Waziri Mkuu wa Uholanzi akiwasili ofisini kwa usafiri wa baiskeli. Je, viongozi wetu wanaweza kufanya hivi?

measkron

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
3,782
2,406
Wakuu katika pita pita nimekutana na hii picha ya Waziri mkuu wa Uholanzi akitumia baiskeli kuelekea ofisini, je viongozi wetu wanaweza hii?

Can-we-ever-imagine-PINDAi-prime-minister-using-cycle-to-go-to-office.jpg

attachment.php
 
Hayo mambo ilikuwa enzi za Mwalimu, sasa hivi wanashindana kubadilisha V8 na BMW...
 
Hayo mambo ilikuwa enzi za Mwalimu, sasa hivi wanashindana kubadilisha V8 na BMW...
Ni lini JKN alitumia baiskeli kwenda kazini? Unajua enzi zake kulikuwa na Rolls Royce na ndege ya Rais ijapokuwa wananchi walikatazwa kabisa kuwa na magari?
 
Ni lini JKN alitumia baiskeli kwenda kazini? Unajua enzi zake kulikuwa na Rolls Royce na ndege ya Rais ijapokuwa wananchi walikatazwa kabisa kuwa na magari?

Mkuu ishu sio "Baiskeli" think out of the box... kinachotafsiliwa hapo ni kwamba mkuu wa nchi anakuwa mtu wa kubana matumizi na kuishi maisha ya chini na ya kawaida, Je, ccm ya JK inafanya hivyo? Je, wanaisha au wanatenda in accordance to their words of mouth??? Jibu ni NO. Serikali imekuwa loose, matumizi ya hovyo na ya juu yako mengi sana...
 
Mkuu ishu sio "Baiskeli" think out of the box... kinachotafsiliwa hapo ni kwamba mkuu wa nchi anakuwa mtu wa kubana matumizi na kuishi maisha ya chini na ya kawaida, Je, ccm ya JK inafanya hivyo? Je, wanaisha au wanatenda in accordance to their words of mouth??? Jibu ni NO. Serikali imekuwa loose, matumizi ya hovyo na ya juu yako mengi sana...

Mkuu umenena vyema, this is how a great thinker anavyopambanua mambo!
 
Mkuu ishu sio "Baiskeli" think out of the box... kinachotafsiliwa hapo ni kwamba mkuu wa nchi anakuwa mtu wa kubana matumizi na kuishi maisha ya chini na ya kawaida, Je, ccm ya JK inafanya hivyo? Je, wanaisha au wanatenda in accordance to their words of mouth??? Jibu ni NO. Serikali imekuwa loose, matumizi ya hovyo na ya juu yako mengi sana...
Mkuu kwa wenzetu kupanda Baiskel siyo kubana matumizi ni sehemu ya kufanya mazoezi. Hata mayor wa London anakwenda kazini na baiskeli tena kila siku
 
pia ni kama zoezu ila kwa tz ni ngumu sana,hata angefanya wabongo wataanza kuongea ,oh anajifanya,oh ni mnafiki,ooh anaaibisha taifa
 
Huenda hicho kilikuwa kipindi cha kampeni na ndiyo maana hata huko Uholanzi kilionekana kitu cha kuvutia, angalia waandishi wa habari walivyo makini kupata hizo piacha. Hii ina maanisha kalikuwa kitu cha kawaida kutoka. Alikwa anatafuata huruma za waholanzi. Hivi ndiyo wananchi wanavyodanganywa na kuaminishwa kuwa kioongozi wa namna hiyo ndiyo anayefaa. Ingekuwa ni jambo la kawaida hapakuwa na haja ya kutoa kitu kama hicho kwenye gazeti. Ni sawa na leo mtu kumtoa Pinda kwenye gazeti akiingia ofisini kwake na VX.

Na kila jambo na wakati wake. Watumie VX leo lakini watuletee maendeleo hatuna ugomvi nao.
 
Purchase and capacity of official vehicles for certain
Government officers.

7. (1) Official vehicles purchased for use by Ministers, the Speaker of the National Assembly, the Chief Justice, the Attorney-General and the Head of the Public Service, shall not exceed 2600 cc for saloon cars and 3000 cc for 4 x 4 utility vehicles.(2) Official vehicles purchased for use by Permanent Secretaries, Accounting Officers, Court of Appeal Judges, the Controller and Auditor-General, the Chairman of the Public Service Commission, the Chairman of the Electoral Commission of Kenya, Provincial Commissioners and the Commissioner of Police shall not exceed 2400 cc for saloon cars and 3000 cc for 4 x 4 utility vehicles.
(3) Official vehicles purchased for use by officers on Job Group R and above, High Court Judges and Chief Executives of state corporations shall not exceed 2000 cc for saloon cars and 2900 cc for 4 x 4 utility vehicles:
Provided that this section shall not apply in case of vehiclepurchased for official use by the President and the Vice-President.
_________________________________________________________________________________________________________________Hii nimeikuta kwenye Sheria ya Umimamiaji wa Fedha za Serikali Kenya.
Watanzania tunaionaje hiyo na msururu wa mashangingi kwa viongozi wetu.
 
Mkuu ishu sio "Baiskeli" think out of the box... kinachotafsiliwa hapo ni kwamba mkuu wa nchi anakuwa mtu wa kubana matumizi na kuishi maisha ya chini na ya kawaida, Je, ccm ya JK inafanya hivyo? Je, wanaisha au wanatenda in accordance to their words of mouth??? Jibu ni NO. Serikali imekuwa loose, matumizi ya hovyo na ya juu yako mengi sana...


Thinking out of the box should not mean "wild thinking"- anything goes because I want it to be that way. I did not want to compare things which are not the same. I wanted to compare a BMW with a Rolls Royce and a plane with a plane. That is all. If there are any other parameters which need to be called into comparison, then lets bring them in.

I do not want to dig deep into what used to happen in Nyerere's time and what is happening now although I know a lot about both sides. Nyerere as a person and most of his subordinates lived frugal life but led a government which was just as wasteful.
 
Pamoja na kuwa sehemu ya kufanya mazoezi hapa kuna mambo mengi. Kwanza miundo mbinu ya wenzetu inaruhusu mtu kwenda na baiskeli kazini maana kuna njia mahususi ya waendesha baiskeli imetengwa barabarani, na hata Bongo ingekuwa hivi wengi tungeendesha baiskeli kwenda kazini. Pili ni suala la usalama. Viongozi kwa hao wenzetu si wezi wa mali za umma. Wako pale kuwatumikia wananchi wao na kwahiyo hawana uadui na watu wanaowatumikia. Hapa kwetu viongozi wamejijengea uadui na watu wanaowaongoza kwa kuwaibia rasilimali zao na kujilimbikia mali ili hali wao (wananchi) wanataabika na maisha. Kwahiyo kiongozi akipanda baiskeli watampopoa kwa mawe.
 
Pamoja na kuwa sehemu ya kufanya mazoezi hapa kuna mambo mengi. Kwanza miundo mbinu ya wenzetu inaruhusu mtu kwenda na baiskeli kazini maana kuna njia mahususi ya waendesha baiskeli imetengwa barabarani, na hata Bongo ingekuwa hivi wengi tungeendesha baiskeli kwenda kazini. Pili ni suala la usalama. Viongozi kwa hao wenzetu si wezi wa mali za umma. Wako pale kuwatumikia wananchi wao na kwahiyo hawana uadui na watu wanaowatumikia. Hapa kwetu viongozi wamejijengea uadui na watu wanaowaongoza kwa kuwaibia rasilimali zao na kujilimbikia mali ili hali wao (wananchi) wanataabika na maisha. Kwahiyo kiongozi akipanda baiskeli watampopoa kwa mawe.

Huwezi kujua adui wa kiongozi ni nani, na uadui siyo lazima utokane na wizi peke yake. Kumbuka wakuu wa nchi wafuatao ambao waliuawa ijapokuwa watu walikuwa wanawapenda sana - Olf Palme wa Sweden na J F Kennedy wa marekani. Kumbuka vilevile kuna watu wanapenda kuuwa watu mashuhuri ili wapate umashuhuri kuwa walimwua mtu mashuhuri - kumbukwa muuaji ya Lennon na aliyetaka kumwua rais reagan wa Marekani.
 
Waziri mkuu wa Holland akirejea nyumbani ndani ya usafiri akitokea ofisini, je wa kwetu anaweza kwenda ofisini na usafiri huu??
 

Attachments

  • waziri mkuu wa Holland.jpg
    waziri mkuu wa Holland.jpg
    66.2 KB · Views: 342
Mh. Pinda (mtoto wa mkulima)ndiye aliye kwenye nafasi nzuri ya kujibu swali lako.
 
Back
Top Bottom