Waziri mkuu wa Canada anakuja Tanzania

nchi ishauzwa na JK na mashaka sana ule mkataba aliosaini bila hata kuusoma
ni sawa na chief mangunge wa msowero alivoambiwa na wajerumani asiani

JK yeye huyoo nchi kichafuka ashaahidiwa pa kukimbilia
kazi ipo Tanzania alisuluhisha migogoro ya kenya zamu hii CCM wasipokuwa makini Kenya watakuja kusuluhisha kwetu
 
Mkuu Mkandara umeanzisha mada muhimu sana bahati mbaya vyama vya upinzani [mbadala] badala ya kuifanyia kazi ziara ya Mheshimiwa Harper utashangaa watakuwa na muda malumbano na RPC wa Iringa ambaye tunaye kila siku.


Ipo haja ya kuandaa maandamano makubwa ya kulaani makampuni ya Canada yanayoshirikiana na wanasiasa wezi atakapotua J N Airport.Nategemea pia kurugenzi ya mambo ya nje ya vyama vyote vya siasa makini watandaa waraka unaoelezea ufisadi wa makampuni yote ya Canada na kuukabidhi kwa Mheshimiwa Harper.

Nakala Ritz Mwita Maranya jmushi1 FJM na wengine.


Wakuu zangu naomba tujadili hii safari ya waziri mkuu wa Canada, Mheshimiwa Harper ambaye atatua nchini muda wowote itakuwa na manufaa gani kwetu na pia tujadili ni jinsi gani ujumbe wetu unaweza kumfikia..
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara umeanzisha mada muhimu sana bahati mbaya vyama vya upinzani [mbadala] badala ya kuifanyia kazi ziara ya Mheshimiwa Harper utashangaa watakuwa na muda malumbano na RPC wa Iringa ambaye tunaye kila siku.


Ipo haja ya kuandaa maandamano makubwa ya kulaani makampuni ya Canada yanayoshirikiana na wanasiasa wezi atakapotua J N Airport.Nategemea pia kurugenzi ya mambo ya nje ya vyama vyote vya siasa makini watandaa waraka unaoelezea ufisadi wa makampuni yote ya Canada na kuukabidhi kwa Mheshimiwa Harper.

Nakala Ritz Mwita Maranya jmushi1 FJM na wengine.
Unajua binafsi yangu sielewi kabisa kama viongozi wetu wanajua walichokifanya na kwa faida ya Tanzania ama watanzania kwa sababu Mkataba wowote unaolinda Kampuni za Nje kwa kutumia sheria za nje unatuweka mahala pabaya sana. Special treatment kwa mashirika haya ni kukubali kukoloniwa - Ukoloni mamboleo.

Kama mnakumbuka Mukama alipotangaza kupitia upya mikataba pamoja na ulipaji kodi, hao Barricks hawakukawia kutangaza wanakitoa na kuuza mali zao kwa Wachina. Mukamam akabadilisha kauli mara tumeona JK akienda Canada nchi ambayo hajawahi kuitemebela kwa miaka yote alikaa Ikulu..Binafsi nina hakika kabisa ujio wa JK nchini Canada haukuwa wa bahati mbaya isipokuwa Barricks na mashirika ya madini nchini waliishinikiza serikali yao kusimama kidete kuetetea Investment zao. Na ndio maana JK akapewa Royal treat kumweka sawa akili wakijua sana jamaa anapenda sifa.

Jamani sielewi Wadanganyika wataelimika lini. Kukubali kutujmia sheria za Canada ktk mkataba huu wa FIPA wakati sisi wenyewe hatuna kipengele cha kulinda makampuni ya Kitanzania nchini Canada na wala hatuna makampuni hayo huko ni kuingizwa mtegoni. Na nawahakikishia Canada haiwezi kukubali sheria hiyo hiyo itumike kwao hata siku moja. Hawawezi kukubali shirika la Tanzania lilindwe na sheria za Tanzania - haiwezekani na sheria au mkataba huo hautapita bungeni NEVER!. isipokuwa sisi tumeenda kuweka mkataba wa sheria inayokata upande mmoja na hata kama ingekuwa inakata kote hatuna mashirika ya uwekezaji Canada -_ tutaibiwa lakini hatuwezi kuwaibia wao ng'ooo...

Hawa jamaa inapofikia maslahi ya nchi zao, inapofikia Interest zao nje wako tayari kupigana vita, kudhulumu na hata kukuwekea vikwazo unapotaka kuwapokonya tonge mdomoni..Nawaomba wanasheria wetu walipitie swala hili kwa umakini mkubwa sana na kuogopa yaliyomo maana yatatufiunga sisi wenyewe baada hata baada ya kuibiwa sana hatutakuwa na mahala pa kushtaki maana UBEBERU kwao ndio mtaji, na hakuna haramu ijnapofikia swala la Mkataba maana huyu huyu harper alipokuja Tanzania miaka 3 iliyopita alisema wazi hawezi kutusaidia lolote kuhusu mikataba tulokwisha iweka.. Ni nje ya uwezo wake, sasa leo imekuwaje yeye tena amekuja tusainisha mkataba unaolinda mashrika ya Canada nchini Tanzania?
 
Canada's main exports to Tanzania, amounting to $61.5 million in 2011, consisted primarily of used clothing, machinery, and wheat. Canadian imports from Tanzania amounted to $5.3 million, comprising mainly coffee, tea, and cashews. In July 2003, Canada and Tanzania signed an agreement to permit duty-free access for almost all goods produced in Tanzania.


Canada - Tanzania Relations
Ningependa sana kuelewa ni mashirika gani yana import coffee, tea na cashews kutoka Tanzania maana sijawahi kuona hata kitu kimoja kimeandikwa made in Tanzania wakati mimi ni mtumiaji mkubwa wa vitu hivyo.
 
Back
Top Bottom