Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,434
- 113,444
Waziri Mkuu Mizengo Pinda apangua hoja KM wa CCM kuwa yeye ni mzigo!.
Upanguzi huo umefanyika bungeni leo asubuhi wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, ambapo aliulizwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM Abrahman Kinana amenukuliwa na media akisema baadhi ya mawaziri akiwemo Mhe. Pinda ni mzigo!, jee yeye anazichukuliaje kauli hizo?.
Pinda alijibu kuwa na yeye amesikia kwenye media na kwa sasa Kinana bado yuko safarini akirejea watakaa naye na kumuuliza alimaanisha nini?.
Ila akesema Waziri Mkuu amesema yeye anasimamia wizara zaidi ya 20, inapotokea wizara 2 ndizo hazifanyi vizuri, sio kumtendea haki Waziri Mkuu kumuita ni mzigo kwa makosa ya wizara mbili huku nyingine nyingi zikifanya vizuri!.
Ila pia amekiri baadhi ya hoja ni mitazamo binafsi dhidi ya Pinda, alitegemea kama kuna hoja za msingi wangekaa naye na kumweleza mapungufu yake ni haya haya na haya, kudai tuu kuwa Waziri Mkuu ni mzigo sio kumtendea haki!, na yeye ni binadamu tuu kama wengine udhaifu ni ubinaadamu!.
Pia amesisitiza kuwa nafasi hiyo hakuomba, ameangaliwa akaonekana anafaa!. Iwapo alionekana anafaa lakini utendaji wake ukawa ni kweli hauridhishi, mamlaka yake ya uteuzi ukijiridhisha hafai, atampumzisha na kusema ukweli majukumu mengine ni mazito ukipumzishwa unashukuru Mungu!.
My Take.
Kwa maoni yangu, Mizengo Pinda anaonewa bure!. Kosa lake kubwa kuwa humble na down to earth!. Watu walimtaraji aonyeshe utendaji kwa kasi zaidi ya mtangulizi wake. Yaani watu walitaraji aonyeshe utendaji zaidi ya Edward Lowassa anything less than Lowassaism then anaonekana anapwaya!. Huku sio kumtendea haki hata kidogo!.
Nimetokea kumfahamu the real Mizengo Kayanza Peter Pinda in reality, he is one of the very few Tanzanzanians that can make the best president this nation has ever had!. Kwa vile ndani ya CCM hakuna utaratibu to pick the best, then there is no chance this country will ever have the best president in foreseeable near future!, tena kule upande wa pili ndio msiseme kabisa!, ni majanga tupu!.
Pasco
Upanguzi huo umefanyika bungeni leo asubuhi wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, ambapo aliulizwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM Abrahman Kinana amenukuliwa na media akisema baadhi ya mawaziri akiwemo Mhe. Pinda ni mzigo!, jee yeye anazichukuliaje kauli hizo?.
Pinda alijibu kuwa na yeye amesikia kwenye media na kwa sasa Kinana bado yuko safarini akirejea watakaa naye na kumuuliza alimaanisha nini?.
Ila akesema Waziri Mkuu amesema yeye anasimamia wizara zaidi ya 20, inapotokea wizara 2 ndizo hazifanyi vizuri, sio kumtendea haki Waziri Mkuu kumuita ni mzigo kwa makosa ya wizara mbili huku nyingine nyingi zikifanya vizuri!.
Ila pia amekiri baadhi ya hoja ni mitazamo binafsi dhidi ya Pinda, alitegemea kama kuna hoja za msingi wangekaa naye na kumweleza mapungufu yake ni haya haya na haya, kudai tuu kuwa Waziri Mkuu ni mzigo sio kumtendea haki!, na yeye ni binadamu tuu kama wengine udhaifu ni ubinaadamu!.
Pia amesisitiza kuwa nafasi hiyo hakuomba, ameangaliwa akaonekana anafaa!. Iwapo alionekana anafaa lakini utendaji wake ukawa ni kweli hauridhishi, mamlaka yake ya uteuzi ukijiridhisha hafai, atampumzisha na kusema ukweli majukumu mengine ni mazito ukipumzishwa unashukuru Mungu!.
My Take.
Kwa maoni yangu, Mizengo Pinda anaonewa bure!. Kosa lake kubwa kuwa humble na down to earth!. Watu walimtaraji aonyeshe utendaji kwa kasi zaidi ya mtangulizi wake. Yaani watu walitaraji aonyeshe utendaji zaidi ya Edward Lowassa anything less than Lowassaism then anaonekana anapwaya!. Huku sio kumtendea haki hata kidogo!.
Nimetokea kumfahamu the real Mizengo Kayanza Peter Pinda in reality, he is one of the very few Tanzanzanians that can make the best president this nation has ever had!. Kwa vile ndani ya CCM hakuna utaratibu to pick the best, then there is no chance this country will ever have the best president in foreseeable near future!, tena kule upande wa pili ndio msiseme kabisa!, ni majanga tupu!.
Pasco