Waziri Mkuu Majaliwa na Katibu Mkuu Dk. Abbas mnapata wapi hii 'Confidence' ya 'Kuwadanganya' Watanzania kuwa itafuzu 2022 FIFA QATAR WORLD CUP?

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Apr 2, 2015
8,011
16,748
Hakuna Watu ambao KEROZENE nawajua vyema ( hasa kwa mbinu na tamaduni zao ) kama akina Bandeko Nangai Wakongo ( zamani Wazaire )

Leo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Katibu Mkuu wa Wizara mpya ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Hassan Abbas mmenishangaza hasa pale mlipofanya Jambo la Kishamba, cha Kipuuzi na kisicho cha Kiufundi cha kwenda na Viti vyenu na Kukaa pembezoni mwa Uwanja mkishuhudia Mazoezi ya Timu ya Taifa ya Tanzania ( Taifa Stars )

Mlichonishangaza zaidi kwa Kutumia Madaraka yenu na Uandamizi wenu mkubwa Serikalini mmeagiza Waganga wengi wa Kienyeji ili waicheze Kishirikina hii Mechi mkisahau kuwa Afrika nzima Makao Makuu ya Uchawi ( Ndumba ) ni Congo DR na Congo Brazaville wakifuatiwa kwa ukaribu na Wanaijeria, Wasenegali, Wakameruni na Waafrika Kusini.

Hongereni Serikali ( hasa Waziri Mkuu Majaliwa na Katibu Mkuu Dk. Abbas ) kwa kufanya na kutengeneza Hamasa ya Kisiasa na Kinafiki zaidi huku mkimdanganya Bibie anayesafiri Cairo na Wamisri Kesho kuwa Tanzania itafuzu 2022 FIFA QATAR WORLD CUP kisha 'mkimpiga' Pesa ambazo mnasema ni za Maandalizi dhidi ya Congo DR na Madagascar kwa Kujiimarisha kwa Ustawi wenu.

Hamtoamini hiyo Alhamisi kwa Mkapa!!!
 
Ukweli ni kuwa, tunashiriki tu mashindano kupata uzoefu kwa mchezaji mmoja mmoja lakini, siioni timu ya Tanzania itakayoweza kufuzu kucheza Kombe la Dunia. Ushauri wangu ni kuelekeza nguvu kwenye soka la watoto kwanza kwa miaka kama kumi hivi ndio tuingie kwenye mashindano.
 
Hakuna Watu ambao KEROZENE nawajua vyema ( hasa kwa mbinu na tamaduni zao ) kama akina Bandeko Nangai Wakongo ( zamani Wazaire )

Leo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Katibu Mkuu wa Wizara mpya ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Hassan Abbas mmenishangaza hasa pale mlipofanya Jambo la Kishamba, cha Kipuuzi na kisicho cha Kiufundi cha kwenda na Viti vyenu na Kukaa pembezoni mwa Uwanja mkishuhudia Mazoezi ya Timu ya Taifa ya Tanzania ( Taifa Stars )

Mlichonishangaza zaidi kwa Kutumia Madaraka yenu na Uandamizi wenu mkubwa Serikalini mmeagiza Waganga wengi wa Kienyeji ili waicheze Kishirikina hii Mechi mkisahau kuwa Afrika nzima Makao Makuu ya Uchawi ( Ndumba ) ni Congo DR na Congo Brazaville wakifuatiwa kwa ukaribu na Wanaijeria, Wasenegali, Wakameruni na Waafrika Kusini.

Hongereni Serikali ( hasa Waziri Mkuu Majaliwa na Katibu Mkuu Dk. Abbas ) kwa kufanya na kutengeneza Hamasa ya Kisiasa na Kinafiki zaidi huku mkimdanganya Bibie anayesafiri Cairo na Wamisri Kesho kuwa Tanzania itafuzu 2022 FIFA QATAR WORLD CUP kisha 'mkimpiga' Pesa ambazo mnasema ni za Maandalizi dhidi ya Congo DR na Madagascar kwa Kujiimarisha kwa Ustawi wenu.

Hamtoamini hiyo Alhamisi kwa Mkapa!!!
Genta una nini wewe?
 
Ukweli ni kuwa, tunashiriki tu mashindano kupata uzoefu kwa mchezaji mmoja mmoja lakini, siioni timu ya Tanzania itakayoweza kufuzu kucheza Kombe la Dunia. Ushauri wangu ni kuelekeza nguvu kwenye soka la watoto kwanza kwa miaka kama kumi hivi ndio tuingie kwenye mashindano.
Ndugu hii post yako kwa jinsi nilivyoipenda na ilivyo nzuri kwani umeandika Ukweli mtupu japo ni Mchungu kwa Wanafiki wengi waliopo Tanzania imetosha kunithibitishia kuwa una IQ Kubwa na nzuri kabisa. Heko Kwako.
 
hahahahaaha unanikumbusha kisa cha Mobutu na ndege nzima ya waganga world cup, halafu wakala goli tisa na Ujerumani...
 
Wazee wa hamasa!!na ukweli wanaujua tu kuwa haiwezekani, hata kufuzu hatua hii, lakini ukisema ukweli utaonekana eti sio mzalendo!!!
 
Back
Top Bottom