Waziri Mkuu na Spika kutoka Zanzibar

Msulibasi

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
5,836
7,492
Wakuu hivi ni sababu gani hatujawahi kuwa na waziri Mkuu wa JMT ama Spika wa URT kutoka Zanzibar . Je, ni sababu za kikatiba na sheria, utamaduni , weledi au sera ya CHAMA tawala?

Ni wakati Sasa wa mgombea wa upinzani kuahidi kutupatia wazanzibari fursa hizi adhimu.

Katika siasa kete mojawapo ni kupata wafuasi kwa kutumia teuzi. Mgombea wa CCM anajua sana hii kazi ya kugawa vyeo. Mfano alipomkata yule pacha mmoja kwenye ubunge akaahidi kumuundia wilaya mpya.

Alipokuwa Shinyanga akaahidi kumpa nafasi Maselle na Kyerwa akaahidi nafasi kwa mama Tibaijuka huku Kigoma akitoa sababu za kuwa na mawaziri watatu.

LISSU anaweza kuahidi nafasi pia katika kuwagawa wapinzani wake na kupata sapoti ya upande Fulani.
 
Salim A. Salim
Unaongelea zaidi ya miaka 35 iliyopita? Zanzibar ni equal patner katika muungano wetu. Tanganyika na Zanzibar zote zilikuwa nchi huru. Wakati umefika kwa Wazanzibar siyo tu kupewa nafasi ya PM lakini hata ya urais, spika na Jaji mkuu wa JMT.

Wake up Zanzibar...hamna cha kupoteza zaidi ya unyonge wenu.
 
Unaongelea zaidi ya miaka 35 iliyopita? Zanzibar ni equal patner katika muungano wetu. Tanganyika na Zanzibar zote zilikuwa nchi huru. Wakati umefika kwa Wazanzibar siyo tu kupewa nafasi ya PM lakini hata ya urais, spika na Jaji mkuu wa JMT.

Wake up Zanzibar...hamna cha kupoteza zaidi ya unyonge wenu.

Kama ni equal partner wangechangia gharama za uendeshaji wa shughuli za muungano eg Police,JWTZ,Uhamiaji na kulipa bill za umeme.
 
Kama ni equal partner wangechangia gharama za uendeshaji wa shughuli za muungano eg Police,JWTZ,Uhamiaji na kulipa bill za umeme.
Hawajawahi kushindwa. Mmeiminya isiweze kupatambulika kimataifa na kupata misaada na mikopo kama Tanganyika inavyofanya kupitia koti la Muungano. Zanzibar haipewei stahiki yake ya mapato toka TRA kila mwaka kama sheria inavyotaka.

Zanzibar ikiachwa huru au ikapewa fursa ya kutumia koti la muungano kama inavyofanya Tanganyika itakuwa mbali sana.

Waacheni wajiamulie wenyewe hatma ya rasimali zake kama mafuta, uvuvi wa bahari na anga halafu tuone kama hawezi kuchangia kwenye Muungano.
 
Tukiwaachia kukopa hovyo bila tahadhari tunaweza kuja kuwalipia madeni yao kama tunavyowalipia bill za umeme.
 
Tukiwaachia kukopa hovyo bila tahadhari tunaweza kuja kuwalipia madeni yao kama tunavyowalipia bill za umeme.
Hivi hata uspika hatupewi ama tu unaibu spika hivi vimekua vyeo vya bara tu
 
Lissu tukonaye humu Jf kwa hiyo fikra na ushauri rukhsa ni msikivu
 
Unaongelea zaidi ya miaka 35 iliyopita? Zanzibar ni equal patner katika muungano wetu. Tanganyika na Zanzibar zote zilikuwa nchi huru. Wakati umefika kwa Wazanzibar siyo tu kupewa nafasi ya PM lakini hata ya urais, spika na Jaji mkuu wa JMT.

Wake up Zanzibar...hamna cha kupoteza zaidi ya unyonge wenu.
Marehemu..Mzee Augustine Ramadhani alitokea wapi!??(Jaji mkuu mstaafu)
 
Ushauri wangu hayo majimbo ya Zanzibar walioiengua ActWazalendo wanaActWazalendo kura zote wapeleke kwa wagombea wa Chadema
 
Back
Top Bottom