu ya muhimu ya kumnyima Dual Citizenship. Zaidi ya kejeli, madongo, na wivu kwa Watanzania wanaoishi nje hakuna sababu ya msingi ya kutokuwa na Dual Citizenship.
 
Ujinga ni pamoja na kushindwa kujenga hoja za msingi, hivi kumlani waziri mwenye uraia wa Marekani ndo kusema na wivu? hebu watu wapime vitu wanavyoandika hapa sio kuweka upuuzi wa namna hii, inakera sana
 
Tatizo la Watanzania ni ushabiki na uivu na ndiyo maana nchi yetu haiendelei. Je ni kwanini hatuna Dual Citizenship mpaka sasa

Nchi za ulaya, India, China, Nigeria, Mexico, USA etc zina ruhusu Dual je sisi ni kwanini hatuna, je tuna kitu gani special na hizi nchi nyingine hazina??. Kama mtu ni mzawa au ni mtoto wa mzawa sioni sababu ya muhimu ya kumnyima Dual Citizenship. Zaidi ya kejeli, madongo, na wivu kwa Watanzania wanaoishi nje hakuna sababu ya msingi ya kutokuwa na Dual Citizenship.
By the way United States of America do not allow Dual Citizenship
 
ndio huyu nini?ndo maaan kwa miaka 5 alichelewesha vitambulisho vya uraia

MashaLaw.jpg


+
 
Tunahitaj majibu,vp raia wa USA awe wazir wa Tanzania?juz tu Obama ilimbidi kuthibitisha uraia wake hadharan,baada ya kuhojiwa km n raia wa Marekan au ni raia wa kenya.inamaana hata wao wenye hiyo dual ctizen hawakubal kiongoz kuwa na uraia POPO.vp cye tusihoji umaluuni huu!? Et twaitwa wenye wivu!? Hawa watu sampuli hii ni mawakala wa wakolon,tena huu n ulemavu wa akil nenden Loliondo mpate tiba nyie watumwa wa fikra.
 
Siyo shida kama ni raia kama Taifa lako ninakubali hilo na kuona jinsi gani tulivyo wagumu kufikiria
 
Fuatilia kwanza vigezo ambavo vinaweza kumfanya rais ajiuzulu. Ndo utoe pendekezo lako. Inaonekana hukusoma siasa wewe.

Usitishe watanzania na usomi wa siasa wewe!!
Tulikuwa na David Balali Akatukomba na kuwasaidia CCM kuiba Benk Kuu akakimbilia Marekani. Kama kazi ya JK ni kuleta mamluki kutuibia na kusaidia ujambazi na kukimbilia nje ya nchi wengine wanakufa kwa kiini macho, TUNAWEZA KUMUONDOA KWA NGUVU YA UMMA HATUHITAJI ELIMU YA SIASA. TUPENI FACTS TUFANYE KAZI HARAKA.

INAKASIRIKA SANA.
 
Hivi huyo waziri amekaa miaka mingapi USA mpaka mufikirie anaweza kuwa raia wa huko?

Kupata uraia wa nchi nyingine sio rahisi sana kwa mtu aliyeenda kama mwanafunzi.

Labda kama aliwahi kukaa USA akiwa mdogo vinginevyo hiyo miaka kama 6 isingeliweza kumfanya awe na sifa za kuwa raia wa USA.
 
Waziri wa fedha naye ni raia wa Malawi.
Wapo wengi tu; ndani ya chama cha magamba tena ndo usiseme.
 
Hivi huyo waziri amekaa miaka mingapi USA mpaka mufikirie anaweza kuwa raia wa huko?

Kupata uraia wa nchi nyingine sio rahisi sana kwa mtu aliyeenda kama mwanafunzi.

Labda kama aliwahi kukaa USA akiwa mdogo vinginevyo hiyo miaka kama 6 isingeliweza kumfanya awe na sifa za kuwa raia wa USA.

Miaka 3 hadi 5 inatosha kabisa mkuu kupata US citizenship!!
 
Unapochukua uraia wa USA huna haja ya kuukana utanzania. You can keep your passport.

Hiyo ni sawa, ila in ukichukua uraia wa nchi nyingine, US inclusive, you have effectively denounced/rejected Tanznaian citizenship.
 
Back
Top Bottom