Waziri Mkuu Pinda ageuka mbogo Dodoma-Na dharau juu

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Waziri Mkuu Pinda ageuka mbogo Dodoma
Ma Michael Uledi, Dodoma

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewajia juu wananchi waliolipwa fidia maeneo ya viwanja vilivyochukuliwa na Chuo Kikuu cha Dodoma,akitaka waondoke mara moja.


Pinda alisema, malipo yaliyofanywa yanatosha na watakaokaidi kuondoka wakamatwe na kufikishwa mahakamani.


Pia, alitaka viongozi wa siasa kuacha tabia ya kutetea wanachi hao kwa sababu, umuhimu wa Chuo Kikuu cha Dodoma kwa maslahi ya nchi ni mkubwa, ikilinganishwa na kura chache za wananchi wa eneo hilo.

Kutokana na hali hiyo, Pinda aliagiza uongozi wa mkoa kukamata wananchi wote watakaobainika kuwa, wanataka kuchelewesha ujenzi wa chuo.


Akikagua ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma juzi, Waziri Mkuu alitoa wito kwa makandarasi kutimiza wajibu wao na kuzingatia ratiba ya ujenzi.


Alitaka kampuni zinazojenga chuo hicho kuhakikisha zinatenda haki kwa wafanyakazi wake, ili kazi hiyo iwe na tija

na kusisitiza kusiwepo ulaliaji kwani, mchango wao ni mkubwa.


Waziri mkuu alipongeza Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa kazi kubwa inayofanya hususan kuimarisha elimu nchini, huku akitaka viongozi wake kuhakikisha wanapokamilisha ujenzi na kukabidhi, yawe yamekamilika na vifaa vyake.


Alishauri ujenzi huo kuzingatia umuhimu wa kuwekeza katika miundombinu ya burudani, ikiwemo viwanja vya michezo, maeneo ya maduka na huduma za vinywaji. Chuo hicho kikikamilika kinatarajia kuchukua wanafunzi 40,000.


Kuhusu viwanja vya ujenzi Manispaa ya Dodoma, Pinda alisema, serikali itabidi kuwezesha Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA), kwa ajili ya viwanja kama ilivyofanyika kwa Jiji la Dar es Salaam.


Akimkaribisha Pinda, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Profesa Idrissa Kikula, alibainisha mafanikio mbalimbali yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwake Septemba 10, mwaka jana.


Profesa Kikula alisema, chuo kilianza na wanafunzi 1, 210 na kupungua hadi 1,116 kutokana na baadhi yao kudahiliwa zaidi ya chuo kimoja.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi wa NSSF, Yacub Kidula alisema, NSSF imejiandaa kuhakikisha inakamilisha kila kitu kwa wakati na hivyo imeingia mkataba na asasi nne za ushauri wa majengo ili kuongeza kasi. Hoteli inayojengwa na NSSF inatarajia kuchukua wanafunzi 20,000.
 
..dharau iko wapi? au hilo suala la "kura chache"

..anyways,hivi bongo lazima kila kitu kiwe siasa tu? just wondering.
 
Kuna mtu kaanzisha thread kuwa anataka kuwa rais dikteta wa Tanzania ili alete maendeleo, ndiyo anataka udikteta wa aina hii?

Kama mikataba ya malipo waliyochukua wananchi inawataka waondoke mara moja, kwa kukubali mikataba hiyo na malipo hayo inabidi waondoke mara moja.

Mizengo Pinda alisema yeye si mwanasiasa na kweli katika hili tunaona.Hiyo issue ya kufanya costing kwa kutumia kura sina hakika kama ni yeye amesema au waandishi tu.

Wahindi na Waingereza wanawaonea wivu Wachina kwa sababu Wachina wakitaka kufanya mipango ya maendeleo hawana a bureaucratic democratic system.While the Chinese do not concern themselves with short term voters backlash and because of that, they can ignore short term issues and focus on long term developments (like PM Pinda seems to be doing here, if the report is accurate).Imesemwa kwamba katika muda uliochukuliwa kujenga terminal 5 ya Heathrow wachina wangeweza kujenga Heathrows 5 zilizo na Terminal 5.

Our problems are compounded by not only the transitional nature of our socio-economic settings, but also the commitment of our leaders to long term planning.If Pinda is playing by the book then I totally support him on this.You just do not take compensation and linger around.

But I am not endorsing authoritarianism.Inabidi wote tuheshimu rule of law, tukitaka viongozi wetu waheshimu rule of law na sisi tuheshimu pia.Ndiyo maana narudia kuuliza mkataba wa kuwahamisha ulikubaliwa? Na wote? Uliwapa muda gani kuhama?
 
Roma ilipokuwa inajengwa kulikuwa na consequeces zake ambazo hazikuepukwa ila ndo maendeleo
 
Roma ilipokuwa inajengwa kulikuwa na consequeces zake ambazo hazikuepukwa ila ndo maendeleo

lakini sidhani kama Roma ilipokuwa inajengwa kuna watu walikuwa wanakwiba pesa za Roma na kuzipeleka kwenye mabenki ya Misri na kuyatunza huko. Just a thought
 
Kuna mtu kaanzisha thread kuwa anataka kuwa rais dikteta wa Tanzania ili alete maendeleo, ndiyo anataka udikteta wa aina hii?

Kama mikataba ya malipo waliyochukua wananchi inawataka waondoke mara moja, kwa kukubali mikataba hiyo na malipo hayo inabidi waondoke mara moja.

Mizengo Pinda alisema yeye si mwanasiasa na kweli katika hili tunaona.Hiyo issue ya kufanya costing kwa kutumia kura sina hakika kama ni yeye amesema au waandishi tu.

Wahindi na Waingereza wanawaonea wivu Wachina kwa sababu Wachina wakitaka kufanya mipango ya maendeleo hawana a bureaucratic democratic system.While the Chinese do not concern themselves with short term voters backlash and because of that, they can ignore short term issues and focus on long term developments (like PM Pinda seems to be doing here, if the report is accurate).Imesemwa kwamba katika muda uliochukuliwa kujenga terminal 5 ya Heathrow wachina wangeweza kujenga Heathrows 5 zilizo na Terminal 5.

Our problems are compounded by not only the transitional nature of our socio-economic settings, but also the commitment of our leaders to long term planning.If Pinda is playing by the book then I totally support him on this.You just do not take compensation and linger around.

But I am not endorsing authoritarianism.Inabidi wote tuheshimu rule of law, tukitaka viongozi wetu waheshimu rule of law na sisi tuheshimu pia.Ndiyo maana narudia kuuliza mkataba wa kuwahamisha ulikubaliwa? Na wote? Uliwapa muda gani kuhama?



Pinda anaweza kuonyesha kwamba kwenye hajui siasa ila kuwatetea akina Mkapa na mafisadi wengine akawa karudia siasa.By the way aweje si mwanasiasa na huku ni Mbunge wa Mpanda ?
 
Kueni na ustaarabu kwani si kila kitu kinachofanywa na serikali kinakuwa na kupewa uzito wa kupingwa ,kama wananchi wamelipwa sasa ,fujo la nini ?
Kuna mambo mengine hayajengi isipokuwa yanabomoa na hli ikiwa vyama vya upinzani vitakuwa vinawatomeza wananchi basi havitokuwa vyama vya siasa bali vyama vya fujo na hapo vitaonekana ndio vinapopata nafasi ya kuwatomeza wananchi,tunasema CCM inawafanya wananchi wajinga lakini kwa hili basi vyama vya Upinzani vinawapumbaza wananchi , isiwe vyama vya upinzani vinajichomeka katika sehemu ambazo sheria na makubaliano yamefanywa kati ya serikali na wananchi vitapoteza muelekeo na vitajenga mchezo ambao utakuwa unarudiwa rudiwa hata hapo hivyo vyama vitakapofanikiwa kuongoza nchi ,ni lazima vyama vya upinzani kujenga tokea sasa utamaduni ambao unamfanya mwananchi wa kawaida kufuata sheria na zaidi pale ambapo kuna makubaliano yalikwisha tendeka ,kwa mfano makubaliano ya kamati za CCM na CUF yalikwisha fanyika na kukubali ,CUF hawakukubali tena kurudi mezani kwani mambo yamekwisha ,sasa wananchi wanapokuwa wameshalipwa serikali haiwezi kukubali kurudi na kukaa tena mezani kujadili malipo mengine.
Kama sheria zimefuatwa na malipo yamekwishafanyika wananchi hawana ubavu wa kudai nyongeza na Mh.Pinda atakuwa yupo katika mstari na wanaoleta fujo ni lazima sheria ifuate mkondo ,mambo mengine yanafaa kuepukwa na vyama vya upinzani viwashawishi wananchi kuwa kutokana na malipo waliyokwisha kubaliana nakupewa au kulipwa basi wakubali kuondoka.Sio kung'ang'ania huo sio upinzani unaotakiwa kufanywa.
Yako mambo mengi ambayo wananchi wanahitaji kufahamishwa na kushawishiwa ili kupata nguvu kwa mfano mabadiliko ya katiba na tume za uchaguzi ,huku ndiko upinzani unatakiwa kuelekeza nguvu zao kuliko huko ambako kuna dalili kuwa malipo yamefanywa.
Upinzani ni kuendeleza nchi katika kufuata mkondo wa sheria na utawala bora ,haiwezekani hapo mambo yamekwenda kisheria halafu upinzani unakwenda kuwaambia wananchi wadai haki yao kwani wamedhulumiwa.
 
Kueni na ustaarabu kwani si kila kitu kinachofanywa na serikali kinakuwa na kupewa uzito wa kupingwa ,kama wananchi wamelipwa sasa ,fujo la nini ?
Kuna mambo mengine hayajengi isipokuwa yanabomoa na hli ikiwa vyama vya upinzani vitakuwa vinawatomeza wananchi basi havitokuwa vyama vya siasa bali vyama vya fujo na hapo vitaonekana ndio vinapopata nafasi ya kuwatomeza wananchi,tunasema CCM inawafanya wananchi wajinga lakini kwa hili basi vyama vya Upinzani vinawapumbaza wananchi , isiwe vyama vya upinzani vinajichomeka katika sehemu ambazo sheria na makubaliano yamefanywa kati ya serikali na wananchi vitapoteza muelekeo na vitajenga mchezo ambao utakuwa unarudiwa rudiwa hata hapo hivyo vyama vitakapofanikiwa kuongoza nchi ,ni lazima vyama vya upinzani kujenga tokea sasa utamaduni ambao unamfanya mwananchi wa kawaida kufuata sheria na zaidi pale ambapo kuna makubaliano yalikwisha tendeka ,kwa mfano makubaliano ya kamati za CCM na CUF yalikwisha fanyika na kukubali ,CUF hawakukubali tena kurudi mezani kwani mambo yamekwisha ,sasa wananchi wanapokuwa wameshalipwa serikali haiwezi kukubali kurudi na kukaa tena mezani kujadili malipo mengine.
Kama sheria zimefuatwa na malipo yamekwishafanyika wananchi hawana ubavu wa kudai nyongeza na Mh.Pinda atakuwa yupo katika mstari na wanaoleta fujo ni lazima sheria ifuate mkondo ,mambo mengine yanafaa kuepukwa na vyama vya upinzani viwashawishi wananchi kuwa kutokana na malipo waliyokwisha kubaliana nakupewa au kulipwa basi wakubali kuondoka.Sio kung'ang'ania huo sio upinzani unaotakiwa kufanywa.
Yako mambo mengi ambayo wananchi wanahitaji kufahamishwa na kushawishiwa ili kupata nguvu kwa mfano mabadiliko ya katiba na tume za uchaguzi ,huku ndiko upinzani unatakiwa kuelekeza nguvu zao kuliko huko ambako kuna dalili kuwa malipo yamefanywa.
Upinzani ni kuendeleza nchi katika kufuata mkondo wa sheria na utawala bora ,haiwezekani hapo mambo yamekwenda kisheria halafu upinzani unakwenda kuwaambia wananchi wadai haki yao kwani wamedhulumiwa.

safi sana !!
 
Hakuna dharau hapa.Huu ndio utawala wa sheria tunaotaka.Makubaliano yalifikiwa,serikali ikatekeleza wajibu wake kwa kuwapa fidia yao kufuatia kubomolewa tembe zao.Leo hii wao wanaambiwa watekeleze kwa sehemu,wanaanza kuleta za kuleta.Hapana,hiyo haikubaliki hata kidogo.Nampongeza sana Mh.Waziri Mkuu kwa kwa kutoyumbishwa na vitisho uchwara kwamba kwa kufanya hivyo pengine CCM inajiweka kwenye hatari ya kukosa kura za wananchi hao kwenye chaguzi zifuatazo.Mimi sina tatizo kabisa hata kama ametoa kauli hiyo, kwamba kura zao ni chache kuliko umuhimu wa mradi wenyewe.Huo ndio ukweli,kwani upanuaji wa haraka wa miundo mbinu ya chuo kutaharakisha ongezeko la idadi ya wanafunzi kutoka kila pende ya nchi watakaojiunga na chuo hicho kwa mihula ijayo.Tena mimi nadhani ilikuwa ni jambo la kuipongeza serikali kwamba imeweza kutoa fidia katika kipindi kifupi tangu makubaliano yafikiwe kulinganisha na miaka ya nyuma.Pinda kaza buti maadamu unasimamia haki na utawala wa sheria,watu makini tutakuunga mkono.Achana na hawa watu wachache ambao ni muflisi katika kuhoji mambo huku wakisukumwa zaidi na mitizamo hasi daima.
 
Kueni na ustaarabu kwani si kila kitu kinachofanywa na serikali kinakuwa na kupewa uzito wa kupingwa ,kama wananchi wamelipwa sasa ,fujo la nini ?
Kuna mambo mengine hayajengi isipokuwa yanabomoa na hli ikiwa vyama vya upinzani vitakuwa vinawatomeza wananchi basi havitokuwa vyama vya siasa bali vyama vya fujo na hapo vitaonekana ndio vinapopata nafasi ya kuwatomeza wananchi,tunasema CCM inawafanya wananchi wajinga lakini kwa hili basi vyama vya Upinzani vinawapumbaza wananchi , isiwe vyama vya upinzani vinajichomeka katika sehemu ambazo sheria na makubaliano yamefanywa kati ya serikali na wananchi vitapoteza muelekeo na vitajenga mchezo ambao utakuwa unarudiwa rudiwa hata hapo hivyo vyama vitakapofanikiwa kuongoza nchi ,ni lazima vyama vya upinzani kujenga tokea sasa utamaduni ambao unamfanya mwananchi wa kawaida kufuata sheria na zaidi pale ambapo kuna makubaliano yalikwisha tendeka ,kwa mfano makubaliano ya kamati za CCM na CUF yalikwisha fanyika na kukubali ,CUF hawakukubali tena kurudi mezani kwani mambo yamekwisha ,sasa wananchi wanapokuwa wameshalipwa serikali haiwezi kukubali kurudi na kukaa tena mezani kujadili malipo mengine.
Kama sheria zimefuatwa na malipo yamekwishafanyika wananchi hawana ubavu wa kudai nyongeza na Mh.Pinda atakuwa yupo katika mstari na wanaoleta fujo ni lazima sheria ifuate mkondo ,mambo mengine yanafaa kuepukwa na vyama vya upinzani viwashawishi wananchi kuwa kutokana na malipo waliyokwisha kubaliana nakupewa au kulipwa basi wakubali kuondoka.Sio kung'ang'ania huo sio upinzani unaotakiwa kufanywa.
Yako mambo mengi ambayo wananchi wanahitaji kufahamishwa na kushawishiwa ili kupata nguvu kwa mfano mabadiliko ya katiba na tume za uchaguzi ,huku ndiko upinzani unatakiwa kuelekeza nguvu zao kuliko huko ambako kuna dalili kuwa malipo yamefanywa.
Upinzani ni kuendeleza nchi katika kufuata mkondo wa sheria na utawala bora ,haiwezekani hapo mambo yamekwenda kisheria halafu upinzani unakwenda kuwaambia wananchi wadai haki yao kwani wamedhulumiwa.



Umetoa tuhuma nzito sana kwa Vyama vya Upinzani.Pinda kasema hajali kura chache .Unajuaje kama ni wana CCM wenyewe hapo wana onyeshana ? Dodoma inakaliwa na wa CCM why Upinzani unaingia kwa nguvu hivi ?
 
Nchi yetu nzuri ina eneo kubwa sana ambalo ni mapori tu kama si mashamba, kila mara najiuliza kwanini miradi mikubwa kama hii isifanyike sehemu ambazo hakuna makazi ya watu? There are some of the things you cant buy, you just cant put value to them, chukulia someone who is 80 yrs old na amekaa mahali hapo toka alipozaliwa alafu leo hii unakuja na kicheque chako unamuambia "tunataka kujenga chuo kikuu!" Na in most cases wakati fidia ambazo serekali inatoa kwa wanaohamishwa ni kichekesho, wala hata hawafanyi consultation yoyote na wananchi, wanakaa tu huko mezani na kufanya hizi decisions!
 
..this fool pinda mizengo naona linaleta ubabe wa Lowassa kuachisha watu kazi kwenye majukwaa
 

Kueni na ustaarabu
...kama wananchi wamelipwa sasa ,fujo la nini ?

Kama sheria zimefuatwa na malipo yamekwishafanyika wananchi hawana ubavu wa kudai nyongeza na Mh.Pinda atakuwa yupo katika mstari na wanaoleta fujo ni lazima sheria ifuate mkondo

Na Pinda nae inabidi umsihi awe na ustaarabu.

Waziri Mkuu huwezi hata siku moja kuoanisha masuala ya wananchi na kura zao. Hutoi haki kulingana na kura. Wasiogope kura chache, sasa, kura nyingi ndio waogope? Ni kwa sababu tuko Tanzania ambapo watu hatuelewi Public Relations manake nini. Lakini hili ni bonge moja la public gaffe la Pinda kama kawaida yake. Hutamki maneno kama hayo! Nilikuwa mtoto mdogo sana Malecela alipo haribu kwa maneno kama hayo, kabla Nyerere hajamtosa kutoka kwenye cabinet, na Pinda alikuwa msaidizi wa Rais Ikulu, yabidi akumbuke hivi vitu vizuri zaidi!

Na kama ni kufuata Sheria, Pinda hana mamlaka ya kuamrisha watu waondoke, bali mahakama.

Yani hili ni bonge la gaffe, yani ni kachemsha vibaya mno!

Alitakiwa awasihi kistaarabu tu, kwamba wananchi mmeshalipwa fidia, sheria ichukue mkondo wake, na sio kimabavu mabavu ambayo hata kisheria hana, tena huku anasema hajali vikura vyao vichache. Yani huoni kasoro hapo Ndugu Mwiba?
 
Waziri Mkuu Pinda ageuka mbogo Dodoma
Ma Michael Uledi, Dodoma

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewajia juu wananchi waliolipwa fidia maeneo ya viwanja vilivyochukuliwa na Chuo Kikuu cha Dodoma,akitaka waondoke mara moja.


Pinda alisema, malipo yaliyofanywa yanatosha na watakaokaidi kuondoka wakamatwe na kufikishwa mahakamani.......................

........Kutokana na hali hiyo, Pinda aliagiza uongozi wa mkoa kukamata wananchi wote watakaobainika kuwa, wanataka kuchelewesha ujenzi wa chuo.

Hawo hapo juu ni wanyonge wanapewa amri


Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliliambia Bunge jana wakati akijibu swali la papo kwa hapo kutoka kwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Bw. Hamad Rashid Mohamed (CUF Wawi).

Alisema iwapo kosa hilo litakuwa la jinai hatua za kisheria zitachukuliwa nakama litakuwa la kisiasa litashughulikiwa kisiasa. Katika swali lake, Bw. Hamad alisema Rais wa Awamu ya Tatu alitumia Ikulu kufanya biashara kinyume na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na hivyo akataka kujua kwa nini serikali inapata kigugumizi cha kumfikisha mahakamani kwa kosa hilo.

``Suala hili limeibuka kwa nguvu sana katika siku za hivi karibuni na sisi tunajaribu kuliangalia likoje na tutakapofikia uamuzi tutawajulisha,`` alijibu Waziri Mkuu Pinda.

Kuhusu kumfikisha mahakamani, Bw. Pinda alisema, ``unampeleka mtu mahakamani pale unapokuwa na ushahidi wa kutosha Ni lazima ifike mahali tujiridhishe iwapo suala hilo ni la jinai au la kimaadili,`` alisema. (Ippmedia)

Na hapo juu ankuwa softie na mwanasiasa......double standard

Akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari Dar es Salaam jana, Waziri Mkuu alisema kuibuliwa kwa masuala hayo ya rushwa kwa viongozi na kulazimisha wengine kujiuzulu, ni changamoto kubwa na sasa inabidi mawaziri wawe makini na waangalifu zaidi.

"Hapa mlipotufikisha sasa ni pagumu," alisema Pinda na kuongeza kuwa ingawa masuala mengi ya vitendo vya rushwa yalifanyika katika awamu zilizopita, lakini ni changamoto kwa serikali ya sasa kujitahidi kuhakikisha haiangukii katika mtego wa wengine kutuhumiwa kushiriki vitendo hivyo-----Mgaya Kingoba
Daily News; Monday,May 12, 2008

Ni huyo Pinda tena, mbona sioni akisema hawo mafisadi wakamatwe wapelekwe mahakamani?

Waziri Mkuu Mizengo Pinda ameitaka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kuhakikisha inajisafisha yenyewe dhidi ya ufisadi kuliondolea taifa dosari itakayosababisha kukosa fedha za misaada kwa wahisani wa mataifa ya nje. Aliyasema hayo jana katika ziara yake fupi ya kutembelea makao makuu ya Tume hiyo Dar es Salaam.---- Daily News; Tuesday,June 03, 2008

Jamani huyu PINDA imekuwaje?anpoongea na wanyonge anakuwa mkali lakini akija kwenye watu wanaojilimbikizia vijisenti anakuwa na lugha laini? kulikoni?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom