Waziri Mkuu Majaliwa: Patahitajika umakini mkubwa sana kama itakuwepo haja ya kuigawa TANESCO

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,902
141,845
Waziri mkuu mh Majaliwa Kassim Majaliwa amesema patahitajika umakini mkubwa sana kama itaonekana kuna haja ya kuligawa Shirika la Umeme Tanesco.
===
1644552633188.png

Picha: Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema unahitajika umakini mkubwa sana kama itaonekana kuna haja ya kuligawa Shirika la Umeme nchini (TANESCO).

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo mchana Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Kinondoni, Bw. Abbas Tarimba kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu.

Bw. Tarimba aliuliza ni kwa nini Serikali haioni haja ya kuigawa TANESCO katika makampuni matatu ya kuzalisha, kusafirisha na kugawa umeme kwa vile Shirika hilo hivi sasa limelemewa na kusababisha matatizo ya umeme kila mara.

Akifafanua suala hilo, Waziri Mkuu amesema: “Kutokana na mvua zinazonyesha hivi sasa, maji yako ya kutosha na uzalishaji unaendelea, kwenye gesi uzalishaji unaendelea na hata maeneo mengine kama mafuta, uzalishaji nako pia unaendelea. Changamoto ni miundombinu iliyopo kwenye maeneo haya ya uzalishaji.Tumewapa kazi wafanye utafiti na waone nani atafanya nini.”

Akielezea kuhusu usambazaji wa umeme vijijini, Waziri Mkuu amesema mkakati wa Serikali ya awamu ya sita ni kuhakikisha inapeleka umeme kwenye vijiji vyote ifikapo Desemba, mwaka huu.

Source: Radio One
 
Mamtu yanawazia wizi na kuhujumu taifa tu, ofcourse kunahitajika umakini sn, pole majaliwa uzalendo kwenye taifa hili unajulika. kwa ujinga wetu huu wa kuwaza pesa tu hamna ugawaji utafanyika ukizingatia maslahi ya taifa.

Tutaendelea kuonekana takataka na kukojolewa na wazungu sababu ya akili mbovu za wanasiasa wetu wasiokuwa na maono.
 
Kilichoikuta UDA ndo kinaweza ikuta TANESCO gafla mwekezaji atadai yy ndo anahisa nyingi kuliko serikali na hapo ndo upigaji utaendelea. Akina rostam na akina nyoka ya makengeza akina gemalila na magwiji mengine ili dili wanalingojea kwa hamu sana.
 
Kilichoikuta UDA ndo kinaweza ikuta TANESCO gafla mwekezaji atadai yy ndo anahisa nyingi kuliko serikali na hapo ndo upigaji utaendelea. Akina rostam na akina nyoka ya makengeza akina gemalila na magwiji mengine ili dili wanalingojea kwa hamu sana.
Makamba aliteua bodi mpya ya tanesco, wapambe Kama kawaida wakasema ni mwanzo wa Tanesco mpya kwa kuwa wameteuliwa wafanyabiashara na watu wanaojua biashara. Haya sasa ngoma hiyo imeshawashinda
 
Makamba aliteua bodi mpya ya tanesco, wapambe Kama kawaida wakasema ni mwanzo wa Tanesco mpya kwa kuwa wameteuliwa wafanyabiashara na watu wanaojua biashara. Haya sasa ngoma hiyo imeshawashinda
Ukiwaambia hivyo wanavimbwa na kufura kama chatu aliyemmeza beberu la Zenj. Wanasema sasa ndio wakati uprofeshono umeingia hasa kwenye wizara ya ^knee-shirt-tea!^
 
Hakuna uhitaji wa kuligawa shirika la umeme Tanzania.kinachohitajika kwa sasa ni kwenda na upepo wa dunia masuala ya monopoly kwa sasa hayana nafasi ni kuruhusu kampuni binafsi zenye uwezo kuzalisha umeme.wananchi wanachotakiwa kufanya ni kuchagua kampuni lenye gharama nafuu na lenye umeme wa uhakika
 
Waziri mkuu mh Majaliwa Kassim Majaliwa amesema patahitajika umakini mkubwa sana kama itaonekana kuna haja ya kuligawa Shirika la Umeme Tanesco.

Source: Radio One
Sasa kwani wangegawa bila umakini? Maccm akili zao sijui zikoje
 
Mamtu yanawazia wizi na kuhujumu taifa tu, ofcourse kunahitajika umakini sn, pole majaliwa uzalendo kwenye taifa hili unajulika. kwa ujinga wetu huu wa kuwaza pesa tu hamna ugawaji utafanyika ukizingatia maslahi ya taifa. Tutaendelea kuonekana takataka na kukojolewa na wazungu sababu ya akili mbovu za wanasiasa wetu wasiokuwa na maono.
Nasikia hangaya huko majuu uzunguni kuna mikataba kadhaa atasaini mbele ya hao wazungu. Kwa kweli Mungu atunusuru.
 
Back
Top Bottom