KONGAMANO LA WAMACHINGA KITAIFA NA UZINDUZI WA MACHINGA SACCOS
Shirikisho la Wamachinga (SHIUMA) Kwa kushirikiana na Machinga Mkoa wa Dar es salaam wanakukaribisha kushiriki (kufuatilia) Uzinduzi wa Machinga SACCOS utakaofanyika katika kongamano la Kitaifa la Wamachinga.
Saccos ya Wamachinga imelenga kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa Wamachinga ili waweze kujikwamua kiuchumi na kukuza Biashara zao.
Kongamano litahusisha Wamachinga kutoka nchi nzima kupitia wawakilishi wao kutoka kila Mkoa, na litafanyika katika Ukumbi wa PTA - SABASABA, Dar es salaam, Februari 19, 2022 kuanzia Saa Mbili asubuhi (8:00am)
Mgeni Rasmi katika tukio hili anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa.
Kongamano hili limedhaminiwa na Benki ya CRDB.
Shirikisho la Wamachinga (SHIUMA) Kwa kushirikiana na Machinga Mkoa wa Dar es salaam wanakukaribisha kushiriki (kufuatilia) Uzinduzi wa Machinga SACCOS utakaofanyika katika kongamano la Kitaifa la Wamachinga.
Saccos ya Wamachinga imelenga kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa Wamachinga ili waweze kujikwamua kiuchumi na kukuza Biashara zao.
Kongamano litahusisha Wamachinga kutoka nchi nzima kupitia wawakilishi wao kutoka kila Mkoa, na litafanyika katika Ukumbi wa PTA - SABASABA, Dar es salaam, Februari 19, 2022 kuanzia Saa Mbili asubuhi (8:00am)
Mgeni Rasmi katika tukio hili anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa.
Kongamano hili limedhaminiwa na Benki ya CRDB.