Waziri Mkuu Pinda asitisha utekelezaji wa agizo la Magufuli la Bomoa bomoa

Kitaratibu, kiutawala, kikatiba, kisheria, ni jambo gani ambalo ni lazima lipitie Baraza la Mawaziri?

Kumbuka Ngeleja alipotangaza kulipa Dowans, Sitta na Sumaye wakasema "haijapita baraza la Mawaziri." Kumbuka kuuzwa nyumba za serikali zilizopita Baraza la Mawaziri, watu wakasema haijapita Bungeni. Kumbuka Mkataba wa Richmond Mwakyembe alioandika hajaona kumbukumbu ya kikao cha baraza. Jambo gani ni lazima lipitie Baraza la Mawaziri, na imeandikwa wapi?
 
waziri mkuu mizengo pinda "mtoto wa mkulima", amesema kazi ya john pombe magufuli ni kushughulikia rushwa iliyokithiri ujenzi na si kubomoabomoa nyumba zilizojengwa kwenye hifadhi ya barabara na kwa hivyo amemtaka aache bomoabomoa.

My take:
Pinda anataka kutuambia kwamba magufuli kazi yake ni kupambana na rushwa ujenzi kwa hiyo tusahau ujenzi wa miundo mbinu, no wonder sijasikia ujenzi wowote uloanza pamoja na uchapakazi wa magufuli. Ahadi hii tuisahau.

Lakini pinda kwa matamshi yake haoni kwamba anavunja sheria kwa kuruhusu watu kujenga kwenye eneo la hifadhi ya barabara? Pinda nilitegemea awe wa kwanza kukemea uvunjaji wa sheria. Hatuna waziri mkuu.

Hivi serikalini bado hakuna collective responsibility? Mambo aliyokuwa anayafanya magufuli ni kwa kukurupuka kwake, hawakuamua kwa pamoja. Hivi tuna serikali kweli au vurugu na fujo?

Mheshimiwa magufuli umedhalilishwa, yaani jitihada zote hizo ni bure, ningekushauri ung'atuke, jiunge chadema, gombea ubunge kwenye uchaguzi mdogo wa chato utakaofanyika baada ya wewe kujiuzulu, utapewa huo uwaziri baada ya cdm kuchukua nchi.

waziri mkuu tunaye sana, tatizo lako kapotolo umelishwa propaganda za magufuli na wewe kuzichukulia zilivyo. Imebidi waziri mkuu aingile kati ili kuokoa fdha za serikali kulazimika kuwalipa watu fidia baada ya kushinda kezi zao mahakamani kama ilivyotokea 2001 wakati magaufuli alapoagiza petrola station mjini mwanza ibomolewe kwa kuwa imejengwa katika hifadhi ya abarabara kumbe sio kweli hata kidogo. Serikali ililazimika kulipa fidia ya bilini 3 kwa mmiliki wa petrol station iliyobomolewa. Baadaye ukweli halisi ulifichuka kuwa magufuli alikuwa na chuki na mahndisi wa jiji la mwazana mahandisi tizeba toka hapo wizarani, tume ya jiji mpaka alipohamishiwa jiji la mwanza kama mhandisi wa jiji la mwanza. Aliwahi hata kufanya jitihada za kujaribu jina la mhandisi huyo kufutwa katika orodha ya wahandisi waliosajiliwa hapa nchini. Katika kutimiza kiu ya chuki zake na mhanddisi huyo ndipo akaamuru ibomolewe.

Jumamosi iliyopita ulikuwepo na mkutano wa waathirika wa eneo la ubugo kimara, zaidi ya watu 50 wana hati miliki, na nyumba zao tayari zimechafuliwa kwa kuweka alama ya x na "maneno bomoa mali ya tanroad" je huo si ukiukwaji wa sheria za nchi? Mtu kama huyu unaweza kusema nafuta sheri kweli? Kwani magafuli anatumika serikali ipi na ni serikali ipi iliyowapatia wananchi hao hati miliki?

Ibara ya 2 ya sheria ya barabara ya 1967 inatamka wazi wazi kuwa hifadhi ya barabara zote kuu (trunk roads) hapa nchini itakuwa futi 75 au mita 22.86 kila upande sawa na futi 150 au mita 45 pande zote mbaiuli. Ibara ya 27 ya kanuni za sheria ya barabara ya 2007 zilizopitishwa kupita tangazo la serikai na 21 la tar 23 januari 2009 inatamka kuwa upana wa chini kabisa wa "lane" moja ya barabara kuu hapa nchin utakuwa si chini ya ni mita 3.25. Hivyo eneo la hifadhi ya barabara la mita 45 lina uwezo wa kuzalisha lane 14; lane 7 za kwenda upande mmoja na lane 7 za kwenda upande mwingine. Nitajie barabar gani hapa nchini imewahi kutumia na kumaliza upana huo uliotengwa kiasi cha magafuli kuwavamia watu walioko mita 120 kutoka katakati ya barabara? Hivyo ni propaganda kudai kuwa msongamano wa magari unasababsihwa na watu kujenga katika hifadhi ya barabara.

Kifungu cha 15 na 16 cha sheria ya aradhi namba 5 ya 1999 vinatamka kuwa ugawaji wa ardhi uliofanyikia wakati wa operesheni vijiji ni halali (soma attachement) hivyo sheria ya barabara ya 1967 anayotumia magufuli mwaka 2001 hadi 2010 imeshafutika na haiapo kabisa. Maaufuli anatakiwa kwanza kujenga lane 14 katika hifadhi ya barabara iliyopo ndipo aje kuwaingilia walioko nje ya eneo hilo. Kwa hali hii utagundua kuwa mambo anayoyafanya magufuli ni matokeo ya kukurupuka kwake katika yote hamshirikishi ofisi ya waziri mku, wizara zingine, ngazi za mkoa, wilaya, manispaa, serikali za mitaa
 
Kitaratibu, kiutawala, kikatiba, kisheria, ni jambo gani ambalo ni lazima lipitie Baraza la Mawaziri?

Kumbuka Ngeleja alipotangaza kulipa Dowans, Sitta na Sumaye wakasema "haijapita baraza la Mawaziri." Kumbuka kuuzwa nyumba za serikali zilizopita Baraza la Mawaziri, watu wakasema haijapita Bungeni. Kumbuka Mkataba wa Richmond Mwakyembe alioandika hajaona kumbukumbu ya kikao cha baraza. Jambo gani ni lazima lipitie Baraza la Mawaziri, na imeandikwa wapi?

Kila kitu kinacholenga maslahi ya Taifa, isipokuwa kama kaufisadi kapo.
 
Kikwete alidahani Magufuli ataona la kufanya. Nadhani Magufuli atakiwi kuendelea kujikomba kwa CCM. Anaipenda nadhani zaidi ya kitu chochote. Nina sababu kusema hivyo kutikana na na yafuatayo:


  • kabla ya 2005 walishiriki kumpa kashfa lukuki za nyumba ambazo tangu kikwete awe rais, ilikuwa kummaliza nguvu ili asigombee urais kwani nyota yake ilikuwa juu sana.
  • kikwete alipopata urais akalazimika kumweka Ardhi, alipofanya mambo yake yaliyogusa vigogo akamweka wizara ya kitoweo nako akafanya mambo yake ikiwa ni kukamata meli inayodaiwa kumilikiwa na vigogo
  • jambo liliokuwa baya ni pale alipopewa wizara ambayo imepunjwa saaaaaana, hii ya sasa. Ujenzi, hasa barabara akaondolewa Bandari ambako kuna ufisadi balaa, Reli na Anga. Akabakizwa barabarani tu!!!!!
Sasa ameonesha makeke yake. Walidhani atakaa ofsini tu kwani serilkali haina hela ya kujenga barabara.
 
magufuli ajiuzulu kwa kuzuiwa kufanya kazi yake kwa ufanisi! That is the next step forward....

ufanisi? Ni ule uliosababisha serikali kulipa fidia ya bilioni 3 kwa kubomoa petrol station jijini mwanza kwa madai kuwa imejengwa katika hifadhi ya barabara au upi?
 
waziri mkuu tunaye sana, tatizo lako kapotolo umelishwa propaganda za magufuli na wewe kuzichukulia zilivyo. Imebidi waziri mkuu aingile kati ili kuokoa fdha za serikali kulazimika kuwalipa watu fidia baada ya kushinda kezi zao mahakamani kama ilivyotokea 2001 wakati magaufuli alapoagiza petrola station mjini mwanza ibomolewe kwa kuwa imejengwa katika hifadhi ya abarabara kumbe sio kweli hata kidogo. Serikali ililazimika kulipa fidia ya bilini 3 kwa mmiliki wa petrol station iliyobomolewa. Baadaye ukweli halisi ulifichuka kuwa magufuli alikuwa na chuki na mahndisi wa jiji la mwazana mahandisi tizeba toka hapo wizarani, tume ya jiji mpaka alipohamishiwa jiji la mwanza kama mhandisi wa jiji la mwanza. Aliwahi hata kufanya jitihada za kujaribu jina la mhandisi huyo kufutwa katika orodha ya wahandisi waliosajiliwa hapa nchini. Katika kutimiza kiu ya chuki zake na mhanddisi huyo ndipo akaamuru ibomolewe.

Jumamosi iliyopita ulikuwepo na mkutano wa waathirika wa eneo la ubugo kimara, zaidi ya watu 50 wana hati miliki, na nyumba zao tayari zimechafuliwa kwa kuweka alama ya x na "maneno bomoa mali ya tanroad" je huo si ukiukwaji wa sheria za nchi? Mtu kama huyu unaweza kusema nafuta sheri kweli? Kwani magafuli anatumika serikali ipi na ni serikali ipi iliyowapatia wananchi hao hati miliki?

Ibara ya 2 ya sheria ya barabara ya 1967 inatamka wazi wazi kuwa hifadhi ya barabara zote kuu (trunk roads) hapa nchini itakuwa futi 75 au mita 22.86 kila upande sawa na futi 150 au mita 45 pande zote mbaiuli. Ibara ya 27 ya kanuni za sheria ya barabara ya 2007 zilizopitishwa kupita tangazo la serikai na 21 la tar 23 januari 2009 inatamka kuwa upana wa chini kabisa wa "lane" moja ya barabara kuu hapa nchin utakuwa si chini ya ni mita 3.25. Hivyo eneo la hifadhi ya barabara la mita 45 lina uwezo wa kuzalisha lane 14; lane 7 za kwenda upande mmoja na lane 7 za kwenda upande mwingine. Nitajie barabar gani hapa nchini imewahi kutumia na kumaliza upana huo uliotengwa kiasi cha magafuli kuwavamia watu walioko mita 120 kutoka katakati ya barabara? Hivyo ni propaganda kudai kuwa msongamano wa magari unasababsihwa na watu kujenga katika hifadhi ya barabara.

Kifungu cha 15 na 16 cha sheria ya aradhi namba 5 ya 1999 vinatamka kuwa ugawaji wa ardhi uliofanyikia wakati wa operesheni vijiji ni halali (soma attachement) hivyo sheria ya barabara ya 1967 anayotumia magufuli mwaka 2001 hadi 2010 imeshafutika na haiapo kabisa. Maaufuli anatakiwa kwanza kujenga lane 14 katika hifadhi ya barabara iliyopo ndipo aje kuwaingilia walioko nje ya eneo hilo. Kwa hali hii utagundua kuwa mambo anayoyafanya magufuli ni matokeo ya kukurupuka kwake katika yote hamshirikishi ofisi ya waziri mku, wizara zingine, ngazi za mkoa, wilaya, manispaa, serikali za mitaa
Jatropha nimekuelewa vizuri lakini kama na wewe umenielewa ugomvi wangu ni kwa waziri mkuu kutamka hivyo hadharani, haoni kwamba hata wale ambao walisitisha ujenzi maeneo husika wataendelea kwa kuwa wameruhusiwa kufanya hivyo.

Na kitu kiinge angemwita ofisini amweleze bwana hili unalofanya litatugharimu, ili wananchi tubaki tunajua kwamba kujenga kwenye hifadhi ya barabara ni kosa, lakini walojenga kwa hizo sheria za zamani wasibomolewe.

Halafu naamini Magufuli sio mbumbumbu wa sheria kiasi hiki, nadhani anafahamu anachokifanya, incidencies za makosa zipo unapotekeleza majukumu yako. Mimi nadhani Magufuli aendelee kusimamia sheria hata kama waathirika wa usimamizi wake wataendelea kumpinga akiwemo PM Pinda.
 
ndiyo maana inasemwa siku zote - ni vigumu kuwa mwadilifu ndani ya serikali isiyo na uadilifu. hao akina magufuli, sita, mwakyembe hawawezi kuwa effective ndani ya serikali ya chama cha sasa.

uadilifu gani unaouzungumzia wewe"? Ni kule kuuza nyumba za serikali kwa bei poa na zingine kuwagawia mahawara zake? Acha kuwa juha. Magufuli ni mtu mbabe wala hafuatia sheria hata kidogo.
 
Wazee nimesikia kwenye taarifa ya habari usiku huu kupitia RFA kwamba Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesitisha ubomoaji wa majengo yaliyojengwa ndani ya hifadhi ya barabara nchini kote. Najua ubomoaji huo ulikuwa unafanywa kwa amri ya Mhe. Pombe Magufuli. Hii amri ya Pinda, imekaaje wazee? Au ndiyo mwendelezo wa tabia ile ile ya serikali yetu ya sasa ambapo kila kiongozi anafanya kazi na kutoa statements kadri anavyojisikia? Mhe. Magufuli atajisikiaje?

Kwaheshima na uungwana Mgufuli jiudhulu wachie wafanye wanavyotaka.
 
Pinda kasema aache au asimamishe kwa muda? Je mnyika na watu wake wa bigbrother kwanini wanapanga kwenda kwa waziri mkuu kwa kile mnyika kupitia blog yake anasema kudai maslahi yao kwa kutumia nguvu ya umma? Boamoa bomoa lazima iambatane na malipo na taarifa za awali before kubomoa. Magufuli ataendelea na ubomoaji wa majengo ambayo yameshafanyiwa tathmini na kulipwa na siyo yale ambayo bado kufanyiwa tathmini.

Swala hili lisifanywe propaganda, magufuli kuhamia chadema haimaanishi ndiyo atakua mtu tofauti ndugu zangu. Cha msingi in building the this nation is kumshawishi PM amwandikie magufuli na siyo kuwaambia wananchi kuwa wamemuomba asitishe ubomoaji, hata hivyo kama ni ombi linaweza kukubaliwa au kukataliwa. Tuache masiasa kwenye hot agenda. Napolioni wa Ufaransa aliitwa dictata na mla rushwa na chama chake mwenyewe pale alipoamua kuijenga upya paris, alibomoa majengo kwa lazima bila malipo baada ya kuwataka watu wahamie kwenye majengo ya serikali wakakataa kwa muda wa mwaka mmoja baada ya hapo jamaa aliikata paris katikati na kupata barabara zilizonyooka na kuijenga kama inavyoonekana sasa.


Kwa taarifa yenu magufuli hataki huo urais mnaousema anajua una majungu ya hapa na pale.
 
jatropha nimekuelewa vizuri lakini kama na wewe umenielewa ugomvi wangu ni kwa waziri mkuu kutamka hivyo hadharani, haoni kwamba hata wale ambao walisitisha ujenzi maeneo husika wataendelea kwa kuwa wameruhusiwa kufanya hivyo.

Na kitu kiinge angemwita ofisini amweleze bwana hili unalofanya litatugharimu, ili wananchi tubaki tunajua kwamba kujenga kwenye hifadhi ya barabara ni kosa, lakini walojenga kwa hizo sheria za zamani wasibomolewe.


Halafu naamini magufuli sio mbumbumbu wa sheria kiasi hiki, nadhani anafahamu anachokifanya, incidencies za makosa zipo unapotekeleza majukumu yako. Mimi nadhani magufuli aendelee kusimamia sheria hata kama waathirika wa usimamizi wake wataendelea kumpinga akiwemo pm pinda.

kwa hakika magufuli maeidhalilisha sana ccm, ccm inajivunia sana sera ya kila kta kuwa na sekondari. Lowasaa alipotaka kutimiza lengo hilo aliwaitia wakuu wa mikoa, wilaya,ameya na wakurugenzi wa halmashauri akawapaq agizo na kuwataka kubuni mbinu za kutekeleza agizo hilo. Ndipo halamashauri nyingi zikabuni vyanzo mbali mbali vya mapato ikiwemo mabango ya matangazo na kufanikiwa kutekelza maagizo ya kila kata kuwa na sekondari. Leo hii watoto wapo mashuleni wanahaudumiwa na halamshauri za miji na wilaya kwa kiwango kikubwa sana; leo hii magufuli nakurupuka na kuua chianzo kikuu cha mapato ya halamshuri hizi yaani mabango ya matangazo kwa kisingizio kuwa eti yanasababisha ajali. Ibara ya 9 ya kanuni anazotumia zinztaka tanroad iondoe magari yanayoharibika na kutelkekezw barabarani kwa zaid ya masaa 6 mijini na 24 vijijini.

Hivi kati ya mabango yaliyoko katika hifadhi za barabara na magari yanayotelekezwa barabarani ni kipi kibachosababisha ajali za barabarani., vifo na majeruhi? Huoni kuwa magufuli hutumia propaganda kufanikisha malengo yake? Akati serikali ya ccm inajaipanga kujenga nyumba za waalimu na maabara katika shule hizi, huyu mbabe anahujumu mapato ya halamashauri kiasi hiki. Kwanini hakumshirikisha waziri mkuu? Kwanini hakushiriki tamisemi? Kwanini hakushirikisha halamashuri zinazohusika?

Magufuli ni mabae hivyo amemfikisha pinda kwenye kona, na akalazimika kumkumbusha terms of reference za uwziri wake. Magufuli nafahamu fika kuwa hivi sasa hakuna mtu yeyote anayajenga kwenye hifadhi ya barabara, majengo yote unayoyaona yakijengwa hapo ni kwa kibali cha tamnroad kuwa wakitaka kutumia eneo hilo watabomoa bila fidia unaweka sahihi ofisin. Lakini kwa kuwa ni mbabe anataka kuwa displace mpaka wote wa zamani, ni lazima tukubali kuwa magufuli hakutumia busara.

Tatizo lake ni kuitia serikali hasara kwa kulipa fidia, tazama mabilioni yaliyolipwa kweny zile samaki, badala ya kuhudumia watoto mashuleni.
 
kwaheshima na uungwana mgufuli jiudhulu wachie wafanye wanavyotaka.

kwa kweli kwa kuwa mpaka leo wapo mawaziri wanaolipiwa hotelin kutokea desemba 2010 walipoteuliwa, magufuli natakiwa kujiuzulu kwa kuuza nyumba za serikali kiubabe na kuingiza uifisadi wa kutisha katika zoezi hilo ambalo sasa ilnalitia taifa hasara.
 
huyu pinda anajaribu kulaghai hasira za wananchi tu hakuna lolote hapo.wanajua wananchi wana hasira na serikali yao na hayo ameyaongea kule bukoba unategemea nini. angekuwa na busara angemwita magufuri wakae chini waone nini cha kufanya then anmwachia maghfuri mwenyewe atangaze kubadilisha maamuzi mpk itakapotangazwa tena. kamdhalilisha waziri wake tu kwa kuonyesha kwamba bomoa bomoa yake haiona baraka ya mabosi wake, kuanzia sasa mawaziri hawataweza tena kufanya maamuzi magumu na nchi ndio itakwenda kubaya mpaka tutajuta, tusubiri tuone. Mambo mengine nchi hii yanatia hasira jamani, natamani kujilipua katikati ya kikao cha baraza la mawaziri akiwepo raisi mwenyekiti wao tuunde serikali mpya, mbwa hawa wanachezea maisha yetu na ya vizazi vyetu vijavyo.
 
Waathirika wa bomoa bomoa ya mhe magufuli kuanzia kiruvia, kibamba, kwembe, mbezi, kimara, ubungo, ubungo maziwa, mabibo, kigogo, manzese n.k walikuwa wafanye maandamano makubwa kufuata majibu ya barua mbali mbali za malalamiko walizoiandikia serikali kuhusu nyumba zenye hati miliki kuwekea alama za "x bomoa", wananchi waliohamishiwa katika vilivyokuwa vijiji vya ujamaa kando kando ya barabara ya morogoro kuwekea alama za "x bomoa" kinyume cha sheria n.k.

Maandamano hayo ambayo yalikuwa yaongozwe na mhe john mnyika mbunge wa jimbo la ubungo yalikuwa yafanyike katikati ya machi 2011 mara tu baada ya mhe mizengo pinda waziri mkuu kurejea kutoka ziara ya kanda ya ziwa.

Ibara ya 2 ya kanuni za sheria ya barabara ya 1967 inatamka kuwa hifadhi ya barabara katika barabara zote kuu hapa nchini itakuwa ni futi 75 tu kila upande wa barabara. Hivyo kuwa kitendo cha mhe john magufuli kuagiza mawe ya na mabango yanayoonyesha mwisho wa hifadhi ya barabara kuwekwa mita 120 kutoka katika ya barabara kila upande mwaka 2001; na kufuatiwa na nyumba zilizopo ndani ya eneo hilo kuwelea alama za "x bomoa" mwak 2010 vimechngia kwa kiwango kikubwa sana kushamirisha umaskini wa wakazi wa maeno haya tofauyti kabisa na maeno mengine ziliko pita barabara kuu kama vile barabara ya bagamoyo, kilwa n.k. Aidha nafasi za ajira, kijiaijiri na kujikimu kimiaisha viliathirika sana kwa ubabe wa magufuli katika maeno kati ya ubungo hadi kiruvia.

Kwa sababu hiyo maandamano hayo yalikuwa yalkitegemewa pia kubeba ujumbe wa watu katika eneo hili kukosa nafasi za ajira, kujiajiri na kujikimu kimaisha kutokana na vitendo vya kibabe vya magufuli.

Inashangaza sana kuona kuwa maeneo kama mbagala unapata huduma za kibenki, atm n.k lakini kati ya ubungo hadi kiruvia hauwezi kupata huduma kama hizo kutokana na ubabe wa magufuli, maeneo haya yamebaki kuwa kama vijiji, mabenki na miradi mingine mikubwa mikubwa imeshindwa kutumia majengo yaliyopo kama vile jengo lililopo luguruni park lingefaa kabisa kuweka atm za benki mabali mbali. Je ni ajira kiasi gani zinapotea?
 
CCM na serikali yake wanadhani kuchukiwa kwao na wananchi kunachangiwa na maamuzi magumu kama haya ya Mh Magufuli ya kulinda sheria zilizopo. Hawajiulizi ni Watanzania wangapi wamejenga kwenye hifadhi ya barabara? Maghufuli anaitumikia serikali ambayo haiko hivyo anavyoifikiria.
 
Huwezi jua labda Magufuli alikataa kutii hiyo amri na akampa masharti labda atangaze mwenyewe Pinda. Unajua Magufulu hapendi kuwa kigeugeu, kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa aliambiwa akakataa sababu kubomoa ni kutii sheria na Magufuli ni mtii sheria siku zote kwa hiyo hawezi kupindisha sheria kisiasa kama Pinda.

Pinda ni mwanasiasa wa kigeugeu tu ili mradi asimuumize mtu, anataka asilaumiwe, hatuna waziri mkuu hapo.

.
Hivi bunge haliwezi kufanya namna wamrudishie Lowasa nafasi yake?
Maana tukisubiri mpaka chadema watakapochukua nchi 2015 tutakuwa hatuna sheria hata moja iliobakia kuheshimiwa na serikali ya Jk.
.
 
huyu pinda anajaribu kulaghai hasira za wananchi tu hakuna lolote hapo.wanajua wananchi wana hasira na serikali yao na hayo ameyaongea kule bukoba unategemea nini. angekuwa na busara angemwita magufuri wakae chini waone nini cha kufanya then anmwachia maghfuri mwenyewe atangaze kubadilisha maamuzi mpk itakapotangazwa tena. kamdhalilisha waziri wake tu kwa kuonyesha kwamba bomoa bomoa yake haiona baraka ya mabosi wake, kuanzia sasa mawaziri hawataweza tena kufanya maamuzi magumu na nchi ndio itakwenda kubaya mpaka tutajuta, tusubiri tuone. Mambo mengine nchi hii yanatia hasira jamani, natamani kujilipua katikati ya kikao cha baraza la mawaziri akiwepo raisi mwenyekiti wao tuunde serikali mpya, mbwa hawa wanachezea maisha yetu na ya vizazi vyetu vijavyo.

SUALA HILO LILIKWISHATOLEWA MAAAGIZO NA MAWAZIRI WAKUU WAWILI YANI LOWASSA MA PINDA MWENYEWE, KWA KUWA WENGI WA WANANCHI HAO WAMEJENGA HAPO KWA MAKOSA YA SERIKALI YENYEWE KUWAHAMISHIA KATIKA AMENOE HAYO, HIVYO SUALA HILO LITASHUGHULIKIWA CASE BY CASE, YAANI INAPOTAKA KUJENGWA BARABARA FULANI WAATHIRIKA WA HAPO NDIPO WANAPOGUSWA. IWEJE TENA MAGUFULI AKIUKE MAAGIZO YA MAWAZIRI WAKUU WAWILI, NA AANZISHE TAFRANI NCHI NZIMA? YEYE KAMA NANI? KAMA AMBAVYO PINDA ALIVYOWAAMBIA ZANZIBAR SIO NCHI BILA KUMUNG'UNYA MANENO HADI WAKAKUMBUKA KUBADILI KATIA ILI ITAMKE KUWA ZBR NI NCHI NDIVYO ALIVYOMUAMBIA MAGUFULI KUWA KATIKA MAMBOA YANAYOGUSA WANANCHI WENGI HUSUSAN WATU KUKOSA MAKAZI NI LAZIMA SERIKALI YOTE IJUE NA KUBARIKI SIO MTU MMOJA.

NATAKA WOTE MKUMBUKE KUWA PINDA NI MWANASHERIA BY PROFESSION, SIO KAMA MAGUFULI AMBAYE KWA SHERIA NI LAYMAN, HIVYO PINDA ANATAMBUA MAMBO YAFUATAYO

Human Rights and Freedom from Forced Eviction

What is the Human Right to Freedom from Forced Eviction?

The practice of forced eviction -- the involuntary removal of persons, families and groups from their homes and communities -- exacerbates global problems of inadequate housing and homelessness. Forced evictions are human rights violations! Reinforcing the right to housing and freedom from forced evictions are universal human rights standards defined in the Universal Declaration of Human Rights, CEDAW, the International Covenants and other widely adhered to international human rights treaties and Declarations -- powerful tools that must be put to use in realizing the human right to freedom from forced evictions!

The Human Rights at Issue

The human right of all persons to freedom from forced evictions includes:

* The human right to adequate housing.

* The human right to an adequate standard of living.

* The human right to security, including enforceable legal security of tenure.

* The human right to protection from forced evictions and the destruction and/or demolition of one¹s home including in situations of military occupation, international and civil armed conflict, establishment and construction of alien settlements, population transfer, development projects and international events.

* The human right to freedom of expression.

* The human right to freedom of association.

* The human right to education and access to information.

* The human right to participate in public decision-making.

* The human right to freedom from discrimination based on sex, race, or any other status.

* The human right to equal protection of the law and to judicial remedy in case of violation of the right to protection from forced eviction.

* The human right to choose one's residence, to determine where and how to live, and to freedom of movement.

* The human right to livelihood and land.

* The human right to freedom from arbitrary interference with one's privacy.

* The human right to access to safe drinking water and sanitation.

* The human right to the highest attainable standard of physical and mental health.

* The human right to a safe and healthy environment.

* The human right to access to resources, including energy for cooking, heating, and lighting.

* The human right of access to basic services, schools, transportation and employment options.

* The human right of the child to an environment appropriate for physical and mental development.

Article 25 OF THE Universal Declaration of Human Rights STATES THAT-"Everyone has the right to a standard of living adequate for the health and well-being of himself and his family, including food, clothing, housing and medical care and necessary social services, and the right to security in the event of unemployment, sickness, disability, widowhood, old age or other lack of livelihood...."

Article 11 OF THE Article 11 STATE THAT "The States Parties ...(TANZANIA) recognize the right of everyone to an adequate standard of living for himself and his family, including adequate food, clothing and housing, and to the continuous improvement of living conditions...."

Article 27 OF THE Convention on the Rights of the Child STATES THAT States Parties (TANZANIA) recognize the right of every child to a standard of living adequate for the child¹s physical, mental, spiritual, moral and social development.... States Parties ... shall take appropriate measures to assist parents and others responsible for the child to implement this right and shall in case of need provide material assistance and support ..., particularly with regard to nutrition, clothing and housing."

HIVYO TUSIMUONE PINDA MBUMBUMBU MAWZZIRI WAKUU WALIMWAGIZA MAGUFULI AENDE CASE BYA CASE ILIKUKWEPA WANTON CREATION OF HOMELESSNES AMBYO NI UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU HUSUSAN KWA KUWA SERIKALI NDIO LIWAHAMISHIWA WENGI WA WANANCHI HAO KATIKA MAENO HAYO WAKATI WA OPERESHENI VIJIJI.
 
Nilikwisha sema Magufuri ni Mpumbavu in Myt. Hatukumwajili kubomoa nyumba za Watu huo siyo ujenzi wa barabara, kama hana wataalam aseme jana nilikuwa napinga hoja na Engineer mmoja feki humu juu ya Jengo la Tanesco, nilishangaa sana kuona mtu anasema ni engineer halafu hajui umuhimu wa majengo mijini.
 
Back
Top Bottom