mshale21
JF-Expert Member
- Apr 8, 2021
- 2,050
- 4,903
Majaliwa ametoa maelekezo hayo leo Alhamisi Septemba 23, 2021 Moshi mkoani Kilimanjaro wakati wa uzinduzi wa kiwanda cha pombe kali cha Serengeti.
Amesema mawaziri hao wanapaswa kujipanga vizuri kwa kushirikiana na sekta binafsi kuja na mkakati utakaoboresha kilimo nchini.
"Natoa maelekezo kwa mawaziri wa Kilimo, Viwanda na Biashara pamoja na waziri wa uwekezaji wakae pamoja ili kuja na mkakati wa kuhakikisha wakulima wanalima kisasa kwa kutumia teknolojia za kisasa na rahisi."
"Wahakikishe pia wakulima wanapata mbegu bora, pembejeo na kuunganishwa na masoko ya uhakika hapa nchini, kuuza mazao yao kwenye viwanda ambavyo viko tayari kununua mazao yao," amesema.
Amesema kwa kufanya hivyo watawezesha kuongezwa fedha za kigeni na ajira nyingi kwa wananchi sanjari na kuhakikishia wakulima soko la uhakika na lenye bei nzuri.
Amesema mawaziri hao wanapaswa kujipanga vizuri kwa kushirikiana na sekta binafsi kuja na mkakati utakaoboresha kilimo nchini.
"Natoa maelekezo kwa mawaziri wa Kilimo, Viwanda na Biashara pamoja na waziri wa uwekezaji wakae pamoja ili kuja na mkakati wa kuhakikisha wakulima wanalima kisasa kwa kutumia teknolojia za kisasa na rahisi."
"Wahakikishe pia wakulima wanapata mbegu bora, pembejeo na kuunganishwa na masoko ya uhakika hapa nchini, kuuza mazao yao kwenye viwanda ambavyo viko tayari kununua mazao yao," amesema.
Amesema kwa kufanya hivyo watawezesha kuongezwa fedha za kigeni na ajira nyingi kwa wananchi sanjari na kuhakikishia wakulima soko la uhakika na lenye bei nzuri.