Pre GE2025 Waziri Mkuu Majaliwa azindua Stendi ya Sh Bilioni 4.3, Nzega Mjini

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

ESCORT 1

JF-Expert Member
Dec 7, 2015
1,436
3,087
Leo kituo kipya cha mabasi Nzega Mjini mkoani Tabora kimezinduliwa rasmi na Mh Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Ujenzi wa kituo hiki cha mabasi umegharimu shiling Bilion 4.327.

Tabora wamepata stend ya kisasa waitunze sasa

Pia soma Pre GE2025 Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze
IMG_5732.jpeg

MAJALIWA AZINDUA KITUO CHA MABASI NZEGA MJINI

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 13, 2025 amezindua kituo kipya cha Mabasi cha Nzega mjini mkoani Tabora ambacho ujenzi wake umegharimu shilingi bilioni 4.327.

Akizungumza baada ya kuzindua kituo hicho ambacho utekelezaji wake umefikia asilimia 100, Mheshimiwa Majaliwa ameipongeza halmashauri hiyo kwa uamuzi wa ujenzi wa kituo hicho kwani kitaibua fursa za biashara kwa wakazi wa eneo hilo. “Kituo hiki ni kizuri na kimejengwa kwa ubora, kituo hiki kinatakiwa kianze kutumika ili wananchi waanze kunufaika nacho, Watumishi wa halmashauri ongozeni Wana-Nzega kunufaika na fursa katika eneo lenu”

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa halmashauri hiyo kuongeza vibanda vya wafanyabiashara badala ya vichache ambavyo vimejengwa mpaka sasa. “Tunataka wananchi wengi zaidi wanufaike, ongezeni vibanda, huu ni ubunifu mzuri sana utasababisha wengi wanufaike, waleteni wajasiriamali hapa wapate rizki zao, mkifanya hivyo mtaongeza mzunguko wa fedha”

Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali inaendelea na mpango kazi wake wa kuwahudumia watanzania wakati wote, “Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi inaendelea kukamilisha malengo yake katika kuwatumikia watanzania ninajua hatua tuliyoifikia”.

Katika hatua nyingine, Mhehimiwa Majaliwa ametoa wito kwa watumishi wa halmashauri nchini kuendelea kujielekeza katika kutatua changamoto za wananchi “Tumueni mapato yenu ya ndani kutekeleza miradi”

Mheshimiwa Majaliwa anaendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Tabora.
MAJALIWA AZINDUA KITUO CHA MABASI NZEGA MJINI.WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 13, 2025 ...jpg

MAJALIWA AZINDUA KITUO CHA MABASI NZEGA MJINI.WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 13, 2025 ...jpg

MAJALIWA AZINDUA KITUO CHA MABASI NZEGA MJINI.WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 13, 2025 ...jpg

Pia soma ~ Hivi waungwana hii Stendi ya Nzega Mjini ndio ya Sh Bilioni 4 kweli? Au mimi sijui kuthaminisha vitu!
 
Leo kituo kipya cha mabasi Nzega Mjini mkoani Tabora kimezinduliwa rasmi na Mh Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Ujenzi wa kituo hiki cha mabasi umegharimu shiling Bilion 4.327.

Tabora wamepata stend ya kisasa waitunze sasaView attachment 3269102
Daaaa haýo ma frame kubaoo ndio bil hizo zote ? Khaaaaa hayaa wajinga ndio waliwaooo
 
B4? Hapo kwenye picha ni upande wa nyuma wa iyo stend au au?

Em ninyamaze zangu mimi sitaki shida
 
uwanja uliozungushwa fremu ni bilioni 4.Tuacheni utani na yeye waziri mkuu anaitajika veta kusoma ili kutofautisha bilioni na matofali pamoja na vifaa vya ujenzi
🤣🤣🤣 VETA haikwepeki
 

Misemo ya wanafalsafa wa Afrika​

  • “Mpaka simba wawe na wanahistoria wao wenyewe, historia ya uwindaji daima itamtukuza wawindaji.” – Chinua Achebe
  • “Elimu ni silaha yenye nguvu zaidi ambayo unaweza kutumia kubadilisha ulimwengu.” – Nelson Mandela
  • “Mimi sio Mwafrika kwa sababu nilizaliwa Afrika, lakini kwa sababu Afrika ilizaliwa ndani yangu.” – Kwame Nkrumah
  • “Mkono unaozama chini ya chungu utakula konokono mkubwa zaidi.” – Wole Soyinka
  • “Ikiwa hupendi hadithi ya mtu, andika yako mwenyewe”- Chinua Achebe
  • “Tishio kubwa zaidi kwa uhuru ni kutokuwepo kwa ukosoaji.” – Wole Soyinka
  • “Ukitaka kujua nchi, soma waandishi wake.” – Aminatta Forna
  • “Hakuna kitu kisichotulia zaidi kuliko watu wenye mamlaka.” ― Dinaw Mengestu
  • “Hali ya wanawake katika taifa ndiyo kipimo halisi cha maendeleo yake.” – Ngũgĩ wa Thiong’o
  • “Elimu ni pasipoti yetu kwa siku zijazo, kwa maana kesho ni ya watu wanaoitayarisha leo.” – Maulana Karenga
  • “Hisia ni za Kiafrika, sababu ni za Kigiriki.” – Leopold Sedar Senghor
  • “Utukufu mkuu katika kuishi haupo katika kuanguka kamwe, bali katika kuinuka kila tunapoanguka.” – Nelson Mandela
Wewe naye kwenye vitu serious unajaza mamisemo yako yasiyo kichwa wala miguu.
 
Kikubwa hyo stendi ijengwe
Pesa inaweza kuliwa na stendi
Msiione 😄

Ova
 
Back
Top Bottom