Waziri Mkuu wa Lesotho na Mkewe wakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya aliyekuwa mke wake wa kwanza

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,500
9,279
Waziri Mkuu Lesotho na mke wake wanakabiliwa na uchunguzi unaohusiana na tuhuma za mauaji ambayo yanaweza kuangaziwa katika tamthilia ya kitabu cha hadithi za uhalifu. Mwandushi wa BBC Pumza Fihlani anajaribu kuchambua kisa chao kutoka mji mkuu wa taifa hilo la kusuni mwa Afrika, Maseru.

Watu wanaendelea na shughuli zao za kila siku katika mji huo. Wauzaji mboga wamepanga bidhaa zao kando ya barabara, magari ya uchukuzi wa umma kama vile taxi pia zinawachukua abiria na kuwapeleka katika sehemu tofauti za kazi na kukimbilia wateja wengine.

Kwa kweli kila kitu kinaendeshwa kwa mpangilio utadhani mambo ni shwari. Lakini ukisoma gazeti utapatana na tangazo maalum. Tangazo hilo limewekwa kwenye mabango ya biashara katika barabara kuu za mji wa Maseru na hata katika madirisha ya maduka jijini humo kuashiria kwamba kuna jambo ambalo haliko sawa Lesotho.

Tangazo lenyewe ni la kumtafuta "Mama taifa aliyetoweka." Hii bila shaka inaelezea bayana kuwa hali sio shwari nchini Lesotho.

Moja ya taarifa kuu katika gazeti imeandikwa: "Polisi inamsaka mama taifa." Nyingine inasema: "Waziri mkuu aliye mashakani akubali kujiuzulu."

Kiongozi huyo wa ngazi ya juu nchini - Waziri Mkuu Thomas Thabane pamoja na mke wake wa sasa Maesaiah Thabane - wanatakiwa kuhojiwa kuhusiana na mauaji ya mwaka 2017 ya mke wa kwanza wa Bw. Thabane, Lipolelo Thabane.

Bi Lipolelo mwenye umri wa miaka 58, alikuwa ametengana na mume wake na amekuwa akiishi kivyake tangu mwaka 2012, aliuawa siku mbili kabla ya Bw. Thabane kuapishwa kuwa waziri mkuu.

Jioni moja akiwa njiani kurejea nyumbani kutoka kwa shughuli zake za siku, alishambuliwa na kupigwa risasi mara kadhaa na baadae kupatikana akiwa amekufa kando ya bara bara.

Kifo chake kilishangaza nchi nzima. Wakati huo Bw. Thabane alielezea mauaji hayo kuwa ya "kinyama".

Wakati huo mauaji hayo tylisemekana kutekelezwa na watu wasiojulikana. Lakini ushahidi wa hivi karibuni uliowasilishwa mahakamani na kamishena wa polisi wa nchi hiyo, Holomo Molibeli, umeibua maswali mengi zaidi ambayo yanahitaji ufumbuzi.

Baadhi ya stakabadhi za mahakama, zilizoonekana na shirika la habari la AFP, ilikuwa ni nakala ya barua iliyoandikwa tarehe 23 Desemba 2019, iliyoandikwa na kiongozi huyo wa polisi kwa waziri mkuu aliye na umri wa miaka 80 na ilisema:

"uchunguzi umebaini kwamba kulikuwa na mawasiliano ya simu katika eneo la uhalifu tunaochunguza... kwa kutumia nambari nyingine ya simu. Nambari hiyo ya simu ya rununu ni yako."

Waranti ya kukamatwa kwa Maesaiah Thabane, 42, ilitolewa Januari 10 baada ya mshukiwa huyo kukataa agizo la kumtaka afike kituo cha polisi kwa mahojiano.

Hajaonekana hadharani kwa wiki mbili na hakuna mtu anayejua alipo na wala hakuna mtu yeyote anayetaka kuzungumzia suala hilo.

Bw. Thabane, ambaye bado yupo nchini, amekwepa kujibu maswali kuhusiana na alipo mke wake.

BBC imewasiliana na maafisa wa serikali kwa tamko rasmi kuhusiana na sakata hii lakini juhudi hizo zimegonga mwamba. Msemaji wa chama cha waziri mkuu amesema kuwa "swala hilo halijashughulikiwa".
 
... kwa Afrika zitapigwa danadana mwisho shauri litafutwa. PM (80) wife (42); what a difference!
 
1580906476825.png
 
Back
Top Bottom